Nimemwendea mke wangu kwa mganga!

Nimemwendea mke wangu kwa mganga!

Habarini wanajamvi!

Najua wengi kichwa cha habari kitawashtua maana mara nyingi au imekuwa mazoea kusikia wanawake tu ndio huwaendea waume zao kwa waganga kwa sababu mbalimbali wanazojua wao!

Mimi yamenikuta na uamuzi niliouchukua kumwendea kwa mganga hata sijutii!
kwa hali ilipofikia sikuwa na jinsi zaidi ya kumuendea huko maana ndio mwisho wangu wa kufikiria ulipofikia.

Nilishaleta uzi hapa kumuhusu huyu mke "MKE WANGU ANASHINDANA KILA KITU NA MIMI"nisiwachoshe kusoma sitaki uzi uwe mrefu kama gazeti la MZALENDO!

Huyu mwanamke alinisumbua sana ilifikie hadi kunitoroka karibu wiki nzima na ukichukulia nampenda!nikafanya maamuzi magumu nikamwendea pangani
niliporudi nyumbani nikamchomea hiyo dawa na kunuiza chumbani hapo mkumbuke nishamfata kwa shangazi yake zaidi ya mara 5 arudi hataki!nilipomaliza kunuia tu mtoto huyu hapa hajachana hata nywele kaja kama amekimbizwa
kidogo mimi nikimbie nimwachie chumba ila nikajikaza!kuna dawa ingine nilipewa ya kupaka kichwa kidogo unachanganya na asali na manuizi wakati kuduu naona mafanikio mtoto karudi anashinda tu hapo nyumbani.
Ikiisha atasepa tena kama kawaida yake,mpende akupendae asiekupenda achana nae
 
Wengi watajifanya kukandia hapa lakini nina hakika dakika hii inbox ya jamaa imejaa maombi ya maelekezo ya unapopatikana mganga.
We hujaenda pm kwa jamaa mlozi bado?
Jamaa anafurahi kugeuziwa mkewe ndondocha.
Mkewe nae atamwendea kwa mganga apewe limbwata akihofia kuachwa maana anampenda sana mumewe.
Mlishwa limbwata akilishwa itakuwaje?
Stay tuned!
 
Yaani bado sijakupatia majibu!!!natafakari
 
Komaa sana dawa likiisha utapata shida endelea kumwendea had I kufa usipofanya hivyo utakuja kuipatapata ya madawa
 
Habarini wanajamvi!

Najua wengi kichwa cha habari kitawashtua maana mara nyingi au imekuwa mazoea kusikia wanawake tu ndio huwaendea waume zao kwa waganga kwa sababu mbalimbali wanazojua wao!

Mimi yamenikuta na uamuzi niliouchukua kumwendea kwa mganga hata sijutii!
kwa hali ilipofikia sikuwa na jinsi zaidi ya kumuendea huko maana ndio mwisho wangu wa kufikiria ulipofikia.

Nilishaleta uzi hapa kumuhusu huyu mke "MKE WANGU ANASHINDANA KILA KITU NA MIMI"nisiwachoshe kusoma sitaki uzi uwe mrefu kama gazeti la MZALENDO!

Huyu mwanamke alinisumbua sana ilifikie hadi kunitoroka karibu wiki nzima na ukichukulia nampenda!nikafanya maamuzi magumu nikamwendea pangani
niliporudi nyumbani nikamchomea hiyo dawa na kunuiza chumbani hapo mkumbuke nishamfata kwa shangazi yake zaidi ya mara 5 arudi hataki!nilipomaliza kunuia tu mtoto huyu hapa hajachana hata nywele kaja kama amekimbizwa
kidogo mimi nikimbie nimwachie chumba ila nikajikaza!kuna dawa ingine nilipewa ya kupaka kichwa kidogo unachanganya na asali na manuizi wakati kuduu naona mafanikio mtoto karudi anashinda tu hapo nyumbani.
Utawahi kufa ww
 
Back
Top Bottom