Nimekota parcel ina milion 9 ndani na kadi ya benki

Nimekota parcel ina milion 9 ndani na kadi ya benki

Deejay nasmile

JF-Expert Member
Joined
Nov 8, 2011
Posts
5,794
Reaction score
5,352
Yaan hapa nimechanganyikiwa hatari

Nilikuwa natoka natoka hapa mitaa ya mabibo hostel naelekea riverside.mbele kidogo nikaona kifungashio cheusi kando kidogo ya barabara kinaonesha kama kina kitu ndani.watu wanakipita tu, sasa sijui hawakukiona au ndo ubize tu wa mjini.

basi nilipokikaribia bila aibu nikaokota na kuendelea na safari mdogo nikitafuta sehem niangalie kuna nn...basi nikaingia kiduka flan kinauza uza vinywaji kuna ile miavuli ya jua nje..nikakaa nikachungulia ndani nikaona bahasha ya kaki ina nembo ya nmb na kadi ya bank (atm card).

Nikiwa na presha na hofu tele nikaichana ile bahasha ikiwa mule mule ndani ya kifungashio. Daaah!! Nakuta noti kibaoo za elfu 10 ..nikafunga fasta na kuinuka kuelekea upande wa pili kuna baa moja hivi..

nikaingia na kupitiliza moja kwa moja chooni nikajifungia huko na kuanza kuhesabu....ni pesa taslimi milion 9 zilikuwa mule..yaani nilipata kiwewe hatari kilichochanganyika na furaha na sala kama zote yaani.

Ghafla kuna mtu akagonga mlango ule wa chooni..kwa mshituko nikazifunga tena fresh na kutoka nje..ili niangalie utaratibu wa kurudi gheto nikaanze kupanga bajeti sasa.

Ghafla nikashtuka toka usingizini.kumbe nilikuwa nao ta tu ndugu zangu..sasa sijui hii ndoto ina maana gani wakuu...watalaam wa ndoto naombeni mnitafsirie ndoto hii!!
 
Ahahahahaha niliposoma tittle nikawaza kukushauri uende bank na hyo card wakupe jina na mawasiliano ya mwenye kadi kisha aje achukue mzigo wake lkn huku mwisho nikaona unaelekea geto kufanya budget 😂😂😂😂😂😂nimecheka sana.
Ila ndoto za hivi zinakera kuna siku niliota nimeangaika kutoa pesa sijui kwenye nini nikazishika kwa makini nilikaza mkono sana mpaka naamka vidole vinauma kwa jinsi nilivyokua nimekaza mkono kushika ile pesa😂😂😂
 
Ahahahahaha niliposoma tittle nikawaza kukushauri uende bank na hyo card wakupe jina na mawasiliano ya mwenye kadi kisha aje achukue mzigo wake lkn huku mwisho nikaona unaelekea geto kufanya budget 😂😂😂😂😂😂nimecheka sana.
Ila ndoto za hivi zinakera kuna siku niliota nimeangaika kutoa pesa sijui kwenye nini nikazishika kwa makini nilikaza mkono sana mpaka naamka vidole vinauma kwa jinsi nilivyokua nimekaza mkono kushika ile pesa😂😂😂
Hahaha...hivi mkuu kiuhalisia ungefanya hivo kweli...yaan uzipeleke benk tena kumtafuta mwenye nazo???
 
Yaan hapa nimechanganyikiwa hatari

Nilikuwa natoka natoka hapa mitaa ya mabibo hostel naelekea riverside.mbele kidogo nikaona kifungashio cheusi kando kidogo ya barabara kinaonesha kama kina kitu ndani.watu wanakipita tu,sasa sijui hawakukiona au ndo ubize tu wa mjini.

basi nilipokikaribia bila aibu nikaokota na kuendelea na safari mdogo nikitafuta sehem niangalie kuna nn...basi nikaingia kiduka flan kinauza uza vinywaji kuna ile miavuli ya jua nje..nikakaa nikachungulia ndani nikaona bahasha ya kaki ina nembo ya nmb na kadi ya bank (atm card)...
Nikiwa na presha na hofu tele nikaichana ile bahasha ikiwa mule mule ndani ya kifungashio.
Daaah!!nakuta noti kibaoo za elfu 10 ..nikafunga fasta na kuinuka kuelekea upande wa pili kuna baa moja hivi..

nikaingia na kupitiliza moja kwa moja chooni nikajifungia huko na kuanza kuhesabu....ni pesa taslimi milion 9 zilikuwa mule..yaani nilipata kiwewe hatari kilichochanganyika na furaha na sala kama zote yaani.

Ghafla kuna mtu akagonga mlango ule wa chooni..kwa mshituko nikazifunga tena fresh na kutoka nje..ili niangalie utaratibu wa kurudi gheto nikaanze kupanga bajeti sasa.

Ghafla nikashtuka toka usingizini.kumbe nilikuwa nao ta tu ndugu zangu..sasa sijui hii ndoto ina maana gani wakuu...watalaam wa ndoto naombeni mnitafsirie ndoto hii!!
Aise naomba mzigo wangu, ni PM nitakupa zawadi.
 
😴😴😴Me nmeota nmepoteza pesa zilikuwa kwenye baasha ya kaki imewekwa ndani ya kifungashio cheusi, naomba turudi kulala kukamilisha ndoto zetu, nijue kama hzo pesa n zangu or la🙆‍♂️🙆‍♂️🙆‍♂️
 
Yaan hapa nimechanganyikiwa hatari

Nilikuwa natoka natoka hapa mitaa ya mabibo hostel naelekea riverside.mbele kidogo nikaona kifungashio cheusi kando kidogo ya barabara kinaonesha kama kina kitu ndani.watu wanakipita tu, sasa sijui hawakukiona au ndo ubize tu wa mjini.

basi nilipokikaribia bila aibu nikaokota na kuendelea na safari mdogo nikitafuta sehem niangalie kuna nn...basi nikaingia kiduka flan kinauza uza vinywaji kuna ile miavuli ya jua nje..nikakaa nikachungulia ndani nikaona bahasha ya kaki ina nembo ya nmb na kadi ya bank (atm card).

Nikiwa na presha na hofu tele nikaichana ile bahasha ikiwa mule mule ndani ya kifungashio. Daaah!! Nakuta noti kibaoo za elfu 10 ..nikafunga fasta na kuinuka kuelekea upande wa pili kuna baa moja hivi..

nikaingia na kupitiliza moja kwa moja chooni nikajifungia huko na kuanza kuhesabu....ni pesa taslimi milion 9 zilikuwa mule..yaani nilipata kiwewe hatari kilichochanganyika na furaha na sala kama zote yaani.

Ghafla kuna mtu akagonga mlango ule wa chooni..kwa mshituko nikazifunga tena fresh na kutoka nje..ili niangalie utaratibu wa kurudi gheto nikaanze kupanga bajeti sasa.

Ghafla nikashtuka toka usingizini.kumbe nilikuwa nao ta tu ndugu zangu..sasa sijui hii ndoto ina maana gani wakuu...watalaam wa ndoto naombeni mnitafsirie ndoto hii!!
Ndoto za aina hii huchelewi kukojoa kitandani, fanya uamke haraka mkuu😂😂
 
Ni mchawi alikuwa anakuotesha hiyo ndoto ili apate pa kuanzia kukupakua humo humo ndotoni usingestuka mdoto ilikuwa hivi.Yule mchawi angekuotea na hela zake angekuambia ukitaka akuachie zile hela akupakue kwanza najua ungekubali tu mbele ya milioni tisa? Hivyo angekupakua kwa hiari yako mwenyewe na ungechukua hizo milioni tisa,ukiamka ahsubuhi unagundua ni ndoto tu ila kwenye ulimwengu wa kiroho mchawi anakuwa amakukamua kiukweliukweli.Kijana siku nyingine humo ndotoni usipende kuokotaokota kitu
 
Back
Top Bottom