Nimelima alizeti zimesombwa na mvua heka 20

Nimelima alizeti zimesombwa na mvua heka 20

Pole mkulima mwenzetu kuna kitu kinaitwa "palio la maji" inaweza lima shamba hata miaka mitatu na ukavuna ila kama hapo ni njia ya maji ya asili basi huwa inatokea maji kupita kama mvua zitanyesha kwa wingi katika eneo ambalo yakijaa yanapita hapo!!!!

Mwaka jana kati heka mia almost 29 zilichukuliwa na maji zikiwa zimeshapandwa, mwaka huu kupanda bado ila maji yamepita almost 31 hazitalimwa kabisa sababu tayari dalili za maji zimeanza!!!
Kama una shamba la aina hii kubali kuacha ile sehemu maji yanapita
 
Mkuu usikate tamaa,
mwaka juzi nilifuga kuku kwa juhudi nakufanikiwa kuwa na kuku 65 lakini walikufa wote
mwaka janaa nikafuga wakafa wote,
na mwaka huu nafuga kwa mara ya tatu,
nikichemka nabadilisha mradi.

Duu.. kweli yataka moyo. Mie vimekufa yapata vifaranga kumi..roho imeumaaaaa..karibu niweke msiba.

Mungu ni mwema, aluta continue.

Back to topic, mkulima pole sana.. usikate tamaa kwa anguko hili, inuka pukuta mavumbi na usonge mbele.
 
Kweli kabisa mkuu, nilifuga kuku wa kienyeji kama 400 hivi wakafa wote, nikarudia tena kama 250 wakafa wote, sasa hivi ninao kama 17 naendelea kupambana! Hakuna kukata tamaa mkuu.....ila kila hatua nimejifunza mambo mengi ya muhimu na yananisaidia sana.Kuku wangu hawa 17 matetea kumi na tatu na wote wanataga sasa na wengine wanatamia mmoja ametotoa kifaranga kimoja na kimekufa, ila nimejua tatizo lilikuwa nini, ni kupambana kwenda mbele....na mbuzi tisa wawili wamezaa wiki iliyopita...naendelea kujifunza...tusikate tamaa na tumtegemee mwenyezi Mungu, kwa hakika tutafika!

Pole sana
Hope ulijua tatizo ni nini!
 
Simvunji Moyo jamaa ila kilimo tz bado sana na inakatisha tamaa
 
@ Shamle- utafanikiwa-- Biblia inasema chunga sana moyo wako ndipo chemchem za uhai zinapotokea... Moyo ukishindwa kila kitu kimeshindwa , utafanikiwa tu.

@nyamchele - Upo sahihi na nafurahishwa na jinsi unavyoendelea kupambana. Huu ni ushuhuda kwa watu wote wenye kutaka mafanikio.

Kuku unawafugia kwenye eneo kiasi gani?
 
daah mkuu pole sana, mimi mwaka jana nililima ekari 22 nilitumia karibu milioni 5 nilichopata ni 2m sijakata tamaa kwa kuwa shamba nilikodi nimeamua kununua langu. hivi mwezi wa tatu naenda kufyeka ekari 200 kwa ajili kulima alizeti na mbaazi kule manyara... hakuna kukata tamaa
 
daah mkuu pole sana, mimi mwaka jana nililima ekari 22 nilitumia karibu milioni 5 nilichopata ni 2m sijakata tamaa kwa kuwa shamba nilikodi nimeamua kununua langu. hivi mwezi wa tatu naenda kufyeka ekari 200 kwa ajili kulima alizeti na mbaazi kule manyara... hakuna kukata tamaa

Kiongozi manyara sehemu gani?
 
kuna bima ya mazao umewahi kuisikia kama ungekuwa nayo ungerudishiwa gharama kwa kiasi fulani
 
Poleni, mshajaribu kununua bima kwa ajili ya mazao au mifugo? Ndo wanavyofanya nchi za wenzetu.
 
Mimi mwaka Jana nimelima vitunguu eka sita (6) nimetumia milion Tisa (9) nikatoka na laki sita sijakata tamaa saivi nina eka mbili nasubiri baraka za mungu mwezi wa pili katikati kwenye mavuno hivyo pia na wewe nakushauri usikate tamaa maana mpaka nilitaka kujuta lakini nikakumbuka kuwa mungu alipa mtihani ule sijui kwanini maana nilitaka ninunue gari na hiyo hela huenda labda ingeniua sijui naomba ndugu zangu tukumbuke kuwa kukata tamaa ni dhambi tupambaneni mpaka kieleweke

Ndugu yangu mkasa wako unafanana na wangu,Mimi nilifanya kwa majaribio ekari mbili,nimetumia kama milioni tatu na nusu,ngoma ime bounce, nimefikiria weee nkaona ngoja nijaribu tena,japo nadhani kufuga vitu kama mbuzi ukiwa na eneo la kutosha ni more sure,kuliko kulima!!!
 
Ndugu yangu mkasa wako unafanana na wangu,Mimi nilifanya kwa majaribio ekari mbili,nimetumia kama milioni tatu na nusu,ngoma ime bounce, nimefikiria weee nkaona ngoja nijaribu tena,japo nadhani kufuga vitu kama mbuzi ukiwa na eneo la kutosha ni more sure,kuliko kulima!!!

Mkuu kilimo ni bora sana ila kinachotakiwa ni ujasiri na kutokata tamaa halafu kujifunza kila kukicha mwisho wa siku unaangukia kwenye bahari ya mafanikio kaza buti MKUU mi siachi kabisa
 
Back
Top Bottom