Mkuu naomba kuchangia kidogo...
Kwa kuwa una GODOWN tayari Ukitaka faida kubwa kwenye biashara ya mchele ni bora ukanunua mpunga toka pale IFAKARA ukauhifadhi mpaka msimu chakula kikiisha mashambani ukawa unaukoboa kidogo kidogo mwenyewe unaingiza sokoni..faida huwa ni kubwa mno ukilinganisha na mtu anayenunua mchele na kuuza mchele..
Ukinunua mchele na kuuza unakua huna tofauti na mchuuzi wa biashara ya maji anayetembea kutwa nzima na maji ya chupa wakati faida ni tsh 30 hadi 100 kwa chupa moja wakati huo huo barekhsa anaingiza tsh 300 kwa chupa moja ya maji.
Maeneo mazuri ya kupata mpunga mzuri wa BIASHARA kama una usafiri mzuri ni IFAKARA kama unaelekea MAHENGE ukishavuka tu mto KILOMBERO kama unatokea IFAKARA MJINI uliza eneo moja wanaita MASHAMBANI, ni maarufu sana wenyeji watakuelekeza... Kawaida ya biashara ya kununua mpunga kuukoboa na kuuza ,SHILLINGI inazaa shillingi so kama utachukua mzigo say wa million 7 tegemea kupata millioni 14 mwisho wa msimu... Ukishamaliza mzigo woote tafuta tena mazao mengine yaliyo katika msimu huo basically alizeti ..usiache fedha ikakaa idle ukisubiri msimu mwingine(hiyo ndio siri ya biashara ya mazao)..
Wazo lako ni zuri sana, Fanya hivo mkuu usife moyo mkuu, asilimia kubwa ya watu wasio na entrepreneurship spirit(wanaopenda kazi za kulipwa mishahara mwisho wa mwezi) ni wazuri sana katika analysis hasa za hasara na kukatika mtaji lakini ni ZERO katika ACTIONS. Ukiwasikiliza sana utakufa masikini ukisubiria kiinua mgongo cha JK...