Nimekosa mwanaume 'serious'

Subiri malaika atakuja kaa tu na vigezo vyako mume sio mtu wa wakusema unamtaka leo ukampata leo utachezewa mpaka utaona dunia chungu sisi hatutafutwi ni upendo wa dhati moyoni kumbuka nkiwa mume wako ntaaka na wewe mpk kufa sio jambo dogo kama unavyodhani
 
binti kuwa na mitego ya kumvuta mwanaume umtakaye acha kulia... halafu wanaokupenda ndiyo wazuri utajifunza kumpenda .. unayempenda atakusumua mnoo

Naona umekalia ugaidi wa mapenzi wewe mama, teh teh

Hatari sana wewe
 
nina miaka 35
Miaka 35 mtoto wa kike bado unaendelea kuchambua sifa unazotaka hujampata na huku watafunaji wanaedelea kutafuna... Te te te teeh, mkuu ujue mko wengi kiasi ambacho mwanaume anaumiza kichwa, amchukue yupi amuache yupi,... Na wewe unachagua.. Mchaguzi ni mtafutaji na aliye na vingi maana anayo option.
 
Ukitaka mume masikini lkn mwenye upendo WA kweli nipo.
Wewe unamdanganya mwenzio.
Huwezi kupenda chochote bila kukiona/kusikia/kunusa/kupapasa.

Sasa wewe unamwambia mwenzio eti una upendo wa kweli...unamfahamu? Tekeleza masharti ya KUPENDA hapo juu ndio uamue upendo upi utahusika, aidha wa KWELI au wa UONGO maana PENDO zote mbili zipo kwa kila mtu.
 
keshapata huyo!! kama hajapata basi aseme haraka tuendelee kumpa maujanja.
 
Hahahaa nimecheka sana hapa job, kuna mdada tumezoeana nimesoma hii post mbeleyake akasema jaaamaaani huyo yuko kama mimi namimi ni hivyo hivyo daa, wanawake mnaugulia mapenzi moyoni sana, vunja ukimya mwambie tu mtu, by the way kumbe mkowengi wenye shida hiyo.
 
kwanza mkubali anayekufuata hasa kama anakidhi asilimia 50 ya vigezo vyako.. pili jitegeshe maeneo wanaume unao wataka wanapokaa lazima uingie gharama...
Minamshauri asijitegeshe hovyo hovyo, azingatie hiyo 50%, otherwise atakutana na fisi atamlamba fasta alafu yuuule!.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…