Nimekutana na mama kwenye daladala anatumia JamiiForums

Nimekutana na mama kwenye daladala anatumia JamiiForums

Status
Not open for further replies.
Uzi wa kindest huu, using wa JF ni IDs sio matumizi mimi huficha IDs yangu ila sio matumizi mimi kila mtu wangu wa karibu anayijua JF anajua natumia JF.

Pia kuna watu hata hizo IDs sio siri kwao, kuna jamaa yangu yupo humu alinitajia jina la ID yake na mpaka Leo naona anatumia humu, kuna jamaa jina la ID yake ndio alikuwa anatumia WhatsApp.
 
Wakuu za usiku .

Leo baada ya kutoka kwenye mihangaiko yangu nikaamua kupanda daladala za kwenda Makumbusho.

Sasa siti zilikuwa zimeisha nikaamua kusimama tu, cha kushangaza aliyekuwa amekaa kwenye siti alikuwa anatazama JF😅 nilishtuka na kufurahi pamoja na kushangaa sana 🤣.

Maana kwangu mimi JF ni kama sehemu zangu za siri, hakuna rafiki au ndugu anayenijua kuwa niko humu.

Hata nikitumiaga JF naitumiaga gizani au sehemu isiyokuwa na watu.

Sasa we mama uliyekuwa unakunywa juisi ya miwa na biskuti nakushauri tu ujifunze kujisitiri ndio maana tunatumia fake IDs humu.

Si vyema ukatumia huu mtandao mbele za watu maana huwezi jua nyampara ni nani 💂💂💂🧑‍✈️.

Yangu ni hayo tu wakuu.
Lakini pia inawezekana anatumia huu mtandao kwa kusoma tu taarifa na si member wa JF.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom