Nimerejea kutazama 'Video' mbalimbali za Hayati Rais Dkt. Magufuli niseme tu Samahani kwa 'Kumkosoa' ila Asante Mungu kwa 'Kutuzawadia' Rais kama yeye

Pole sana mkuu, Binafsi Magufuli naamini ndiye Rais bora ambae aliiwaza Tanzannia ya miaka 2050, Magufuli alikuwa kiongozi sema Watanzania wengi wanataka wanasiasa.

Hii picha hapa chini iko ndani kwangu tena chumbani kwangu!

 
Haya majibu wa nayo wakazi wa Kimara,Walio ajiliwa na vyeti vya darasa la saba,wafanya kwzi wa umma ambao wana jua maana ya madaraja
 
Tangu mwaka uanze nahisi huu ni uzi wako wa maana kuliko zote.

Anyway binafsi jpm nillikuwa namkubali kawaida tu hasa nikiwa sehemu ya changanyikeni kama humu, nilikuwa simchukii kama wengine, kuna vitu alikuwa akifanya nasema huyu kweli rais hata kama sisem ila moyoni nasema hili jembe.

Siku niliposikia habari za kifo chake trh 9 nilisikia maumivu ambayo sikujua yametoka wapi.

Miliogopa hata kumwambia mtu yeyote maana alienihakikishia kafa alinitaka nifunge mdomo wangu.
Nilikuwa nikiingia humu nakuta watu wanachangia nyuzi kibao eti jpm yupo wapi na mimi najilazimisha kuchangia as if sijui kinachoendekea.
Pili moyo haukuamini nilichoambiwa nikawa akisemea ' huyu mbwa nae mwongo jpm atakufaje kizembe hivi?

Siku moja nikataka kumwambia mama yangu moyo ukasema hapana yupo hai yule fala mzushi.
Trh 17 usiku nikaota eti kafa nikastuka usingizini nikajisemea hapana ni nawazo yaliyo kichwani mwangu coz nishapewa hiyo habari wiki moja kabla.
Niliamka nikapiga magoti nikasali mikasema hii ndoto isiwe kweli, nikaingia jf nikakuta mtu kapost eti kwa nini wasitangaze tu rais kashakufa kha! Ndo niliamini yale maneno.

Baada ya kutangaza nilipata maumivu ambayo sikujua yametoka wapi, maana niliona Tanzania ambayo jpm alikuwa akiitengeneza ikiyeyuka.

Niliona ujinga ukirudi kwa kasi, wizi, miradi yake ikifa, nidham ya watumishi ikirudi 0, ufisadi nje nje , majambazi wakirudi kwa kazi, unyanyasaji wa wanyonge, viongozi kula mishahara ya bure,kupewa kazi kwa kujuana, vyeti feki,
Nikaona lile genge sugu la majambazi wanaotesa nchi wakifurahia kifo chake, nililia sana nikasema Mungu alitupa malaika ila wengi tulichukulia poa.
Huko ulipo jpm ulale salama, hakuna siku imepita bila kukukumbuka. Binafsi nimekumiss sana.

Rip jpm.
 
Nchi zilizoendelea ukiondoka madarakani au ukifariki wanakuwa wamemaliziana na wewe, sisi tunaendelea kuwa na matumaini kuwa atatukomboa!
 
Pole sana, Yule alikua rais Chuma kweli kweli. Best president wa muda wote. Keep Resting In Peace Legend.
 
Chuma kile, kiboko cha PUMBAVU hizi...

Jambo ambalo watu wengi wanaliletea mzaha ni kufikiri demokrasi ya mzungu ya kubembelezana na kuleana leana ndio italeta maendeleo Africa..

Africa inahitaji Ubabe, unyama na kila aina ya ukatili kwa watu wake ambao wengi wao ni wapumbavu ili maendeleo ya kweli yapatikane..

RIP JPM...
 
Sijawahi kuwa mnafiki juu ya JPM hakika yule alikuwa ni mwanaume wa shoka hotuba zake zilitikis na zilivutia, wazungu na wawekezaji makanjanja waliufyata, majirani waliufyta wanyonge walipeta, wezi walipata tabu sana, alitujengea heshima na misingi ya kizalendo.

Kelele nyingi dhidi yake zilipigwa na wale waliozoea maslhi binasfi. Embu tuwe na utaratibu wakumsifia mtu akiwa hai sio mpaka afe. Chini ya JPM hakika nchi ilijengw kwa kasi kubwa sana, kila mkoa ulifaidika kama sio hospitali basi ni stendi, soko au barabara za lami. Alale salama Mwamba.
 
Angalau mmoja mmoja anaanza kuona umuhimu wake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…