Nimekutana na mwanajamiiforum

Nimekutana na mwanajamiiforum

Nishakutana na watatu ila huyu mmoja ilikua historia aisee, tulikutana bila kupeana namba za simu yaan tulichat jf mpaka siku ya miadi tupo online tunawasiliana mpaka tukakutana was so funny,

Me nashangaa watu wanaoogopa kuonana na mtu wa mtandaoni kwa zama hizi za technolojia mbona kawaida sana.
 
Binasfi nishaonana na wangi sana, mpaka unakuja kukumbuka hee kumbe tumejuliana jf

Wateja wangu wazuri sana Wana JF, kwanza hawaliilii kupunguziwa bei nk
 
Asee mi juzi nilikuwa zangu kirai nikawa nimepanda daladala pale ubumgo inayoelekea mbezi nikawa nimesimama!! Kwa mle ndani tulikuwa wengi!!kufika baruti kuna lijamaa likapanda!!haki ya mungu lilikuwa bonge balaa hadi nikamwonea uruma!!sasa kufika korogwe kuna abiria walishuka mimi nikapata siti nikakaa gule bonge akawa amesimama!mi nikajisikia huruma nikaona nimpe tuu ile siti!! Nikamwambia broo njoo ukae hapa!!asee akanishukuru sana akakaa!!laa haula akatoa cm aina ya sony kubwa hivi mi nikawa namcheki tuu anavyohemea juu juu ikaingia j.f mi kiroho kikaanza kudunda jujuu nijue ni nani!! Asee bahati mbaya alikuwa ameshalog in lakini akawa anacoment tuu!asee nilitamani nijue yule ndo nani ila bahati mbaya asee!!!!
Wewe broo uliepanda daladala baruti kuelekea mbezi nikakupa siti pale korogwe juzi j.pili jioni mimi ndo wa stendi niliekupisha ukakaa!!
Ushauri wangu kwako!!! Mkuu kama na wewe uko humu nakushauri upunguze mwili huo kijana bado taifa tunakuhitaji!!!
Hahahaahah,unene ni tatizo kubwa watajihisi kutengwa lakin kiukweli ni mbayaa
 
Back
Top Bottom