Nimekutana na Supermarket ya Wachina mafichoni Dar es Salaam

Nimekutana na Supermarket ya Wachina mafichoni Dar es Salaam

Wiki iliyopita nilienda kwenye nyumba moja Mikocheni baada ya kusoma kibao nje, hicho kibao nakifahamu maana mwenye kampuni hiyo zamani nilishafanya nae biashara. Nilipiga honi mlinzi akafungua geti, nikaingiza gari. Akafunga geti, nje nikakutana na mswahili nikamuuliza kama wenyeji wapo, akaniambia wapo ndani, kuna nyumba mbili moja kubwa ya ghorafa mbili na nyingine iko nyuma pembeni ya fibre ya kuunganisha, nikaingia umu nyumba ya pembeni, kuingia tu nikakutana uso kwa uso na wachina 3, wanaume 2 msichana 1, wakashtuka, wanaume wakatoka nje, nikamuuliza msichana mtu fulani yupo? hakujibu, akajifanya hajui kingereza wala kiswahili, baadae akaita mwenzake nikamuuliza, tukawa atuelewani ikabidi nitoa business card kumuonyesha, kanimbia jamaa alisharudi kwao,
cha kushangaza mle ndani tulipokuwa ni supermarket kubwa tu, ina vitu vya China na bei zimeandikwa kichina na ila kuna sehemu digit ni kawaida, nikajifanya naangalia vitu na kuzunguka ndani, lakini hapo hapo naangalia licences zilipotundikwa sikuona, Nilivyoona hili supermaket kwa ajili ya wao tu.
Inakuwaje una supermaket geti limefungwa wakati wote, ata nilipoingia mchina mmoja alimfata mlinzi getini nikaona kama anamgombeza kwa kufunguliwa geti. Sijui kama amepewa onyo au kufukuzwa,
Sijui kama mamlaka husika wanajua kama hiyo supermaket ipo na inalipa kodi stahiki na ipo kihalali,
Na kwa nini wafunge geti wakati wowote, na kibao kilichopo nje ambacho mimi nilikisoma nikajua yule jamaa ndio kahami pale ni tofauti na biashara inayofanyika ndani, maana niliwauliza kama biashara yake anasimamia nani wakaniambia hicho kibao kipo tu akijatolewa tu.
Nawasilisha.
Mkuu kwanini usitoe ripoti katika mamlaka husika? At least utakuwa umefanya sehemu yako kama mzalendo!
 
Sio mchina, muarabu, mhindi, mzungu wala yeyote yule kila mtu anatakiwa kulipa kodi na kumfichua asielipa kodi kwa kutumia rasilimali zetu ni kitendo cha uzalendo.

Inawezekana sio kufanya biashara tu labda kuna vitu vingine zaidi wanavyojishughulisha navyo. Tafadhali ukiwa kama mzalendo toa taarifa kwenye vyombo husika.
 
Ipo ikitoka Rose garden kuelekea kwa Mwl Nyerere, baada ya kukata kona na kuvuka tuta la pili kuna kibao kimeandikwa Tanzania China Tourist development Ltd, pale karibu palipokuwa na Office ya TCU,
Ipo umo ndani.
 
nlisikia ukifanikisha kumkamata mkwepa kodi TRA wanakujaza mapesa. tumia fulsa hii
 
Unaweza ukaenda ku report sehemu husika ukashangaa unabaki humo kituoni! ukaanza kufuatiliwa wewe! Mbona zipo biashara na makampuni kibao ya kichina biashara zao za kujificha ficha sana halafu ni waoga!
 
Hawana uwoga, waoga ni wahindi, mchina anaogopa kuwekwa ndani wakati ana uwezo wa kulala site anakojenga, wengine wanazibaziba chumba kimoja wanalala wengine wanalala kwenye container, sasa ata ukimweka ndani haoni tofauti kubwa.
 
Ni bora uparipoti.. maana haisaidii kuileta humu halafu ikaishia juujuu.. kwanza je hao wachina wana vibali halali vya kuishi nchini??
Akaripoti wapi? Ndo swali la msingi. Maana anaweza kuwapa watu fursa...hawa jamaa wa mazoezi ya kawaida mtaani wanaweza kwenda kuanza kuchukua mshiko!! Siwaamini hata kidogo.
 
Ipo ikitoka Rose garden kuelekea kwa Mwl Nyerere, baada ya kukata kona na kuvuka tuta la pili kuna kibao kimeandikwa Tanzania China Tourist development Ltd, pale karibu palipokuwa na Office ya TCU,
Ipo umo ndani.
KaMa ni ipo muda mrefu sana nakumbuka mwaka juzi December nikiwa na watching flani nilimpenda ano nikanunia chai za kichina. Wanauza bidhaa zakichina tuu na wapo full. Aisee ni kuwachoma tuu hamna namna. Ngoja niwasiliane na TRA mwenge kesho asubuhi wakakinukishe
 
Sasa we hapo unataka nini mura kwani ujui kuwa hawa ni wasaidizi wa richama retu rire mura
 
Sasa nawe

Wahusika wa Serikali ikisoma hapa iote ilipo hiyo supermarket???

Siungeweka details kamili hapa???
 
Wiki iliyopita nilienda kwenye nyumba moja Mikocheni baada ya kusoma kibao nje, hicho kibao nakifahamu maana mwenye kampuni hiyo zamani nilishafanya nae biashara. Nilipiga honi mlinzi akafungua geti, nikaingiza gari. Akafunga geti, nje nikakutana na mswahili nikamuuliza kama wenyeji wapo, akaniambia wapo ndani, kuna nyumba mbili moja kubwa ya ghorafa mbili na nyingine iko nyuma pembeni ya fibre ya kuunganisha, nikaingia umu nyumba ya pembeni, kuingia tu nikakutana uso kwa uso na wachina 3, wanaume 2 msichana 1, wakashtuka, wanaume wakatoka nje, nikamuuliza msichana mtu fulani yupo? hakujibu, akajifanya hajui kingereza wala kiswahili, baadae akaita mwenzake nikamuuliza, tukawa atuelewani ikabidi nitoa business card kumuonyesha, kanimbia jamaa alisharudi kwao,
cha kushangaza mle ndani tulipokuwa ni supermarket kubwa tu, ina vitu vya China na bei zimeandikwa kichina na ila kuna sehemu digit ni kawaida, nikajifanya naangalia vitu na kuzunguka ndani, lakini hapo hapo naangalia licences zilipotundikwa sikuona, Nilivyoona hili supermaket kwa ajili ya wao tu.
Inakuwaje una supermaket geti limefungwa wakati wote, ata nilipoingia mchina mmoja alimfata mlinzi getini nikaona kama anamgombeza kwa kufunguliwa geti. Sijui kama amepewa onyo au kufukuzwa,
Sijui kama mamlaka husika wanajua kama hiyo supermaket ipo na inalipa kodi stahiki na ipo kihalali,
Na kwa nini wafunge geti wakati wowote, na kibao kilichopo nje ambacho mimi nilikisoma nikajua yule jamaa ndio kahami pale ni tofauti na biashara inayofanyika ndani, maana niliwauliza kama biashara yake anasimamia nani wakaniambia hicho kibao kipo tu akijatolewa tu.
Nawasilisha.
Hii style ya kutoa taarifa inapaswa uirudishe kule FB.
Huku JF taarifa hutolewa kwa umakini zaidi, uwazi zaidi na ujasiri zaidi.
Kwa JF hii sio taarifa ni majungu.
 
Back
Top Bottom