Nimemuona Hassan Mwakinyo akipigana, maoni yangu ni haya

Nimemuona Hassan Mwakinyo akipigana, maoni yangu ni haya

Marehemu Thomas Mashali, Mbwana Matumla hawa ndio walikuwa maboxer, Marehemu Mashali alikosa discipline ya maisha akapotea.. Kwa sasa namuona Dullah Mbabe anakuja vizuri huyu Mwakinyo amepata promota au management nzuri inambeba lakini ni wa kawaida sana..

Watanzania wenzangu michezo ni fursa hebu wale wenye vipato mjaribu kuchukua management ya hawa watu kuanzia boxing, football na basketball.. Uwekezaji kwenye tasnia ya sports unalipa..na Tanzania vipaji viko vingi tatizo havifikiwi na hakuna watu serious wakuendesha hii biashara.. Nawaona maboxer wengi sana uswahilini huko ambao kama wanapata bahati ya kuingia kwenye ring za USA na EUROPE ni biashara kubwa sana..
Thomas alikuwa talented boxer Ila hakuwa na nidhamu,
 
Katika mchezo wa ngumi kumkuta mpiganaji aliyrkamilika ' a perfect fighter' ni ngumu sana utamkuta ana hiki lakini kakosa kile, mpiganaji kama mwakinyo ana punching power lakini kuna vitu bado anastahili kuvifanyia kazi kama defence na footwork na kutokana na madhaifu haya na yale ndio maana wapiganaji hawaachi kufanya mazoezi ukiangalia historia utakuta wachezaji wachache sana wenye almost kila kitu mtu kama Roy Jones huyu tulizoea kumuita naturally gifted boxer alikuwa amekakilika sana, kwa sasa kumpata mtu kama huyu sio rahisi ukiangalia top dogs for now in welter weight ambayo mwakinyo anacheza utamkuta mtu kama Spence Jr, Terence bud, Thurman, mikey Garcia na mzee pac man utaona wengi wao katika hii list wana mapungufu kadha wa kadha kwa mfano Spence nae sio defensive na ana poor head movement while Crawford hana good footwork n.k ninacho muombea bwana mdogo mwakinyo ajitahidi ku improve mechi baada ya mechi kama alivyo canelo na apate walimu sahihi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Afanye sana zoezi la kulenga target,.... vinginevyo kweli huko mbele tutakuja pata aibu sie wa tz
 
Boxer wa Kweli Tanzania alikua Snake boy..nadhani mwanae pia atakuja kuwa boxer mzuri angalau toka pambano lake lile aliopigana na Dullah mbabe akapigwa kwa KO ambalo lilisababisha Hadi fuvu la kichwa kuwa na hitilafu na kuambiwa apumzike sijafamfatilia Kama bado asharudi ulingoni. Maboxer wengine tulionao silaha ni punch tuu foot work ovyo,ila kinachosabisha hivi maboxer wengi tulionao Tanzania hawajapita katika misingi ya ngumi wengi walianzia kwa ajili ya kujilinda kwakua wanakaa maeneo ya wahuni Kama keko manzese,Tandale,mabibo,Mwananyamala au wakabaji ule ukabaji wa uswahilini unapigwa nakozi Hadi unatepeta....kwaio hi inawafanya wasipitie katike ile misingi maana hapa Tanzania maboxer wengi hawa wanaotamba wachache walikua Timu ya ngumi ya Taifa kwenda kushiriki mashindanoni ya jumiya ya madola au Olympic Yani kuanzua Amateur Bali wengi wao wanaanza ngumi tuu na kuwa professional.

Boxer mzuri anaanzia Amateur baadae anakuja kuwa professional

Ila majeshi sijui yanasaidia kutoa Ajira au pia yanaharibu vipaji vya ngumi maana maboxer wazuri maeneo yetu ya uswahilini wakianza kupigana amateur wakiwa wazuri wanapewa Ajira na kipaji kinaishia huko huko jeshini na hatuwaoni kwa Sana kutamba kimataifa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom