Nimepanga kuhamia Dodoma, nitoke huku niliko.

Nimepanga kuhamia Dodoma, nitoke huku niliko.

Kapange chang'ombe vyumba bei ya dezo na daladala za uhakika hadi mjin kati
 
Inaweza kuwa shiling ngapi huko
Chumba chenye umeme na kumesakafiwa kwa sumendi unapata kwa elfu 15 kwa mwezi na unakula daladala moja hadi town kati. Na in fact hii ndio mitaa yenye daladala za uhakika. Mitaa kama kikuyu, chadulu area A, Area D skuiz haina daladala.

Lakini pia kwa harakaharaka tu afungue pale banda la video aonyeshe "mpira wa ndani" atarudi kusini mihela inamuelemea kuibeba
 
Chumba chenye umeme na kumesakafiwa kwa sumendi unapata kwa elfu 15 kwa mwezi na unakula daladala moja hadi town kati. Na in fact hii ndio mitaa yenye daladala za uhakika. Mitaa kama kikuyu, chadulu area A, Area D skuiz haina daladala.

Lakini pia kwa harakaharaka tu afungue pale banda la video aonyeshe "mpira wa ndani" atarudi kusini mihela inamuelemea kuibeba
Nashukuru sana Kaka, nitayafanyia kazi mawazo yako
 
Heshima kwenu wakuu,

Bila kupoteza muda, Mimi ni kijana wa miaka 27, kwa Sasa nipo kusini mwa nchi lakini siku za usoni natarajia kuhamia Dodoma ili nipambane mbali na nyumbani.

Nimefanya maamuzi haya kwa kuzingatia Mambo mengi:

Kwanza, Dodoma Kuna fursa nyingi za kiuchumi ambazo zimechagizwa na uwepo wa watu wengi (wanafunzi wa vyuo, wabunge, mawaziri na wafanyakazi wengi wa umma). Huku kusini hasa Lindi, kusema ukweli kumesahaulika kabisa, idadi ya watu ni ndogo na mzunguko wa pesa ni mdogo sana.

Pili, Dodoma ni makao makuu ya serikali na ofisi nyingi za umma ziko Dom. Nikiwa hapo sitawaza tena kuhusu interview za utumishi ambapo awali nilikuwa siwezi kuzifanya kutokana na umbali, yaani kutoka huku kwetu hadi Dom kuja kufanya interview ingenighalimu Sana ukizingatia pia interview zinakuwa nyingi kwa post moja (oral na written)

Tatu, ninapafahamu Dodoma kwa uchache, kwasababu nimemaliza degree yangu UDOM, kwaiyo Dodoma ni jiji nalolijua.

Nne, natamani kukaa mbali na home.

Tano, nimepapenda Dodoma.

Changamoto nayoipata (swali nalojiuliza) kwa Sasa ni nini nitafanya nikiwa Dodoma? Na hapa ndio nahitaji mawazo ya wadau na wenyeji wa Dom mnipe faida na hasara, raha na shida za kukaa Dom.

Mwenyewe niliwaza kufanya shughuli hizi,

Kwanza, Bodaboda (kwakua nina kamtaji kidogo naweza nunua pikipiki yangu hata used na Kuanza nayo biashara)

Pili, kuuza nguo na bidhaa nyengine ndogondogo

Tatu, shughuli yeyote ya mtaani Kama kubeba zege, kufyatua matofari n.k.

Kwasasa najipanga ili nisije mikono mitupu katika miji ya watu, nasubiri kidogo nijichange change ili nije vizuri.

Najua huu ni mpango tu na unaweza usiwe sahihi Sana, hivyo nahitaji ushauri wenu wadau, hali ikoje hapo makao makuu? Bei za vyumba vya kupanga ikoje?
Ushauri wenu ni wamuhimu sana, karibuni wanajamiiforums
karibu Mwanza wala hautajutia ujio wako
 
Kapange chang'ombe vyumba bei ya dezo na daladala za uhakika hadi mjin kati
Nani kakudanganya?
Chang'ombe sasa hivi wanakaa sana wafanyakazi wa Serikali (wale waliokuja kuanzia 2018) ni ghali mno

Self moja inaenda kuanzia 70k kwa mwezi na ni kidogo mno unaweka kitanda cha 5/6 tv ukutani friji na kikochi vyombo utaweka nje kudaadeki na hama uone kupata kama hicho utasubiri mno
 
Ukikaribia kuja nichek nikupe room mjini kati bei nzuurii cha kuanzia maishaUmeme na maji vipo
 
Daaaah! mkuu mimi nilitegemea wakati unasoma chuo UDOM ungekuwa tayari ushafanya utafiti wa kutosha nini utafanya kwenye huo mji wakati utakapomaliza chuo. Tatizo vijana wengi wakiwa chuo hujisahau na kudhani ya kuwa wakimaliza tu chuo watapata ajira.

Binafsi wakati nasoma chuo huko Rock City nilijichanganya sana huko mtaani hasa ziwani, nilizunguka karibu mialo yote ya samaki na dagaa na kufanya tafiti zangu ili kuchek fursa, na nilianza kuchangamkia hizo fursa nikiwa mwaka wa kwanza semester ya pili. Ashukuriwe Mungu sikurudi mkoani kwangu nilipomaliza chuo, nilibaki rock city tena nilihama maeneo ya chuo na kusogea maeneo ya ziwani huko. Nilipiga biashara zangu na sikuwahi kujutia ile biashara maana ilinifanya niishi maisha mazuri tu mjini na sikuwa na ajira.

Ushauri wangu kwako ni huu hapa, tumia network yako uliyoicha huko Dodoma wakati unasoma chuo inaweza kukupa ushauri mzuri wa nini cha kufanya, licha ya hayo network hiyo pia inaweza kukupokea tena mjini na kukupa usaidizi mdogo mdogo hasa wa malazi wakati biashara yako bado changa.
 
Daaaah! mkuu mimi nilitegemea wakati unasoma chuo UDOM ungekuwa tayari ushafanya utafiti wa kutosha nini utafanya kwenye huo mji wakati utakapomaliza chuo. Tatizo vijana wengi wakiwa chuo hujisahau na kudhani ya kuwa wakimaliza tu chuo watapata ajira.

Binafsi wakati nasoma chuo huko Rock City nilijichanganya sana huko mtaani hasa ziwani, nilizunguka karibu mialo yote ya samaki na dagaa na kufanya tafiti zangu ili kuchek fursa, na nilianza kuchangamkia hizo fursa nikiwa mwaka wa kwanza semester ya pili. Ashukuriwe Mungu sikurudi mkoani kwangu nilipomaliza chuo, nilibaki rock city tena nilihama maeneo ya chuo na kusogea maeneo ya ziwani huko. Nilipiga biashara zangu na sikuwahi kujutia ile biashara maana ilinifanya niishi maisha mazuri tu mjini na sikuwa na ajira.

Ushauri wangu kwako ni huu hapa, tumia network yako uliyoicha huko Dodoma wakati unasoma chuo inaweza kukupa ushauri mzuri wa nini cha kufanya, licha ya hayo network hiyo pia inaweza kukupokea tena mjini na kukupa usaidizi mdogo mdogo hasa wa malazi wakati biashara yako bado changa.
Nashukuru sana, ni ushauri wa kiwango Cha SGR
 
Dodoma unaweza ukakaa bila kula na watu wanakuangalia tu!! Watu ni wachoyo sana
 
Dodoma njoo uku unaconnection ya kufikia,na mwenyej wa kukupa michongo inayoendelea wanavyuo wanaosomea udom wengy wao hamuijui ddma vzuri maana hamchangaman Sana uraian,
Cha msingi tafuta mwnyeji kuusu chumba vipo ad vya 20k wasikutishe lkn kzuri n kuanzia 50k
 
Back
Top Bottom