Nimemuelewa Halima Mdee. Amekubali makosa, anataka maridhiano; yuko tayari kujirudi na kurekebisha mambo chamani mwao

Nimemuelewa Halima Mdee. Amekubali makosa, anataka maridhiano; yuko tayari kujirudi na kurekebisha mambo chamani mwao

2010 Dr Slaa si aliibiwa kura?
2015 Lowassa si aliibiwa kura?...
Mara zote hizo walikubaliana kwenda bungeni. Lakini safari hii walikuwa hawajakubaliana. Kwa nini sasa atumie njia za udanganyifu? Usitunge sababu za uongo eti sababu wanaume hawatakuwa wabunge, hapo umezusha uwongo.
 
2010 Dr Slaa si aliibiwa kura?
2015 Lowassa si aliibiwa kura?...
Kwa hiyo tukubali tu kuwa mfumo wa Tanzania ni wa chama tawala kuiba kura? Sisemi kama mara zotehizo ulizozitaja kuwa kuliibiwa kura kwa sababu sina ushahidi kama ambapo sina ushahidi mara hii, nisichokubaliana na wengi wenu mnaokuja na sentensi hizi za kuwa huko nyuma kura ziliibiwa na mara hii ikubalike tu.

Kwa mtizamo wenu huu si bora basi kuwepo na chama kimoja tu na watu wajue na kuacha kupoteza muda na pesa za nchi kwa uchaguzi usio na umuhimu wowote ule.
 
Leo, kama mtanzania wa kawaida nisiye mwanachama wa chama chochote cha siasa nchini na kwingineko, nimepata bahati ya kumsikiliza Mhe. Halima Mdee aliyekuwa mzungumzaji mkuu kwenye mkutano wao na waandishi wa habari...
Tunafanya uchaguzi bawacha kupata mwenye kiti mpya, hivyo halima akiomba radhi kurud atakuwa tu mwanachama tu wakawaida.,
 
Leo, kama mtanzania wa kawaida nisiye mwanachama wa chama chochote cha siasa nchini na kwingineko, nimepata bahati ya kumsikiliza Mhe. Halima Mdee aliyekuwa mzungumzaji mkuu kwenye mkutano wao na waandishi wa habari...
Je, amekiri kughushi nyaraka?
 
Leo, kama mtanzania wa kawaida nisiye mwanachama wa chama chochote cha siasa nchini na kwingineko, nimepata bahati ya kumsikiliza Mhe. Halima Mdee aliyekuwa mzungumzaji mkuu kwenye mkutano wao na waandishi wa habari...
Somo hili kwa bahati mbaya sana halieleweki kwa Ndugai.
 
Anaweza. Rais Mstaafu Kikwete aliwahi kumteua Mhe Mbatia akiwa si MwanaCCM. Na nimeeleza kuhusu hilo kwenye mada yangu

Sawa kabisa. Lakini ikitokea hivyo au hata kwa hivi viti maalum vya Ndugai basi huyo hatakuwa yule Halima Mdee aliyefahamika kupitia CHADEMA.

Atakuwa tayari kaunga mkono juhudi. Hataweza tena kuongea kwa ile “jeuri ya chama” aliyokuwa akiitumia.
 
Leo, kama mtanzania wa kawaida nisiye mwanachama wa chama chochote cha siasa nchini na kwingineko, nimepata bahati ya kumsikiliza Mhe. Halima Mdee aliyekuwa mzungumzaji mkuu kwenye mkutano wao na waandishi wa habari....
Hata Mzee Msekwa ndivyo anavyojua hivyo. Mtu angemhoji Jaji Mzee Warioba angesema hayo hayo. Mheshimiwa Ndugai hajui hayo. Akishaapisha ameapisha. Sheria zote hazi-apply baada ya yeye kufanya kiapo. Anajua kuwa hesabu zake za kuongoza bunge lisilo na wapinzani hazikubali. Ndio maana anahaha na kuharibu kutumia nguvu na kila ubabe. Sijui kama atafanikiwa.

Hapa kuna Halima na wenzake 18 kwa upande mmoja na Mbowe na Chadema kwa upande nwingine. Kuwasamehe kina Halima ili waendelee kuwa wabunge kutagawa chama kwa mazingira ya sasa ukiangalia reaction ya wanachama walio wengi. Sijui itatumika hekima gani.
 
Ila kuna suala la msingi na ki-utaratibu.

Je, JJM ambae ni katibu Mkuu wa CHADEMA, kamuandikia spika wa Bunge la JMT kuthibitisha kuwa akina Halima wamevuliwa uanachama?

Kwa kuwa "wakubwa" wa nchi hii hawafanya kazi kwa press conference ila barua rasmi; nadhani JJM afanye hivyo ili ku-justify kile alichosema Msekwa kuwa applicable.

Vinginevyo, utakuwa mchezo wa kuviziana kwa CDM kuacha kuandika barua maana "inaogopa" kutambua mamlaka ya spika, na Mhe. Ndugai huenda hiyo ikawa karata yake kubwa sana kwenye hili "figisu"
 
Kikatiba hao siyo wabunge tena wa bunge la JMT,mara tu baada ya kuvuliwa uanachama
Unaota wewe
Vyama vya kisanii utavijua tu,mbona Aida hamjafukuza?mbona madiwani wanaapa hamjawafukuza?
 
Ubunge wa viti maalumu kutoka cdm utakuwa na maana sana kwa ccm endapo hao wamama watakuwa wanachama hai wa cdm, vinginevyo inakuwa ni biashara ambayo hailipi kwa ccm,

ccm aka gambas wanawahitaji hao wamama wa cdm ili justify kuwa uchaguzi ulikuwa huru na haki hivyo kuwafanya Serikali kupata msaada sasa kitendo cha cdm kuwafuta uwanachama kimeharibu kila kitu,

na hii ndio sababu imewafanya kuwataka hao wamama wajirudi na kureconcile na chama chao ili lengo lao litimie, ila kiufupi hili bunge kama akina halima kipindi kile walikuwa wanapewa adhabu ya kukaa mwaka nje ya bunge, this time watapewa adhabu ya kuwa nje ya bunge kwa vipindi vyote au kuwavua kabisa huo ubunge as long wao wanapata mpunga toka kwa wahisani.

Sasa sijui kwanini akina halima hawalioni hili, kwamba wao wanatumika tu kama rubber stamp, baada hapo wanatupwa huko, Kifupi hao wamama wakae pembeni maana naona wamelewa madaraka kiasi cha kujiona wao ni untouchable.
 
Unaota wewe
Vyama vya kisanii utavijua tu,mbona Aida hamjafukuza?mbona madiwani wanaapa hamjawafukuza?
Ndiyo tushawafukuza uanachama sasa na yale mabillioni mnayoyapigania muyapate toka kwa mabeberu hamuyapati maana taarifa za kufutiwa uanachama hao wabunge tayari wanazo
 
Umeamua na kuchangia vyema mawazo yako. Lakini, kauli ya kutokuwa na chama ni muhimu kwangu kuonyesha jinsi nisivyolalia upande wowote kisiasa. Ubarikiwe sana!
Ile siku bwana mdogo Ndugai anamuapisha Polepole lakini anaongelea mambo ya Chadema na kusema kuna "unyanyasaji wa kijinsia" akiwatumia akina Halima Mdee kama Mfano. Halima anafanya press yake na kusema Chadema hakuna mfumo dume kama inavyoelezwa, maana wao wamekuwa viongozi huko. Ndugai anajionaje?
 
Hao akina mama tayari wanachama wameshapoteza imani nao kiasi kwamba hata ikitokea wakarejeshwa kundini wanachama hawatakuwa na imani nao tena na hata nyadhifa walizokuwa nazo kabla hawawezi kuzipata tena.

Wao kama kweli wanakipenda chama chao kama wanavyodai basi wajiandae kwenda kukitumikia wakiwa kama wanachama wa kawaida na kinyume cha hapo watafute pa kwenda.

Waliweka maslahi yao binafsi juu ya maslahi ya chama na kukubali kurubuniwa na Magufuli na Ndugai ili ionekane uchaguzi mkuu uliopita ulikuwa huru na haki wakati ulikuwa ni uhuni mtupu.

The traitor pays with his/her own blood, let them face the music.
 
Rule of law should be a cornerstone of our nation! Even the persons that have the power to be above the law by instruments, should observe the existence of such instruments as the law itself !

Wenye mamlaka wasitumie mapungufu ya kisheria yanayotoa mianya ya ubabe kuwa wababe. Huo ni ushamba uliopitiliza.
CCM haipo hivyo tena. Haiangalii utawala wa sheria. Kwa kuwa hawana tena ridhaa ya walio wengi hutumia hoja ya nguvu na ubabe. Walipora kwa nguvu uchaguzi wa vijiji na serikali za mitaa. Haiwezekani kwa levo ya upinzani ilipofikia CCM wapate asilimia 100 ya mitaa na vijiji vyote. Uharamia ulitumika. Wamepora uchaguzi wa madiwani, wabunge na raisi.

Huenda wangelishinda lakini sio kwa asilimia 100. Uharamia na ubabe ulitumika kupora ushindi kwa aslimia zote hizo. Kwanza Ndugai anaona aibu kuwa waliiba ushindi kijinga. Sasa kuna bunge la chama kimoja. Fomula ya kupanga Kamati za bunge inatatizika kwa kuwa kikanuni kamati zingine lazima zisimamiwe na wapinzani.

Anatumia nguvu nyingi na ubabe uleule kupata wapinzani ndani ya bunge. Hiyo hapo ni njama yake na Mahera wa NEC kuwarubuni akina Mdee ili kujaribu kuficha aibu ya uso.
 
Tano, iko wazi kikatiba (na haijalishi kauli ya yeyote yule) kuwa Mbunge anapopoteza uanachama wa chama kilichompendekeza na kumdhamini, ubunge wake hukoma pia. Hivyobasi, kwa kufukuzwa uanachama wao (kwakuwa uamuzi wa CHADEMA bado haujabadilishwa au kubadilika) Mhe. Halima Mdee na wenzake 18 walikoma kuwa Wabunge kikatiba na kisheria..
☝️☝️
Ajabu ya karne ni kuwa ndu/gay, kiongozi wa mhimili wa bunge hajui haya
 
Aandike barua kwa spika, amweleze hawezi kuwa mbunge viti maalumu sababu hana chama, hivyo atangaze kujiuzulu ubunge viti maalumu hadi watakapopata baraka za chama. Hapo atakuwa ameyataka maridhiano
Mh. Mdee akifanya hivi itakuwa ni unyenyekevu na ataonesha kweli anamaanisha kutaka maridhiano
 
Back
Top Bottom