Nimepata mil 10 ghafla, nataka ninunue mchele kisha niuze mwezi 10. Je, kuna zao lingine bora zaidi?

Nimepata mil 10 ghafla, nataka ninunue mchele kisha niuze mwezi 10. Je, kuna zao lingine bora zaidi?

Mkuu hiyo biashara ni nzuri ila nakushauri usiweke mayai yote kwenye kapu moja nunua mpunga wa 5M na Mahindi ya 5M itakulipa tu asikukatishe tamaa mtu swala la msingi katika biashara ya mazao ni kwamba si rahisi kupata hasara don't give up keep the spirit high,keep the faith,Keep the fight
 
Wadau ktk muda ambao sikutarajia nimepata mil 10 kutokana na mikopo kwa wafanyakazi niliopewa na benki yangu kama mfanyakazi - sikutegemea kabisa japo nilikuwa natafuta fedha hizi muda mrefu.
Sasa nataka niende Morogoro ninunue mchele kisha niweke ktk Godown halafu nitauza bei ikipanda. Kwa sasa ndo wazo nililo nalo. Je, kuna mtu mwenye wazo bora kuliko hilo? Au je biashara hii ina changamoto gani?

Je, huko kwenye godown kuko salama?
Je, hakuna uwezekano wa bei kutopanda?
Niliwahi kufanya biashara ya namna hii Upande wa Mahindi huko Arusha miaka mingi. Sina uzoefu wa mchele. Naombeni ushauri wenu.

Fanya hiyo biashara ya mchele sawa lakini kumbuka kudiversify your business..Mil 10 inatosha kwenda na mfano mpunga, mahindi, na vinginevyo..mchele ukishuka bei unakuwa na back up plan la sivyo you will live by mchele business and die by mchele business.
 
Ni PM nikuelekeze mademu wazuri na mastaa wa bongo moviez wanaojiuza walipo...Walahi jioni haifiki ushamaliza hiyo 10m.
 
Wazo zuri sana Moriah.

-Cha msingi nikupata wenyeji ambao ni waaminifu kwakua wewe ni mgeni ktk biashara hiyo maana uwa kuna tabia ya wanunuzi(wale uwatumao kwenda shambani) kupotea na hela
-Ifakara mjini sio sehemu nzuri ya kununua mpunga,ningekushauri uingie chaka kama malinyi,mtimbila,chita hayo ni maeneo ambayo utapata mpunga kwa bei rahisi na kwa wingi wakati mmoja
-Ifakara hua hamna utapeli wa Godown,na ni sehemu nzuri yakuhifadhia maana wateja wengi wakati wa uuzaji hua pale na pia hawakuchaji dhaidi watataka ukoboe kwao wakati wa kuuza
-Usipokua na tamaa ya bei kupanda sana mara nyingi utapata faida tuuu
 
Kipindi hichi sii cha kununua mazao ni mpaka july!nenda kawakopeshe wakulima sh 40,000 kwa gunia la mpunga july wakivuna, ambapo hapo hapo shambani utauza gunia sh 80,000

Hi, nimependa ushauri wako huu nina hamu ya kujua zaidi inakuwaje je kuna mikataba mtu anaweza copy akawaana tumia? Na wapi mashambi wanapokopa? In short ningefurahi kama ungnipatia maelezo. Nina ndugu yangu jobless labda kazi hii ya kufatilia itamkeep busy na kumfanya ajitegemee.
 
Mkuu naomba kuchangia kidogo...

Kwa kuwa una GODOWN tayari Ukitaka faida kubwa kwenye biashara ya mchele ni bora ukanunua mpunga toka pale IFAKARA ukauhifadhi mpaka msimu chakula kikiisha mashambani ukawa unaukoboa kidogo kidogo mwenyewe unaingiza sokoni..faida huwa ni kubwa mno ukilinganisha na mtu anayenunua mchele na kuuza mchele..
Ukinunua mchele na kuuza unakua huna tofauti na mchuuzi wa biashara ya maji anayetembea kutwa nzima na maji ya chupa wakati faida ni tsh 30 hadi 100 kwa chupa moja wakati huo huo barekhsa anaingiza tsh 300 kwa chupa moja ya maji.

Maeneo mazuri ya kupata mpunga mzuri wa BIASHARA kama una usafiri mzuri ni IFAKARA kama unaelekea MAHENGE ukishavuka tu mto KILOMBERO kama unatokea IFAKARA MJINI uliza eneo moja wanaita MASHAMBANI, ni maarufu sana wenyeji watakuelekeza... Kawaida ya biashara ya kununua mpunga kuukoboa na kuuza ,SHILLINGI inazaa shillingi so kama utachukua mzigo say wa million 7 tegemea kupata millioni 14 mwisho wa msimu... Ukishamaliza mzigo woote tafuta tena mazao mengine yaliyo katika msimu huo basically alizeti ..usiache fedha ikakaa idle ukisubiri msimu mwingine(hiyo ndio siri ya biashara ya mazao)..

Wazo lako ni zuri sana, Fanya hivo mkuu usife moyo mkuu, asilimia kubwa ya watu wasio na entrepreneurship spirit(wanaopenda kazi za kulipwa mishahara mwisho wa mwezi) ni wazuri sana katika analysis hasa za hasara na kukatika mtaji lakini ni ZERO katika ACTIONS. Ukiwasikiliza sana utakufa masikini ukisubiria kiinua mgongo cha JK...

Mkuu maelezo yako yametulia na yapo detailed sana. Mara nyingi ushauri wa mawazo ni muhimu na maradufu kuliko wa-kimaterial!
 
Wadau ktk muda ambao sikutarajia nimepata mil 10 kutokana na mikopo kwa wafanyakazi niliopewa na benki yangu kama mfanyakazi - sikutegemea kabisa japo nilikuwa natafuta fedha hizi muda mrefu.
Sasa nataka niende Morogoro ninunue mchele kisha niweke ktk Godown halafu nitauza bei ikipanda. Kwa sasa ndo wazo nililo nalo. Je, kuna mtu mwenye wazo bora kuliko hilo? Au je biashara hii ina changamoto gani?

Je, huko kwenye godown kuko salama?
Je, hakuna uwezekano wa bei kutopanda?
Niliwahi kufanya biashara ya namna hii Upande wa Mahindi huko Arusha miaka mingi. Sina uzoefu wa mchele. Naombeni ushauri wenu.

ulikuwa unazitafuta kwa muda mrefu ili iweje?
 
Wadau ktk muda ambao sikutarajia nimepata mil 10 kutokana na mikopo kwa wafanyakazi niliopewa na benki yangu kama mfanyakazi - sikutegemea kabisa japo nilikuwa natafuta fedha hizi muda mrefu.
Sasa nataka niende Morogoro ninunue mchele kisha niweke ktk Godown halafu nitauza bei ikipanda. Kwa sasa ndo wazo nililo nalo. Je, kuna mtu mwenye wazo bora kuliko hilo? Au je biashara hii ina changamoto gani?

Je, huko kwenye godown kuko salama?
Je, hakuna uwezekano wa bei kutopanda?
Niliwahi kufanya biashara ya namna hii Upande wa Mahindi huko Arusha miaka mingi. Sina uzoefu wa mchele. Naombeni ushauri wenu.

Kwakuwa ni fedha za mkupuo na Huna malengo nazo madhubuti. Ni bora ufanye investment isiyo na Risk Hata kidogo, Biashara za kukurupuka unaweza kujikuta Mtaji umekatika, biashara imekufa na Hela bado unadaiwa na Bank...
Ushauri wangu: Tafuta Kiwanja chenye HATI (Title Deed), Either Gezaulole (kigamboni), Buyuni (chanika), Au kokote kule Dar Es Salaam unakoweza kupata Kiwanja chenye hati kwa bei hiyo.

Endelea na Kazi yako kama kawaida huku unafanya utafiti wa nini cha kufanya na hiyo pesa yako. Viwanja Huwa havishuki bei, japo sometimes vinachukua muda kuuzika...Ukishakuwa na action plan ya kutosha na kueleweka. Kiuze Utapata faida kidogo na pesa zitakuwa salama. NB: Kama Ukifanikiwa kukaa na kiwanja chako kwa Miaka miwili, unaweza kujikuta unakiuza kwa mil20.... And who knows, unaweza kubahatisha pesa nyingine za mkupuo ukakijenga na kusahau habari za biashara... hii itakuwa pensheni yako... (lol)
 
Back
Top Bottom