tang'ana
JF-Expert Member
- Apr 3, 2015
- 11,931
- 15,849
Wakuu, naandika hii thread huku nikiwa na hasira za kufa mtu.
Kuna litoto la uncle wangu naishi nalo hapa ghetto, huyu mtu namuona kama sio mzima kichwani kabisa.
Kamaliza Mzumbe na Ka GPA kake ka 4 (nadhani ndio kanampa kiburi)
Alivyomaliza chuo two years back nilimpambania akapata kasehemu ka kujishkiza huko kwenye viwanda vya wachina coz kuna jamaa yangu alinifanyia maneuvers flani wakawa wanampa 500k ambayo haina makato yoyote coz wanamchukulia kama trainee tu.
Well baada ya kuona kila leo anahudhururia Dodoma kupiga paper za utumishi na bado hatoboi nikamshauri aweke nguvu zaidi kwenye private sector kuliko kupoteza resources huko utumishi. So last two weeks kuna mdau wangu mmoja yuko kampuni flani aliniambia ofisini kwao wanataka kijana muaminifu aliyesomea mambo ya kama huyu dogo wangu hivyo nimsaidie kutafuta nikamuambia ninae binamu yangu, tuka arrange kila kitu dogo kafanyiwa interview ya kizushi na akafanikiwa kupita.
So jana wamemtumia offer letter, wamemuambia atareport kwenye office zao zilizopo huko Mbeya na salary ni kama 1.5m gross dogo kasema hayuko tayari kwenda Mbeya kwa mshahara huo labda wambakishe hapa hapa Dar, nimembembeleza dogo naona haelewi, nimewashirikisha wazazi wake naona pia hawajaelewana.
Sasa labda mnisaidie wakuu, huyu mtu mimi nimfanyaje maana pia ananiharibia sifa kwa yule jamaa yangu aliyenipa hii ramani?
Kuna litoto la uncle wangu naishi nalo hapa ghetto, huyu mtu namuona kama sio mzima kichwani kabisa.
Kamaliza Mzumbe na Ka GPA kake ka 4 (nadhani ndio kanampa kiburi)
Alivyomaliza chuo two years back nilimpambania akapata kasehemu ka kujishkiza huko kwenye viwanda vya wachina coz kuna jamaa yangu alinifanyia maneuvers flani wakawa wanampa 500k ambayo haina makato yoyote coz wanamchukulia kama trainee tu.
Well baada ya kuona kila leo anahudhururia Dodoma kupiga paper za utumishi na bado hatoboi nikamshauri aweke nguvu zaidi kwenye private sector kuliko kupoteza resources huko utumishi. So last two weeks kuna mdau wangu mmoja yuko kampuni flani aliniambia ofisini kwao wanataka kijana muaminifu aliyesomea mambo ya kama huyu dogo wangu hivyo nimsaidie kutafuta nikamuambia ninae binamu yangu, tuka arrange kila kitu dogo kafanyiwa interview ya kizushi na akafanikiwa kupita.
So jana wamemtumia offer letter, wamemuambia atareport kwenye office zao zilizopo huko Mbeya na salary ni kama 1.5m gross dogo kasema hayuko tayari kwenda Mbeya kwa mshahara huo labda wambakishe hapa hapa Dar, nimembembeleza dogo naona haelewi, nimewashirikisha wazazi wake naona pia hawajaelewana.
Sasa labda mnisaidie wakuu, huyu mtu mimi nimfanyaje maana pia ananiharibia sifa kwa yule jamaa yangu aliyenipa hii ramani?