Nimemsikiliza Mayele kupitia Youtube Channel ya Azam TV, nadhani ana shida mahala

Nimemsikiliza Mayele kupitia Youtube Channel ya Azam TV, nadhani ana shida mahala

Em ngoja kwanza
Inamaana hadi dunia ya leo mtu unashindwa kuelewa lugha? Tena kwa mchezaji mkubwa kama yeye?
Kwanini asitafute usaidizi?
 
Wachezaji wengi wa kigeni wanapokuja Tanzania wanakua wamekaa mda mrefy bila kuwa na timu wengi ni free agent wengine wamekaa miezi sita hawana timu na wengine hata mwaka sasa mtu amekaa mda mrefu bila timu unampaje mkataba mzuri mda mwingine hizi timu zinalaumiwa bure tu

Mayele angekua mchezaji mzuri congo asingekuja Yanga in first place angeenda timu kubwa zaidi ya yanga huo ndo ukweli
Kumpa mkataba unaoendana na hali yake ni sahihi ila ajue kabla kuwa anasaini nini.
 
Mayele kinachomuuma ni kusahaulika ghafla Yanga. Ile shangilia yake pia imepotezewa yaani anaona kama kawa ignored completely
Kwahiyo alitaka Yanga isimove on?

Yanga haiwezi kufanya ujinga ukiondoka tunamove siyo, Simba walimlilia Chama mpaka karudi, lakini Yanga ni mbele Kwa mbele.
 
Kumpa mkataba unaoendana na hali yake ni sahihi ila ajue kabla kuwa anasaini nini.
Saa nyingine acheni upumbavu, kuna document kibao tunapokea kutoka Uarabuni huwa tunapeleka mpaka Bakwata kutafsiriwa.

Sasa issue ya kutafsiri nayo dunia ya leo ufanyiwe? Huu ni upuuzi sasa.
 
Katika mahijiano ya Dakika 50 na sekunde 3 aliyofanyiwa na Azam TV ambayo yameonyeshwa kwenye youtube channel ya kituo hicho, Fiston Mayele ameongea mambo kadhaa, lakini mimi nimeamua kuongelea suala lake la mahusiano na timu aliyoichezea, yaani Yanga pamoja na anayoichezea hivi sasa, yaani Pyramids FC.

Katika mahijiano hayo, Mayele ameonyesha kukerwa na comments za mashabiki wawili au watatu dhidi yake au familia yake na kuamua kuibebesha lawama timu nzima ya Yanga kwa comments za watu hao.

Mayele anasema alipojiunga na Yanga alipewa mkataba na aka sign, ali sign sababu alikuwa hajui kiingereza, Manager wake alikuwa hajui Kiingereza na alikuwa anachekacheka tu.

Ulipoisha msimu wa kwanza, ndipo akasmua kubadili Manager na kumtumia Jasmine ambaye kwanza alishangazwa na ule Mkataba. Akasimamia ubadilishwe, akaongezwa mshahara pia ukampa uhuru wa kuondoka ikitokea club inamhitaji.

Amesema aliahirisha kusema live alichotaka kusema sababu Tanzania ameacha watu wake (familia) ila ameshauriana na Jasmine kwamba mwisho wa msimu ndiyo aongee kila kitu.

Hayo sikuona kuwa ni big issue kivile, kilichonistua na alipoiponda hadi timu aliyoichezea sasa. Mayele anasema alipewa Mkataba na Pyramids FC, mkataba ule Jasmine akaukataa, kwa maelezo yake Mayele akasema “waarabu ni wahuni kama usupotumia akili watakukandamiza”.

Hii kauli inatosha sana kumuweka Mayele katika sintofahamu na maboss wake hao wa sasa.

Mayele anaonekana ni mtu anayependa sana social media na attention zake, siyo mbaya ila, anapaswa kuelewea negative na positive effects za social medias. Hivyo awe mwangalifu sana na aongeacho.

Wana Yanga waliokwazika na Mayele ningewashauri wasiyabebe hayo, ni kijana anajipigania, pia kati ya vitu vinavyopelekea kuwa na kauli zile ni limits aliyo nayo katika uelewa na matumizi ya lugha ya kiswahili. Anajifunza Kiswahili the hardway hali inayompelekea kutoa kauli zinazoonekana kuwa ni kero, kukosa ustaarabu n.k ila yote ni sababu ya kuwa na ufinyu wa uelewa wa lugha anayoitumia, maana anajifunza kurusha ndege huku akiendelea kufanya assembling.

Kama angetumia lugha ya kwao au Kifaransa kamwe asinge strugle. Hivyo muleweni tu na mumuache aendelee na maisha aliyoyachagua.
Umeeleza vizuri sana, japo sijatazama hayo mahojiano lakini kwa maelezo haya, nimeelewa vizuri alichoongea na sababu ya kuongea.

Lakini, kubwa zaidi ni ushauri uliotoa ni wa msingi sana. Ni kweli Mayele ana shida ya ujuzi wa Kiswahili, na hii ndiyo sababu ya aina ya kauli zake.

Asamehewe tu.

Ova
 
Saa nyingine acheni upumbavu, kuna document kibao tunapokea kutoka Uarabuni huwa tunapeleka mpaka Bakwata kutafsiriwa.

Sasa issue ya kutafsiri nayo dunia ya leo ufanyiwe? Huu ni upuuzi sasa.
Mihemko ya nini? Umeshinda njaa siku nzima? Mambo ya kawaida haya, tunajadili kubadilishana mawazo, Upuuzi kwani unatumia hizi hoja kuombea ongezeko la mshahara?
 
Ni ukosefu wa akili huo ma boss Pyramid wakiona hio interview watapata tafasiri gani? sijui kwanini hajui kipi aongee kipi aache
1. hana busara atapata wapi mawazo ya kipi aongee kipi asiongee
2. anaongozwa na meneja ambaye hana professionalism licha ya exposure yule mwanamke ni mjingamjinga
3. anapenda sana mitandao. alifikiri Misri ni ligi sawa na ukimani. badala ya kukaza matako na kujifua analeta stori za uchawi kuwa anarogwa. jamaa lifala kweli.

viongozi wa simba wakiichukua hii takataka nitawaona hawana akili. hata yanga nao wakimrudisha nitawaona ni wajinga
 
Point kubwa ni kuwa Yanga wanamshambulia Kwa njia za kishirikina...hiyo ndo main point anachojaribu kusema...

Kuna mashabiki anawajua...watu wa ndumba ...wanatumika na club kwenye mambo ya kishirikina...wamekuwa pia wanamshambulia na yeye since aondoke Yanga...


Hiko ndo kilio chake
Angerogwq morisson,fei au bangala waliondoka kwa vurugu,mayele kaiingizia pesa Yanga na hata huko aliko ndani ya mkataba wake kuna pesa ya Yanga iwapo atauzwa,mayele mpaka anaondoka Yanga ukiangalia ile documentary ya Yanga alivyoongea akua na ugomvi na Yanga,kikubwa kinachomuuma mayele perhaps alijiona mkubwa kuliko klabu na akajua kuondoka kwake Yanga itayumba,matokeo imekua tofauti na alichokitarajia
 
Umeeleza vizuri sana, japo sijatazama hayo mahojiano lakini kwa maelezo haya, nimeelewa vizuri alichoongea na sababu ya kuongea.

Lakini, kubwa zaidi ni ushauri uliotoa ni wa msingi sana. Ni kweli Mayele ana shida ya ujuzi wa Kiswahili, na hii ndiyo sababu ya aina ya kauli zake.

Asamehewe tu.

Ova
Mayele hajui Kingereza, lakini Kiswahili anaongea kuliko Mimi.

Mayele anajuwa kuchamba kama Mange huwezi kusema hajui vizuri Kiswahili.

Mayele anajuwa kuna watu wanaishi Kwa mizinga, Mayele anawachamba Hadi mashabiki wa Yanga wanaokwenda kuingia bure na kuvunja geti.

Labda Kiswahili mnachosema anazidiwa na Haji Manara na siyo Kiswahili bali uswahili.
 
Angerogwq morisson,fei au bangala waliondoka kwa vurugu,mayele kaiingizia pesa Yanga na hata huko aliko ndani ya mkataba wake kuna pesa ya Yanga iwapo atauzwa,mayele mpaka anaondoka Yanga ukiangalia ile documentary ya Yanga alivyoongea akua na ugomvi na Yanga,kikubwa kinachomuuma mayele perhaps alijiona mkubwa kuliko klabu na akajua kuondoka kwake Yanga itayumba,matokeo imekua tofauti na alichokitarajia
Sure mkuu.
 
Back
Top Bottom