Nimemwaga mboga...lakini nafsi inanisuta.

Nimemwaga mboga...lakini nafsi inanisuta.

Hata mimi niko kama wewe! yaani kuna watu ni wadwanzi sana, sasa zaidi ya hapo unaleta na watu eti washuhudie!! kwa kweli simlaumu Nduka ku fanya alichofanya.

yeah man,......lazima heshima iwepo mkuu
 
Was thinking in the same line, but to face the devil alone, my stomach shake.

Achana na hii habari ya vikao, wewe tengeneza SMS nzuri ukiwa umetulia na waeleze ulichofanya, watakaa wao na kuyamaliza kama hiyo ndoa kweli ilikuwa iwe, otherwise utaharibu kuweka vikao.

Ukizingatia jamaa sasa anaweza kuleta wale kina mama sijui wa clouds, si unajua kile kipindi chao cha redio.. fikiria na wewe tena na mabaki ya Ndumu!!
 
Jaman si jambo jema kuharibiana NDOA,,,,,,,nduka hujatenda haki,,,,ndoa ni kitu adhwiiiim
 
Kweli ubinadamu kazi.

Unachoweza kufanya sasa hivi ni kumtafuta mume wa huyo dada umweleze kwamba maneno uliyotoa pale yote yalikua ya uongo na umweke sawa kuhusu uhusiano wako na mkewe (kwamba ilikua ni ishu ya kiofisi tu iliyowaweka karibu) alafu umuombe na dada wa watu samahani.
Siku nyingine ukiwa na shida watu watakataa kukusaidia kwa kua na tabia za ajabu ajabu...kuanzisha ugomvi kwenye nyumba ya mwenzako kwa maneno ya uongo sio kitu kizuri hata chembe.

Tena ikiwezekana mhusishe mkeo...uwaombe hao wanandoa wengine mkutane wote wa nne na kuongea. Na ukifanya hivyo usianze kutafuta visingizio vya sijui nilifanya kwasababu hii au ile maana hamna chochote kilichokupa wewe haki ya kuropoka maneno ambayo yanaweza kuharibu ndoa ya wenzako..kwahiyo wewe elewesha na omba samahani kama mtu aliyokosa na sio kujifanya ulilazimishwa/lazimika/sukumwa kufanya vile.
 
mhhhhhhhh!..yaani hapo ndipo ninapokiri keli Mungu katuumba tofauti_maake mimi nilivyo na kislani hata ex_wa girlfriend wangu sitaki kukaa naye karibu(thanx God hata simfahamu na wala sitaki kujua habari zake..hope hata wenzangu wenye hulka kama zangu hawataki kujua).,,sembuse mwanamke niliyemuoa alete ex wake eti tuongee,.....yaaani sijui

Mkuu maisha haya huwezi waepuka hawa ma x, hasa kama ulikuwa una date watu wa class(social) yako maana wataendelea kuwepo arround lakini kama unacheza na mahaus geli na ma bar maid mnaweza kuka miaka mia tano bila kuonana.
 
Hapo umeshasambaratisha ndoa ya watu. Nenda kaonane nao na uwaombe radhi.
 
Tena ikiwezekana mhusishe mkeo...uwaombe hao wanandoa wengine mkutane wote wa nne na kuongea. Na ukifanya hivyo usianze kutafuta visingizio vya sijui nilifanya kwasababu hii au ile maana hamna chochote kilichokupa wewe haki ya kuropoka maneno ambayo yanaweza kuharibu ndoa ya wenzako..kwahiyo wewe elewesha na omba samahani kama mtu aliyokosa na sio kujifanya ulilazimishwa/lazimika/sukumwa kufanya vile.

Nakubaliana na wewe 100%, ila sasa nimejifunza hili suala halihitaji kuwa husisha wake zetu maana inaweza kuwa ndio tunachochea moto. Thanks kwa kunipa mwanga, u r a true angel
 
Mkuu maisha haya huwezi waepuka hawa ma x, hasa kama ulikuwa una date watu wa class(social) yako maana wataendelea kuwepo arround lakini kama unacheza na mahaus geli na ma bar maid mnaweza kuka miaka mia tano bila kuonana.

Pamoja na hili mzee , lakini ni muhimu sana kujaribu ku avoid ile close contact kwani ni lazima itafikiriwa sivyo tu.
Nakupa mfano mimi kuna ex wangu nilikutana nae, akanishauri eti tufanye familia zetu za sasa ziwe zinatembeleana, kumbuka mumewe hanijui, nikafikiria nikaona huyu analeta udwanzi nikampa live kuwa hilo haliwezekani na sitaki mawasiliano ya namna hiyo, ka kasirika na hiyo nimeifurahia manake alitaka kuniharibia bure maisha yangu na my lovely family!
 
Nakubaliana na wewe 100%, ila sasa nimejifunza hili suala halihitaji kuwa husisha wake zetu maana inaweza kuwa ndio tunachochea moto. Thanks kwa kunipa mwanga, u r a true angel
Kuwahusisha kunaweza kukawa kuzuri au kubaya..binafsi nadhani itakua vizuri maana inaweza ikawasaidia (nyie wanaume) kubehave.Kama mara ya kwanza mkeo angebaki usingedhubutu kutoa hayo maneno labda kama ungekua umelewa njwi hujielewi..ila vyovyote vile
samahani ya dada wa watu umpatie.
 
Pamoja na hili mzee , lakini ni muhimu sana kujaribu ku avoid ile close contact kwani ni lazima itafikiriwa sivyo tu

Hilo la close contact haliwezi kukubalika maana hata kama hamna lengo hilo lakini mnaweza kuamsha mashetani yaliyolala, nakubaliana na wewe mkuu.
 
sikushauri vikao, hata kama una nia ya kurekebisha , hakuna mwanaume anaweza kukaa meza moja na mwanaume aliyelala na mkewe na yeye akajua mbaya zaidi amejua mbele ya kadamnasi, kama unataka kumwagiwa tindikali endekeza vikao,! tuma msg jieleze mwanzo mwisho then waache wenyewe wayasolve.
 
Kuwahusisha kunaweza kukawa kuzuri au kubaya..binafsi nadhani itakua vizuri maana inaweza ikawasaidia (nyie wanaume) kubehave.Kama mara ya kwanza mkeo angebaki usingedhubutu kutoa hayo maneno labda kama ungekua umelewa njwi hujielewi..ila vyovyote vile
samahani ya dada wa watu umpatie.

Ku behave sio wanaume tu, mbona huyo dada aliniogesha kilimanjaro kubwa ya baridi mbele ya watu? Ila bora awepo mke wake maana mke wangu sioni anahusika vipi from the begining wenye matatizo ni sisi wa tatu.
 
sikushauri vikao, hata kama una nia ya kurekebisha , hakuna mwanaume anaweza kukaa meza moja na mwanaume aliyelala na mkewe na yeye akajua mbaya zaidi amejua mbele ya kadamnasi, kama unataka kumwagiwa tindikali endekeza vikao,! tuma msg jieleze mwanzo mwisho then waache wenyewe wayasolve.

Nailyne napata tabu kuamini hii avatar yako, wewe utakuwa mwanaume piga ua galagaza, unachosema ndicho halisi kwa mwaume , unless awe na tatizo!!!
IGWE atakubaliana na mimi!!!
 
Ku behave sio wanaume tu, mbona huyo dada aliniogesha kilimanjaro kubwa ya baridi mbele ya watu? Ila bora awepo mke wake maana mke wangu sioni anahusika vipi from the begining wenye matatizo ni sisi wa tatu.

Kwahiyo wewe ulitegemea huyo dada akuangalie tu?!Kilimanjaro aliyokumwagia imekuathiri vipi zaidi ya kipande cha sabuni cha sh. 150 ambacho bado ungekutumia kufulia na kuogea bila hata kumwagiwa kitu...?!

Nwy umeomba mchango/mawazo na mimi nimekupa yangu...sasa changanya na zako.
 
kama unataka kumwagiwa tindikali endekeza vikao,.

Sasa hapo itabidi niongee na jamaa wa boda boda aniazime Helmet nianze kutembea nayo, seriously njia ya sms bado naiona kama haita faa sana, labda inaweza tu kumpa ushahidi akitaka kuni sue, maana kuna kesi hapo akiamua kunikomoa.
 
Sasa hapo itabidi niongee na jamaa wa boda boda aniazime Helmet nianze kutembea nayo, seriously njia ya sms bado naiona kama haita faa sana, labda inaweza tu kumpa ushahidi akitaka kuni sue, maana kuna kesi hapo akiamua kunikomoa.

Then tafuta namna ya kuongea nae kwa mbali mkuu, kikao sikushauri, utaharibu....
 
Then tafuta namna ya kuongea nae kwa mbali mkuu, kikao sikushauri, utaharibu....

ngoja tuone waungwana wengine wanasemaje, mimi naona kama man on man itakuwa ndio suluhu ya kweli.
 
Nailyne napata tabu kuamini hii avatar yako, wewe utakuwa mwanaume piga ua galagaza, unachosema ndicho halisi kwa mwaume , unless awe na tatizo!!!
IGWE atakubaliana na mimi!!!

mkuu wewe sio wa kwanza ku-observe hicho kitu bt am a lady who 'think like a man n act like a lady' ha ha ha lol
 
Back
Top Bottom