Nimependwa na jimama nifanyeje?na kuna tetesi kuwa mme wake alikufa kwa ugonjwa wa ukimwi

Ebu fikiria mzazi wako (babako/mamako) anakuja kusikia kuwa unatembea na jimama mwenye umri kama wake, atajiskiaje? atakuonaje mwanawe?

Halafu jimama lenyewe lina backgrond mbaya!
 
Kama unampenda mwambie mkapime kwani mapenzi hayaangalii umri. Halafu usiwe na nidhamu ya woga mwendapole sifa ya kwanza ya msomi wa chuo kikuu ni kujiamini ww utakuaje muoga hvyo!! Inamaana hata mtu mzima akitaka kukukameruni utasita kukataa kwa woga au?
 
Kama unamtaka, na hasa kama unampenda pia, nendeni mkapime ngoma. Ikiwa unataka ile hit and run, potelea.
 
Zaari kama hiyo igeniangukia mimi duh,huyo rika yako kabisa chamsingi mukapime ujitambue ule baata kwa amani.
 
Mwendapole bana yaani issue ndogo unakimbia kuja kuomba ushauri.
Hapa ni kwamba nawe umezimika kwa huyo mama,solution ni kuwa nendeni mkapime ili ufaidi tunda,umri kitu gani bana,kwani huyo mama hajui wewe ni mdogo?Pia kumbuka solution ya kupima sio rahisi kihivyo huenda wote wawili ikawashinda,basi tumia SALAMA CONDOM,sijui siku hizi mnaziitaje.

Ala,yaani mtoto analilia wembe halafu unakuja kutuomba ushauri,kula maini,usisahau kinga tafadhali.
 
achana na majimama endelea na mpenzi wako kwan hilo jimama litakuambukiza tu ukimwi na kukuacha.
 

Mwendapole nenda polepole
 
Hivi hawa ndo viongozi wetu wa kesho?hata huo u CR wamekupendelea tu, hufai kuongoza watu wakati huna maamuzi. Hivi tukikushauri utembee na huyo mama utakubali??? je tukikuambia achana naye utakubali??? Ulitakiwa kufanya maamuzi mapema co unakuja kuomba ushauri huku. Jitambue kijana, umeenda chuoni kusoma na sio mapenzi. Hivi kila mwanamke atakayekutaka utamkubali???au utakuja huku JF kuomba ushauri???? Kuwa na msimamo kijana, usije juta baadae!!!!
 
Jilipue, kwanza dawa ya ukimwi inapatikana soon,trust me! Si umesema una shida (ya lift)?

duuuuuuu! madam ni kama na wewe unapalilia njia yke ya kufka haraka kwa Muumba!
 
Nina kila sababu ya kuamini kuwa mfumo wetu wa elimu umekufa........yaani mwanafunzi wa chuo kikuu mwaka wa pili unaomba ushauri kwenye jambo kama hili ambalo common sense tu ingetosha kufanya maamuzi?

1. Jimama.
2. Mumewe inasemekana alikufa kwa ngoma ++++++++.

Mbona decision variables ni chache sana kukufanya ushindwe kujua optimal solution? Embu fikiria kidogo halafu uje utuambie umeamua nini then tutakushauri kama ni uamuzi sahihi au la!
 
Jilipue, kwanza dawa ya ukimwi inapatikana soon,trust me! Si umesema una shida (ya lift)?

yap. Akishajilipua asubuhi anawahi hospitali. Kuna dawa ya kuzuia maambukizi ndani ya 3days.
 
Mdanganye kuwa wewe unaishi kwa matumaini( yaani mdanganye kuwa una ngoma) alafu uone atasemaje.
 

Mwambie kwanza akununulie usafiri halafu mkacheki ngoma akiwa +ve ndoo nitoleee hakuna kumrudishia huo usafiri
 

wewe kijana hivi ni kweli hata hiyo miaka 2 ya kuwa chuoni haijakusaidia? Wewe sema kama unamtaka huyo mama na si kutafuta ushauri wa kukuingiza motoni. wewe toka lini mtu wa admnistration akawa na impact kwenye shule yako? Na kama ni mlimani (udsm) yeye ataweza ku-access masomo yako vipi wkt walimu husika ndiyo wanaopost matokeo kwenye aris? wewe kwa tamaa zako za pesa na ngono unaelekea kutotimiza malengo yako. Hivi, wazazi wako wapo? Je, una wadogo zako? Je, una malengo gani ktk maisha yako? Hivi ukimwi unaujua au unasikia tu kwenye midomo ya watu au vyombo vya habari? panga weekend mmoja uende muhimbili kwenye wodi ya wenye ukimwi ili ujue nini maana ya ukimwi, then utafanya maamuzi ya kutaka kuwa na uhusiano na huyo mama.
Ushauri wangu kwako; acha tamaa na elekeza nguvu zako kwenye shule yako, kwani ndiyo urithi pekee utakaokusaidia kwenye maisha yako. Kuhusu shule hilo unajua kwamba waalimu ndiyo wana-access kwenye aris na si watu wa utawala.
 

mwendapole; achana kabisa na wazo la kwenda kupima, kwani mama kama huyo huwezi kujua network yake na malengo yake kwako. Anaweza akacorrupt hata huko hospitalini ili majibu yawe negative. Na inavyoelekea huyo mama unamwogopa, hivyo huwezi kuwa na ujasiri wa kumwambia mkapime.
Pia, kitu kingine ni cha ajabu ni wewe kuwa na data za huyo mama kwamba mme wake alifariki miaka 3 iliyopita kipindi wewe haujajiunga chuo. Pia ni mtu wa utawala-hakika mdogo wangu unanipa mashaka na unakoelekea. Nimeandika tena kwasababu nasukumwa kukusaidia ili uweze kutimiza malengo yako ya shule. Tafadhali sana mdogo wangu, achana na huo mpango bado una future. Zingatia masomo yako na soon utaweza kutembelea gari nawe.
 

wanaume tukitongozwa tunakuwa wapoleeeeeeeeeeee. afikiria pale alipokuwa anasema anakupenda hali ilikuaje kwao.
 
Kula kitu roho inapenda ila ujue unachezea shilingi chooni
 
Kula kitu roho inapenda ila ujue unachezea shilingi chooni
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…