Nimekumbuka mbali sana leo

Kuna wale ambao wanalelewa na ndugu(kaka) sasa kwenye picture anaingia shemeji ndio anaanza tabia za umama wa kambo.
Huyo ni kiherehere tu nae, utamnyanyasaje shemeji wa kiume??

Hamnaga nongwa kabisa
 
Unaongozwa na mihemko unashindwa kuzungumzia uhalisia
 
No thank you wa kwako itakuwa ndo wale mama wa kambo wenye utu ambao ni 1 kati ya 1000

Mama wa kambo wengi ni wakatili mno acha mzee
Muache aelezee mama wa kambo wa kwene tamthilia ila sio wa uhalisia
 
Hatuzungumzii single maza,tunazungumzia mama wa kambo asa kuwapa mimba hao na mada hewani vinahusiana nini
Na wao watakosa malezi ya mzazi mmoja kama ilivyokuwa kuwa kwako, sasa hivi matukio ya baba wa kambo wanao walawiti na kuwabaka wa toto wa kiume na wakike wa wake zao ya mezidi; kwaiyo uhusiano upo hapo wewe umekuwa kipofu hauwoni
 
Si kweli wamama wa zamani eti afadhali inategemea na nafsi ya mtu wapi wa zamani sana roho mbayaaa tena mnoo wa sasa pia wapo waungwanaa....nafsi ya mtu haijalishi umri
Mimi naona wa mama wa kambo wengi wa zamani walikuwa pouwa sana gubu walikuwa nalo dogo: wanao zingua ni hawa waliozaliwa 1980s kuja mbele.
 
Zamani hakukua na mitandao ndo maana walikua hawasikiki tena walikua wakatili wa kutisha mnoooo
 
Nakumbuka toka Thithiemu ipate dereva mpya ani wapendwa mwenzenu nanyanyathika athikwambie mtu
 
nilikua nakaa na mama wa kambo enzi nipo form one siku moja tukatumwa wazazi shule mzee hakuwepo nikamwambia mother huyo wa kambo eti akanijibu kamfukue mama yako kaburini ndo umpeleke huko shuleni kwenu dah! akili yangu akawaga kama kichaa yani kwanzia siku hiyo ilikuani mwendo wa ngumi tu na mama wa kambo chupa,mawe,chuma,kisu hakuna salamu nikiamka nipo tu na mishe zangu yaani mama wa kambo akimgusa tu mdogo wangu mimi huyo nimeibuka ni kasheshe mzee akajaga kumtimua. angebaki mpaka nifike form three ningemuua kabisaaaa...
 
Si kweli wamama wa zamani eti afadhali inategemea na nafsi ya mtu wapi wa zamani sana roho mbayaaa tena mnoo wa sasa pia wapo waungwanaa....nafsi ya mtu haijalishi umri
Hahaha Dada ake kizazi cha sasa mnaji tetea naona sema kuna point ameiongea kapeace nimeielewa sana; ana sema ni ngumu sana kwa mwanamke yeyote wa sasa na wa zamani kumlea mtoto ambae si wake kwa mapenzi Yale kama ambavyo atamlea mtoto wake wa kumzaa.
 
Muulize membe
 
Ha ha


Nakumbuka mama wa kambo alikuwa anapenda sana kumuaminisha baba mimi sina akili basi akiwa anamwambia tu mimi huwa natoa bonge la cheko ha ha ha ha ha ha ha ha

Yaani hadi leo angekuwa ananilea NINGEGONGA MBALI
 
Na wao watakosa malezi ya mzazi mmoja kama ilivyokuwa kuwa kwako, sasa hivi matukio ya baba wa kambo wanao walawiti na kuwabaka wa toto wa kiume na wakike wa wake zao ya mezidi; kwaiyo uhusiano upo hapo wewe umekuwa kipofu hauwoni
Mada hewani ni mama wa kambo

Afu baba wa kambo wene roho kama hizo wachache sana na nafasi ya kufanya hay ni chache sana maana muda mwingi yupo kazini
 
Ifahamike suala la mtu kuchukia mtoto wa mwingine ni la asili maana hata wanyama wengi wapo hivyo.Kinachomsaidia binadamu ni utashi tu. Hivyo, haishangazi mama wa kambo kuonekana hivyo.Hata mababa wengi tu huchukia watoto wa kambo,sema wanaume kwa kulinganisha ni wavumilivu, pia wao hawapo karibu na watoto.Aidha, ndiyo maana kuna kundi kubwa la wanaume hukwepa kuoa mwanamke mwenye watoto, baadhi ya sababu zikiwa eti mtu kashachakazwa na kuwa hawezi kulea watoto wa mwenzake.

Lakini kuna suala ambalo wengi tunakosea, kufikiri mtu akiwa mama wa kambo tu basi ni mbaya. Wakati mwingine wanajamii ndiyo hukuza suala hili. Wasione au kusikia mtoto ameadhibiwa, watasema. Adhabu ileile ambayo angeitoa mama mzazi,akiitoa mama wa kambo ni vita.Mimi nimelelewa na mama wa kambo, lakini si kila jambo baya analokufanyia au kukuudhi anafanya kwakuwa si mwanae, niliona maudhi mengi ni yaleyale anawafanyia wanae kila mtu kwa muda tofauti. Sasa mimi au ndugu zangu tusipokuwa wavumilivu ndipo tunakurupuka na kuanza kuwaka, huyu mama ni binadamu,nae anawaka, awapigie mogoti nyinyi ni nani?

Laiti wanajamii na watoto wangekuzwa kwa kutomuona mama wa kambo ni adui, tatizo lingepungua.Kumaliza haiwezekani, maana ni nature.Hivyo,ninakiri kuishi na wamama wa kambo kuna changamoto,lakini pia huchagizwa na wanajamii. Hii ni sawa na mtu na mawifi au mama mkwe.Maudhi yaleyale ambayo mama mzazi hukufanyia, akifanya mama mkwe anakunyanyasa.Na mkwe ni hivyohivyo,kosa lilelile analokufanyia binti yako wa kuzaa akifanya mkwe, hafai.
 
Watu hawafanani! Wapo wazazi wenye kuwalea watoto wao vizuri, wengine ndo vile tena!
Mara ngapi tunasikia mzazi kamchoma mwane kisa kala mboga?! Wengine hudiriki kuwatupa kabisa watoto wao wa kuwaza!

Hawa wamama wa kambo wapo wazuri na wabaya pia! Ila sababu tushajijengea dhana kwamba hawafai jamii nayo inaamini hivyo!

Binafsi meishi na mama wa kambo, sijawahi kuona ubaya wake! Na mpaka nimekuwa mtu mzima bado tunapendana namheshimu naye ananijali!

Tatizo lilikuwa kwa majirani, na hao ndo wanaowajengea watoto kiburi hawa wanaoishi na mama mlezi! Lakini kwangu mimi hawakufanikiwa, imagine ningejenga chuki nikiwa mdogo sijui kama ningekaa nimpende!

Pole kwa yaliyokukuta Mkuu, la mno uzima upo! Mshukuru Mungu kwa kila jambo!
 
mama angu uyo; mwenyewe
 
Fanya tena udadisi mkuu nini kinafanya uamini hivyo kwa sasa. Najua utandawazi ndio sababu kuu inayofanya mama wa kambo wa sasa waonekane wabaya zaidi kwakuwa tunayaona katika mitandao maovu yao kwa watoto wa kambo kuliko kipindi cha nyuma miaka uliyoitaja wewe lakini binadamu ni yuleyule na roho mbaya yake.
Mimi naona wa mama wa kambo wengi wa zamani walikuwa pouwa sana gubu walikuwa nalo dogo: wanao zingua ni hawa waliozaliwa 1980s kuja mbele.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…