Nimekuwa mtu wa kuumizwa, kutopewa thamani na kusalitiwa kwa wale wote niliowaamini na kuwapenda

Nimekuwa mtu wa kuumizwa, kutopewa thamani na kusalitiwa kwa wale wote niliowaamini na kuwapenda

Habarini ndugu zangu. Niende Moja kwa Moja kwenye mada. Maisha ya mwanadamu ni mjumuisho wa vitu vingi sana, tunapambana Kila kukicha kuhakikisha tunakuwa Bora zaidi ya tulivyokuwa Jana.

Lakini kwa sasa kwangu hii imekuwa tofauti. Najua wengi tunapitia changamoto lakini tunapambana na kuzishinda.

Kwenye maisha yangu, nimekuwa nikipambana kama wafanyavyo wengine lakini changamoto ninazopitia kwa sasa hazihusiana kabisa na mali... Bali ni mahusiano kwa wanaonizunguka, nimekuwa mtu wa kuumizwa, kutopewa thamani na kusalitiwa kwa wale wote nilio waamini na kuwapenda.

Sina furaha Wala sioni tumaini, sioni umuhimu Tena wa Mimi kuwepo katika ulimwengu huu.

Maisha yangu mwenyewe yamekuwa ni maumivu tosha, nikiri wazi najichukia Mimi, historia yangu na Kila kitu kinachonizunguka, moyo wangu umekufa ganzi.. hauhisi chochote Tena.

Nimewahi kufikiria kujiua lakini naingiwa na hofu na uoga mkubwa sana, nakiogopa kifo.

Kitu ambacho naona kwangu ni nafuu na ninaweza kukifanya kikaniweka sawa katika hili.

Natamani kubadilisha Kila kitu kwenye maisha yangu, sio mali , nguo , ndugu marafiki na majamaa.

Yani kiufupi sihitaji kuwa na chochote kitakachonipa historia ya nyuma, hata Jina langu silihitaji Tena hata huu mwonekano wangu ubadilike natamani kwenda mbali sana Kila kitu kiwe kipya nianze upya nahisi Nitakuwa na Amani na nitapata nguvu ya kupambania furaha na ubora wangu Tena .

Sijui haya yote ni kwa namna Gani yanawezekana lakini natamani niache Kila kitu nitokomee mbali na nisionekane Tena kwenye Dunia yangu ya zamani.

Nawaombeni ushauri ndugu zangu nawezaje kulifanikisha hili.

Natangulisha shukrani🙏
Shida ni kuwa amani unaitafuta nje, bila kujua kuwa amani, furaha, upendo vinaanzia ndani yako. Hata uanze uende wapi kama hivyo vitu havimo ndani utabaki kujiona hivyo. Njia rahisi ya kuvipata hivyo vitu ni kujipenda mwenyewe. Love yourself, jipe kipaombele maisha yako yatabadilika.
 
Habarini ndugu zangu. Niende Moja kwa Moja kwenye mada. Maisha ya mwanadamu ni mjumuisho wa vitu vingi sana, tunapambana Kila kukicha kuhakikisha tunakuwa Bora zaidi ya tulivyokuwa Jana.

Lakini kwa sasa kwangu hii imekuwa tofauti. Najua wengi tunapitia changamoto lakini tunapambana na kuzishinda.

Kwenye maisha yangu, nimekuwa nikipambana kama wafanyavyo wengine lakini changamoto ninazopitia kwa sasa hazihusiana kabisa na mali... Bali ni mahusiano kwa wanaonizunguka, nimekuwa mtu wa kuumizwa, kutopewa thamani na kusalitiwa kwa wale wote nilio waamini na kuwapenda.

Sina furaha Wala sioni tumaini, sioni umuhimu Tena wa Mimi kuwepo katika ulimwengu huu.

Maisha yangu mwenyewe yamekuwa ni maumivu tosha, nikiri wazi najichukia Mimi, historia yangu na Kila kitu kinachonizunguka, moyo wangu umekufa ganzi.. hauhisi chochote Tena.

Nimewahi kufikiria kujiua lakini naingiwa na hofu na uoga mkubwa sana, nakiogopa kifo.

Kitu ambacho naona kwangu ni nafuu na ninaweza kukifanya kikaniweka sawa katika hili.

Natamani kubadilisha Kila kitu kwenye maisha yangu, sio mali , nguo , ndugu marafiki na majamaa.

Yani kiufupi sihitaji kuwa na chochote kitakachonipa historia ya nyuma, hata Jina langu silihitaji Tena hata huu mwonekano wangu ubadilike natamani kwenda mbali sana Kila kitu kiwe kipya nianze upya nahisi Nitakuwa na Amani na nitapata nguvu ya kupambania furaha na ubora wangu Tena .

Sijui haya yote ni kwa namna Gani yanawezekana lakini natamani niache Kila kitu nitokomee mbali na nisionekane Tena kwenye Dunia yangu ya zamani.

Nawaombeni ushauri ndugu zangu nawezaje kulifanikisha hili.

Natangulisha shukrani🙏

Mkuu pole sana, unahitaji tiba. Jiamini na jipende mwenyewe kwanza. Muombe Mungu akusadie.
 
Pole sana Mkuu.

Ila jitahidi uwe na utamadani wa kufanya ibada hasa majira ya saanane usiku kuelekea saatisa .

Utaanza kuona utofauti mkubwa.

Kabla ya kujenga mahusiano na watu jenga mahusiano na Mungu wako ambaye ndo chanzo cha uhai wako.

Na kisha muombe akuletee watu sahihi.

Kupitia night prayers hata akili yako itapata utulivu mkubwa na sio Kama ilivyo sasa hivi inapepesuka.


Pray , pray , pray 24/7.
🌤️🙋‍♂️✍️🎯👏👌👍👊🤝🙏
 
puker hizi hali si wewe pekeyako unapitia.. Kila mmoja katika hatua ya makuzi, utu uzima ama uzeeni hupitia changamoto zinazofanana na zako ama nginginezo.. Tunachotofautiana ni nyakati, vipindi na uzito
Umefika mahali pa kujikataa na kukata tamaa .. Hii ni mbaya sana.. Kamwe usipoteze tumaini kwakuwa hakuna gumu lisilo na mwisho..
Kuna miaka na vipindi vigumu sana tunapitia kwenye maisha.. Ambao hawakuwa imara walijidhuru kwa vilevi nk na wengine walijimaliza

Katika nyakati hizi mshike sana Mungu wako kwa imani yako.. Sali sana fanya sana ibada.. Kuna nguvu kubwa kwenye sala na ibada.. Muombe sana Mungu akuvushe salaam lakini kubwa kuliko yote muombe akupe mwisho mwema!
Una nafasi ya kuingia JF na kuandika. Una simu una bundle una mikono.. Kuna wengine hawana vyote hivyo
Maisha ni fumbo gumu na majibu yake yako kwenye utulivu na ukimya na sala
Don't give up buddy.. For in the darkest hour of life there is always a twinkle of light to lead you through...

Nakuombea....!!!
🌤️🙋‍♂️✍️🎯👏👌👍👊🤝🙏🆒
 
Hisia zako ni common sana kwa watu wengi, ni kama vile roho inaoza ikibaki katika mazingira uliyonayo Sasa; kama una mwanamke basi pasua kichwa unatamani umkimbie, wazazi nyumbani unaona kama vile kwenye mategemeo Yao umefeli, ndugu ukiangalia unaona unafiki mwingi, marafiki unaona kama vile wapo na wewe kwasababu unashika vijisenti na wanaburudika ukiwa around, we mwenyewe ukijiangalia kwenye kioo unaanza kujichukia......... It's common
A lot of people would like to disengage with their lives, mie binafsi ningepata mtu wa kuniajiri akaniambia kituo cha kazi ni huko Mtwara basi ningeenda maana inakuwa kama opportunity ya kuanza upya
wewe umeeleza 90% ya ninachokupitia kwa sentensi chache🙄
 
Ni ngumu sana ila jifunze kusamehe ili moyo wako uwe na amani ukiweka kinyongo hutokuwa na furah daima
Maan hata upate mtu atakae kupa furah na yeye pia n mwanadamu Kuna mapungufu yapo
 
Ngum sana.hii tatizo wengi mnatafutaga watu wakiwataka badala yanyinyi muwafae
 
Nilikuja ku realise kwamba dunia haiwezi kukutreat vizuri kwakuwa wewe ni mtu mzuri
 
"ni mahusiano kwa wanaonizunguka, nimekuwa mtu wa kuumizwa, kutopewa thamani na kusalitiwa kwa wale wote nilio waamini na kuwapenda." Hapo ndo unapokosea,,, hivi kuna watu bado mna upendo ? Dunia imevaa bukta, ishi kivyako, focus focus
 
Nanukuu maandishi yako yanasomeka "Sina furaha Wala sioni tumaini, sioni umuhimu Tena wa Mimi kuwepo katika ulimwengu huu". Conscious mind+Subconscious mind=Reality, kiufupi aliwazalo mjinga ndo litakalomtokea, acha kuplay victim simama badili mtazamo wako waza mema juu yako.
 
Back
Top Bottom