Marehemu Thomas Mashali, Mbwana Matumla hawa ndio walikuwa maboxer, Marehemu Mashali alikosa discipline ya maisha akapotea.. Kwa sasa namuona Dullah Mbabe anakuja vizuri huyu Mwakinyo amepata promota au management nzuri inambeba lakini ni wa kawaida sana..
Watanzania wenzangu michezo ni fursa hebu wale wenye vipato mjaribu kuchukua management ya hawa watu kuanzia boxing, football na basketball.. Uwekezaji kwenye tasnia ya sports unalipa..na Tanzania vipaji viko vingi tatizo havifikiwi na hakuna watu serious wakuendesha hii biashara.. Nawaona maboxer wengi sana uswahilini huko ambao kama wanapata bahati ya kuingia kwenye ring za USA na EUROPE ni biashara kubwa sana..