Nimenunua 'novel' ya Kiswahili nikakutana na neno 'Tafadhari' hapa naenda kudai refund

Nimenunua 'novel' ya Kiswahili nikakutana na neno 'Tafadhari' hapa naenda kudai refund

Kama mtu aliyekulia nje na mwenye nia ya kuboresha Kiswahili changu, si nikaamua ninunue novels za Kiswahili ili zinisaidie.
Yaani nimefungua tu ukurasa wa kwanza nikakutana na hilo neno hapo juu "TAFADHARI".
Hivi muandishi mzima uliyeenda shule unaweza kukosea lugha kiasi hicho. Uandishi wa namna hii ni janga kwa taifa letu na unatakiwa kupigwa vita naona watu wengi mno ni wahanga.
ELIMU ELIMU ELIMU.
Hapa niko njiani naenda kurudisha mtabu wao!
Hakika hakuna kitu nachukia kama watu kutumia lugha kipuuzi kabisa. Bora kabisa kawadai na ikibidi tuwafungulie kesi kwa kutokuitunza tunu ya Taifa.
 
Mkuu hiyo ni novel tu.. Nenda kwenye vitabu vya ziada vya mashuleni huko ndo utakimbia.. Unaweza kukutana na kitabu kwenye maswali ya mazoezi kumeandikwa rais wa awamu ya kwanza wa tanzania anaitwa (a) mkapa (b) mwinyi (c) kikwete. Afu unakutakipo shuleni kinatumika kufundishia ndo utashangaa..
 
Mimi bado najifunza ila huyu ni MWANDISHI mzimaaa! Aibu sana.
Sawa kabisa.
Ni vyema na wewe uboreshe, ukikosoa basi weka jitihada na wewe kwa upande wako.

N.b.
Inawezekana makosa ya kiuandishi sio yake bali ni ya mchapishaji. Mpe nafasi. Soma kitabu, kielewe na kama kinaeleweka unaweza kutoa mrejesho kwa manufaa ya mwandishi na wapenzi wa kusoma vitabu pia. Naamini kuna mawasiliano ya mwandishi na/au mchapishaji.
 
Back
Top Bottom