Nimemzidi umri kwa miaka 12

Nimemzidi umri kwa miaka 12

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
57,761
Reaction score
216,011
Umri wangu ni miaka 44, sijaolewa na sina mtoto. Ninafanya kazi katika Taasisi ya Serikali, mwanzoni mwa mwaka huu nilipelekwa semina kwa wiki moja.

Tukiwa kule kiti changu kilikuwa karibu na kiti cha kijana mmoja, mrefu, nadhifu, mcheshi. Tulifikia hoteli moja, baada ya siku tatu tulibadilishana number za simu maana tuliweza kuelekezana migahawa mizuri kwa chakula.

Semina iliisha Ijumaa na tuliagwa kwa tafrija baada ya hapo kila mtu aliekea alikotoka.

Mimi na kijana tuliendelea kuwasiliana kwenye whatsApp, imefikia katika hali kuwa, nikiamka asubuhi lazima tusalimiane, tunabadishana picha za lunch, usiku ndio kabisa tunachat masaa mawili-matatu. Ilitokea nikamuuliza hivi unahisi mimi nina miaka mingapi?

Akajibu 28, nilicheka, nikaamua kukaa kimya. Moyo wangu umempenda sana, sasa lakini niliamua kumueleza ukweli. Alishtuka na kukaa kimya, nikajua basi ameshaondoka.

Kesho yake alinipigia simu akaniuliza kama nilishawahi kuolewa, je nina mtoto. Akajibu umri kwake sio tatizo. Yeye ana miaka 31, anakazi nzuri sana.

Weekend iliyopita alikuja kunitembelea, alifika Jumamosi asubuhi, kwa sababu bado tunafahamiana alichukua hoteli mjini, alikuja kwangu jioni, tulikaa tukaongea mpaka saa nane usiku, akaondoka kurudi hotelini kwake, kesho yake alirudi kwake.

Dada yangu mkubwa ambae mtoto wake wa kwanza ana miaka 29 ameniambia nimuache kijana kwani ni sawa na mwanangu! Kijana mwenyewe amekiri kuwa kwao wazazi wataleta zengwe, amenishauri tuzae kwanza kabla hajanipeleka kwao.

Ushauri jamani
 
Dada mpaka sa8 usiku mnaongea tuu live bila chenga wala umeme kukatikakatika??
ushauri....wewe kama mnapendana bebaneni tu muoane tena kwa shangwe zote! wambie unamiaka28! kwani wakwe watadai cheti cha kuzaliwa???
 
Hakikisha kama anajua maana ya tofauti ya umri uliopo.
Mara nyingi wanawake wanakuwa matured kuliko wanaume kama unadhani mmebalance humtreat kama bwana mdogo.
Kama unadhani unaweza kumsikiliza kama MUME na yeye sio anakupenda umlee kama mama yake na sio kuchukua rensponsibility ya MUME endleeni.

Lakini kwa uzoefu hawa vijana hupenda mteremko wewe umeshajiestablish hana shida ya kukusaidia kupata mwelekeo wa maisha hana shida ya kuhakikisha uko salama.
Lakini kuna wachache ambao wanaishi vizuri sana tu.
Inategemea unataka nini kutoka kwa mwenzi wako
 
Usithubutu kuzaa, huu ushauri wa bure tu nakupa!
Kwani wangapi wamezaa na wameachwa?.

Km kweli yupo serious na ni mpango wa Mungu itakua tu dada yangu!!...

Huyo Dada ako nae ataingiliaje mapenzi ,hajui ni makubaliano ya watu 2!
.sorry,huyo Dada ako kaolewa?

Huyo kaka anasema kwao wataleta zengwe,kwahiyo ataenda kuwatangazia ndugu zake kuwa umemzidi?..
If so,hayupo tayari kukudefend huko kwao!?

Dada Yangu muombe Mungu,ukipata amani moyoni jua ndie ,na km ndie hakutakuwa na chochote kitakachozuia,means kila mmoja wenu atakua tayari kudefen penzi lenu!!

Nb:naona anataka kujua km unaweza kuzaa.
Mtazamo wangu tu!!!
 
Hivi miaka 44 wanazaa bila shida?

nafikiri ana wasiwasi akikuoa atapata watoto?
ndo maana anataka mzae kwanza

na wewe ukuendelea kusubiri utazaa na mika 50?

nafikiri huna choice...zaa nae hata asipokuoa angalau utakua na mtoto

tena zaa nae watoto wawili kwa haraka haraka halafu muache mwenyewe aamue kukuoa au kutokuoa.....
 
Hivi miaka 44 wanazaa bila shida?

nafikiri ana wasiwasi akikuoa atapata watoto?
ndo maana anataka mzae kwanza

na wewe ukuendelea kusubiri utazaa na mika 50?

nafikiri huna choice...zaa nae hata asipokuoa angalau utakua na mtoto

tena zaa nae watoto wawili kwa haraka haraka halafu muache mwenyewe aamue kukuoa au kutokuoa.....

Na mi nimewaza hivyo,ana wasiwasi na kupata watoto!

Miaka 44 wanazaa vzr tu!!
 
Usithubutu kuzaa, huu ushauri wa bure tu nakupa!
Kwani wangapi wamezaa na wameachwa?.

Km kweli yupo serious na ni mpango wa Mungu itakua tu dada yangu!!...

Huyo Dada ako nae ataingiliaje mapenzi ,hajui ni makubaliano ya watu 2!
.sorry,huyo Dada ako kaolewa?

Huyo kaka anasema kwao wataleta zengwe,kwahiyo ataenda kuwatangazia ndugu zake kuwa umemzidi?..
If so,hayupo tayari kukudefend huko kwao!?

Dada Yangu muombe Mungu,ukipata amani moyoni jua ndie ,na km ndie hakutakuwa na chochote kitakachozuia,means kila mmoja wenu atakua tayari kudefen penzi lenu!!

Nb:naona anataka kujua km unaweza kuzaa.
Mtazamo wangu tu!!!

We dogo kumbe kichwa eeh?
 
Usithubutu kuzaa, huu ushauri wa bure tu nakupa!
Kwani wangapi wamezaa na wameachwa?.

Km kweli yupo serious na ni mpango wa Mungu itakua tu dada yangu!!...

Huyo Dada ako nae ataingiliaje mapenzi ,hajui ni makubaliano ya watu 2!
.sorry,huyo Dada ako kaolewa?

Huyo kaka anasema kwao wataleta zengwe,kwahiyo ataenda kuwatangazia ndugu zake kuwa umemzidi?..
If so,hayupo tayari kukudefend huko kwao!?

Dada Yangu muombe Mungu,ukipata amani moyoni jua ndie ,na km ndie hakutakuwa na chochote kitakachozuia,means kila mmoja wenu atakua tayari kudefen penzi lenu!!

Nb:naona anataka kujua km unaweza kuzaa.
Mtazamo wangu tu!!!



Mkuu Upo?
Ulikuwa Kimya Sana

Yaani Watu Kwenye Hii Thread Wanashangaa Huyu Dada Kuwa Na Umri Mkubwa Wakat
Haya Ni Mambo Ya Kawaida Sana

Ajaribu Kuwa Makini Shida Kubwa Watu Hupenda Slope Mno
 
Sky Eclat

Mnaweza kuoana kwasasa, ila kubali tu kesho kutwa utakapokua fifty yrs utaletewa dogo dogo ama kukimbiwa na kuambiwa kua wewe mzee na kusema alikosea kukuoa. Blive me kwa sasa kakutamani sana kwa umri uo simply bcoz hamjaishi pamoja kama husband and wife. Ukimpa amege tu na mkikaa kidogo ataanza iyo sababu ya umri,na tofauti ya umri wenu itakua silaha yake kukuadhibu.

Ushauri : Tafuta age mate wako aliyekwisha tumia ujana wake na kutulia, ambaye kwasasa hana mke, 42-50yrs uko labda ita work out,..........But imekuaje umechelewa hivi?jua limezama dada yangu dah. Anyway All the Best
 
Usithubutu kuzaa, huu ushauri wa bure tu nakupa!
Kwani wangapi wamezaa na wameachwa?.

Km kweli yupo serious na ni mpango wa Mungu itakua tu dada yangu!!...

Huyo Dada ako nae ataingiliaje mapenzi ,hajui ni makubaliano ya watu 2!
.sorry,huyo Dada ako kaolewa?

Huyo kaka anasema kwao wataleta zengwe,kwahiyo ataenda kuwatangazia ndugu zake kuwa umemzidi?..
If so,hayupo tayari kukudefend huko kwao!?

Dada Yangu muombe Mungu,ukipata amani moyoni jua ndie ,na km ndie hakutakuwa na chochote kitakachozuia,means kila mmoja wenu atakua tayari kudefen penzi lenu!!

Nb:naona anataka kujua km unaweza kuzaa.
Mtazamo wangu tu!!!

In a way tulikuwa tunaongea akaniambia ukikutana na mama yangu wakati unadamu yake mikononi hatakuwa na jinsi, aliongea kama utani lakini ilikuwa sentensi nzito
 
Back
Top Bottom