nimemsikiliza Prof. Kabudi hadi mwisho, wanaoipinga sana katiba hawajaisoma vzur!!!

nimemsikiliza Prof. Kabudi hadi mwisho, wanaoipinga sana katiba hawajaisoma vzur!!!

Kuna vitu vya kupinga na kurekebisha kidogo ktk rasimu lakin cyo suala la uraisi, hilo lipo vyema saaaaana. Ni mfumo ambao umeprove efficiency kuanzia USA. Kwa federal govt ya obama na zile states gvts, hapa kwetu vyuo vikuu mfano UDSM & UDOM vimekuwa vikitumia mfumo huu ktk serikali zake za wanafunzi. Naupa 100. Yah sure ni moja ya michango yangu pia niliotoa ktk maoni.
 
mi namkubali sana prof kabudi wa pale kitivo cha sheria udsm ila katika hili la serikali tatu siwezi nikakubali ata kidogo kushawishiwa ni mzigo kwetu na atuhitaji mzigo huo.

Kwanza kabisa naipongeza tume kwa kazi nzuri na kwakufanyia kazi kwa umahiri mkubwa maoni ya wananchi "Wananchi have spoken, we are duty bound to respect their voices".

Muundo wa serikali tatu ni mzuri kisheria. Kila nchi itakuwa huru kujifanyia mambo yake bila kuathiri muungano/shirikisho.
Hoja ya gharama kubwa na kuvunjika muungano, hizo ni hoja ambazo wanasiasa, ambao masilahi yako yameathirika kwa muundo wa serikali tatu wanahaha kujificha katika hoja hizo. Kimsingi hizi hoja ni za kupikwa na wanasiasa ili kujustfy interests zao kisiasa.
Gharama: Hii siyo hoja, kwani serikali za Tanzania bara na Zanzibar watatakiwa kuunda mabaraza ya mawaziri pasipo kuweka mbele urafiki na vyama vyao.Watatakiwa kuzingatia ufanisi zaidi.Hivyo hawatahitaji kuwa na baraza kubwa la mawaziri, wasiozidi 10. Wabunge nao,tume za uchaguzi za nchi hizo 2 zitalazimika kupunguza majimbo yasiyo ya lazima. Mishahara ya wabunge hao kupunguzwa.

Kuvunjika kwa Muungano: Atavunja nini? Hizi ni hofu za bure. Kwani maraisi wote wa nchi 2 watakuwa ni wajumbe wa baraza la usalama la taifa.

NOTE: -Wanasiasa waache mchezo huo mchafu wa kuingilia "sauti za wananchi", kwa masilahi yao kisiasa.
- Watanzania tuwe makini na propaganda hizi za wanasiasa wanaotaka kupindisha ukweli kwa masilahi yao kisiasa.
 
Ila jamani hii inchi itakuwa ya marais. Marais wa3?!! Khaaa!

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums

Hasa pale tutakapokuwa kuwa na marais watatu wastaafu wanaopata 80% ya marais walio madarakani!
 
Mkuu Mystery umekosea kidogo,ngoja nikuweke sawa nafasi yenye ulaji mkubwa itakuwa ni Rais wa Tanganyika Bwana.Rais wa shirikisho atakuwa kama Gorberchev wa USSR ya zamani,Zenj hakuna ulaji wowote sana sana Rais wa huko itabidi kila mara avae helment kwa usalama wake au umesahau kile kikundi cha kigaidi cha UAMSHO kitakuwa na nguvu kubwa mara baada ya askari shupavu RAIA wa TANGANYIKA watakuwa wameshafungasha virogo n kuwaachia magaidi yafanye yatakavyo.

Hiyo rasimu ya Katiba,ni nzuri sana,tunapaswa waTZ wote wanyonge wa nchi hii tumpongeze jaji Warioba na timu yake kwa ujasiri wao mkubwa kwa kuja na rasimu,ambayo ni kinyume cha matakwa ya watawala.

Si mmemsikia Kinana ametamka hadharani kuwa wao CCM hawaiungi mkono rasimu hiyo,hadi wameitisha kikao cha dharula cha CC yao,ambacho kitakutana siku ya Jumatatu.

Lakini waliopigwa na bumbuazi zaidi,ni wale waliokuwa wanausaka urais wa Muungano,kwa udi na uvumba.

Kwa kuwa kwa rasimu hiyo ilivyo hivi sasa ambapo,tutakuwa na Rais wa Zanzibar na Rais wa Tanzania bara,aka Tanganyika,maana yake ni kuwa marais watakaokuwa na nguvu zaidi ni Rais wa Zanzibar na yule mwenzake wa Tanganyika.

Kwa kuwa rasilimali zote za nchi,kama vile gesi,mafuta,madini ya aina mbali mbali,rasilimali hizo,zitakuwa kwenye wizara za serikali za Zanzibar na Tanganyika,kwa maana hiyo wale.wagombea,waliokuwa wameanza kumwaga mabilioni yao wakiamini mabilioni hayo yatarudi,mara tu wsingiapo Ikulu,kwa namna watakavyofisadi radilimali zetu, wagombea wa design hiyo wajihesabu tu wameliwa,kwa kuwa Rais wa Muungano,baada ya 2015,atakuwa hana tofauti yoyote na malkia Elizabeth wa UK,ambapo nafasi yake ni ceremonial post,mtendaji mkuu wa serilali ya Uingereza ni David Cameron.

Vivyo hivyo ndivyo itakavyotokea kwa TZ,ambapo Urais wa Muungano,utakuwa ceremonial post,nafasi za utendaji na ulaji,zitakuwa ni zile za urais wa Zenj na Bara!!
 
Last edited by a moderator:
Mabwana wa maandamano wamesemaje???naona kama wamemwagiwa maji,waliwatukana sana wakina Prf.Beregu!!!
 
Kuwarudisha MaDC na MaRC kama wateule wa Rais hili sikubaliani nalo kamwe.Wanakula tu kodi bure bila ya kuwa na faida yoyote kwetu ni wakati wa kuwa-get rid of all dead-woods in the government system to make it more efficient and productive for God'sake.

mkuu hujastuka?wameondoa viti maalum sasa hao mahawara wa mzee na vibaraka wake watapewa nafasi gani?lazima ziwepo nafasi za kutupa chakula za mzee na wapambe wake.
 
Fanyeni mfanyavyo,bila ya mamlaka kamili ya z'br no muungano.

mamlaka kamili mnaipata kwa kuvunja muungano,so kwa nini mnazunguka mbuyu?kama kweli mko na dhamira ya dhati kabisa anzeni kuwapa habari wenzenu waliojenga na kuanzisha maduka huku waanze kujiandaa kuondoka au kuchagua uraia kama watataka kuukana uzanzibar!??kwa sababu kiukweli kabisa hawa ndio watakuwa kachumbari yetu muungano ukivunjika kwa jinsi tulivyo na hasira na nyinyi.mnakera sana,sijui hata mnataka nini maana hamjitambui.
 
hiyo rasimu ya katiba,ni nzuri sana,tunapaswa watz wote wanyonge wa nchi hii tumpongeze jaji warioba na timu yake kwa ujasiri wao mkubwa kwa kuja na rasimu,ambayo ni kinyume cha matakwa ya watawala.

Si mmemsikia kinana ametamka hadharani kuwa wao ccm hawaiungi mkono rasimu hiyo,hadi wameitisha kikao cha dharula cha cc yao,ambacho kitakutana siku ya jumatatu.

Lakini waliopigwa na bumbuazi zaidi,ni wale waliokuwa wanausaka urais wa muungano,kwa udi na uvumba.

Kwa kuwa kwa rasimu hiyo ilivyo hivi sasa ambapo,tutakuwa na rais wa zanzibar na rais wa tanzania bara,aka tanganyika,maana yake ni kuwa marais watakaokuwa na nguvu zaidi ni rais wa zanzibar na yule mwenzake wa tanganyika.

Kwa kuwa rasilimali zote za nchi,kama vile gesi,mafuta,madini ya aina mbali mbali,rasilimali hizo,zitakuwa kwenye wizara za serikali za zanzibar na tanganyika,kwa maana hiyo wale.wagombea,waliokuwa wameanza kumwaga mabilioni yao wakiamini mabilioni hayo yatarudi,mara tu wsingiapo ikulu,kwa namna watakavyofisadi radilimali zetu, wagombea wa design hiyo wajihesabu tu wameliwa,kwa kuwa rais wa muungano,baada ya 2015,atakuwa hana tofauti yoyote na malkia elizabeth wa uk,ambapo nafasi yake ni ceremonial post,mtendaji mkuu wa serilali ya uingereza ni david cameron.

Vivyo hivyo ndivyo itakavyotokea kwa tz,ambapo urais wa muungano,utakuwa ceremonial post,nafasi za utendaji na ulaji,zitakuwa ni zile za urais wa zenj na bara!!
upo sawa ingawa watakubishia si unajua hapa jf watu hawapendi ukweli
 
Nadhani haya ni maoni yako, kwani Prof Kabudi hakusema hivyo. Alichosema ni kwamba Serikali ya shirikisho itasimamia zile wizara saba zinazohusiana na mambo ya Muungano, ila mambo yasiyo ya muungano yatasimamiwa na individual governments zilizo katika shirika. Ukiangalia utaona hizo wizara saba zote ni zile muhimu. Rais wa Muungano ni kiongozi wa NCHI na kiongozi wa SERIKALI ya JMT, na ni Amiri Jeshi Mkuu wa majeshi ya JMT. Ndiye mteuzi wa Jaji Mkuu. Sasa power zote hizo bado unasema urais wa shirikisho ni ceremonial post?
Kwani mkuu si ulisikia benki kuu ya uswisi mwaka jana ilipotangaza kuwa vigogo 6 wa serikali ya CCM, wamewekewa dola milioni 197, kwenye nchi hiyo, na makampuni yanayochimba gesi na mafuta hapa nchini?

Sasa kwa kuwa gesi na mafuta, ipo chini ya wizara ya Nishati na madini, ambayo siyo wizara ya muungano, kwa maana hiyo "ulaji" huo, utawaangukia marais wa Zenj na Tanzania bara!

Vile vile, hukumsikia Zitto Kabwe, kwenye kikao kinachoendelea, jinsi alivyomkomalia, waziri wa ujenzi, John Magufuli, jinsi wizara yake, ilivyotafuna pesa kiasi cha shilingi bilioni 252, tuhuma ambayo alishindwa kabisa kuitolea maelezo?

Wizara ya ujenzi nayo sio ya Muungano, kwa maana hiyo, "ulaji" wa wizara ya ujenzi, upo chini, ya madaraka ya Rais wa Tanganyika.
 
Back
Top Bottom