Nimekutana na Supermarket ya Wachina mafichoni Dar es Salaam

Nimekutana na Supermarket ya Wachina mafichoni Dar es Salaam

Mkata Mtaa

Senior Member
Joined
Jun 10, 2016
Posts
136
Reaction score
142
Wiki iliyopita nilienda kwenye nyumba moja Mikocheni baada ya kusoma kibao nje, hicho kibao nakifahamu maana mwenye kampuni hiyo zamani nilishafanya nae biashara. Nilipiga honi mlinzi akafungua geti, nikaingiza gari. Akafunga geti, nje nikakutana na mswahili nikamuuliza kama wenyeji wapo, akaniambia wapo ndani, kuna nyumba mbili moja kubwa ya ghorafa mbili na nyingine iko nyuma pembeni ya fibre ya kuunganisha, nikaingia umu nyumba ya pembeni, kuingia tu nikakutana uso kwa uso na wachina 3, wanaume 2 msichana 1, wakashtuka, wanaume wakatoka nje, nikamuuliza msichana mtu fulani yupo? hakujibu, akajifanya hajui kingereza wala kiswahili, baadae akaita mwenzake nikamuuliza, tukawa atuelewani ikabidi nitoa business card kumuonyesha, kanimbia jamaa alisharudi kwao,
cha kushangaza mle ndani tulipokuwa ni supermarket kubwa tu, ina vitu vya China na bei zimeandikwa kichina na ila kuna sehemu digit ni kawaida, nikajifanya naangalia vitu na kuzunguka ndani, lakini hapo hapo naangalia licences zilipotundikwa sikuona, Nilivyoona hili supermaket kwa ajili ya wao tu.
Inakuwaje una supermaket geti limefungwa wakati wote, ata nilipoingia mchina mmoja alimfata mlinzi getini nikaona kama anamgombeza kwa kufunguliwa geti. Sijui kama amepewa onyo au kufukuzwa,
Sijui kama mamlaka husika wanajua kama hiyo supermaket ipo na inalipa kodi stahiki na ipo kihalali,
Na kwa nini wafunge geti wakati wowote, na kibao kilichopo nje ambacho mimi nilikisoma nikajua yule jamaa ndio kahami pale ni tofauti na biashara inayofanyika ndani, maana niliwauliza kama biashara yake anasimamia nani wakaniambia hicho kibao kipo tu akijatolewa tu.
Nawasilisha.
 
wachina wengi tuu wanaishi kihuni huni hapa nchini
 
mkuu waripoti tu..maana nishalipa sana kodi mwaka huu mpaka najisikia uchungu na maumivu
 
bora ungekaa kimya tu maana hujata ni wapi ili ifuatiliwe hiyo supermarket wewe umetoa maelezo yasiyo na msingi
Mkuu nadhani mleta mada anakusudia kushirikisha Jamii ya wana JF ili tupanuane mawazo kisha la maingi lipatikane.hata kama hakutaja ni wapi lakini kupitia JF atachukua hatua stahiki kama mhenga nchi.
Nyamalagala
 
Hiv sio ile aliyoisema yule bonge wa pb Wa clouds fm kipind fulan
 
tuliambiwa wana mahela mengi tu hayana kazi,labda ndio wamekuja kuyatumia mahela yao
 
Mkuu hao waunguze tu. .. Nikiwazia kodi tunazoliwa sisi alaf wao washangweke kimya kimya, ujinga huu
 
Ni bora uparipoti.. maana haisaidii kuileta humu halafu ikaishia juujuu.. kwanza je hao wachina wana vibali halali vya kuishi nchini??
 
Wiki iliyopita nilienda kwenye nyumba moja Mikocheni baada ya kusoma kibao nje, hicho kibao nakifahamu maana mwenye kampuni hiyo zamani nilishafanya nae biashara. Nilipiga honi mlinzi akafungua geti, nikaingiza gari. Akafunga geti, nje nikakutana na mswahili nikamuuliza kama wenyeji wapo, akaniambia wapo ndani, kuna nyumba mbili moja kubwa ya ghorafa mbili na nyingine iko nyuma pembeni ya fibre ya kuunganisha, nikaingia umu nyumba ya pembeni, kuingia tu nikakutana uso kwa uso na wachina 3, wanaume 2 msichana 1, wakashtuka, wanaume wakatoka nje, nikamuuliza msichana mtu fulani yupo? hakujibu, akajifanya hajui kingereza wala kiswahili, baadae akaita mwenzake nikamuuliza, tukawa atuelewani ikabidi nitoa business card kumuonyesha, kanimbia jamaa alisharudi kwao,
cha kushangaza mle ndani tulipokuwa ni supermarket kubwa tu, ina vitu vya China na bei zimeandikwa kichina na ila kuna sehemu digit ni kawaida, nikajifanya naangalia vitu na kuzunguka ndani, lakini hapo hapo naangalia licences zilipotundikwa sikuona, Nilivyoona hili supermaket kwa ajili ya wao tu.
Inakuwaje una supermaket geti limefungwa wakati wote, ata nilipoingia mchina mmoja alimfata mlinzi getini nikaona kama anamgombeza kwa kufunguliwa geti. Sijui kama amepewa onyo au kufukuzwa,
Sijui kama mamlaka husika wanajua kama hiyo supermaket ipo na inalipa kodi stahiki na ipo kihalali,
Na kwa nini wafunge geti wakati wowote, na kibao kilichopo nje ambacho mimi nilikisoma nikajua yule jamaa ndio kahami pale ni tofauti na biashara inayofanyika ndani, maana niliwauliza kama biashara yake anasimamia nani wakaniambia hicho kibao kipo tu akijatolewa tu.
Nawasilisha.

Ni PM mkuu
 
Mkuu nenda ukawaripoti TRA haiwezekani sisi tunanyonywa na hizi kodi lukuki halafu hawa mazombi wakaja kufaidi uku kwetu.
 
Back
Top Bottom