Nimerudi kazini sijamkuta mke wangu, nauliza majirani naambiwa ameondoka kwenda kwao

Nimerudi kazini sijamkuta mke wangu, nauliza majirani naambiwa ameondoka kwenda kwao

Dezoizo52

JF-Expert Member
Joined
Jan 30, 2017
Posts
528
Reaction score
1,070
Nafanya kazi mbali na ninapoishi kwa hiyo huwa ninalala huko ninakofanyia kazi ambako nimepanga chumba cha dharura.

Siku ya jtano wiki hii niliagana na mke wangu kuwa naelekea kazini na nitarudi siku ya alhamisi au ijumaa akaitikia na tukaagana vizuri.

Mshtuko wa moyo nilioupata ni pale nilipojisikia kurudi siku ya pili yake yaani Alhamisi baada ya kugonga mlango kwa muda bila majibu nikaamua niulize jirani aliko mke wangu, najibiwa jana ulipoondoka mkeo nae kasafiri ila funguo hizi hapa. Nilihisi kuishiwa nguvu lakini nilijikaza nikachukua ufunguo taratibu nikaingia ndani kiukweli sijaamini macho yangu hakukua na kitu chake hata kimoja zaidi ya kuniachia picha za ndoa.

Nimeumia sana na huo ulikuwa mwisho wa kupata usingizi hadi sasa. Nimempigia simu lakini haipatkani, ndugu zake hawajui yuko wapi ila leo hii Jumamosi mpangaji mmoja kanionea huruma kaniambia aliongea na mke wangu siku ya Alhamisi jioni na alimfahamisha kuwa anakaribia kufika kwao Chamwino Dodoma akitokea kwetu Mtwara.

Lakini kwao nikiuliza naambiwa haonekani na simu hapatikani, sijui cha kufanya kwanini mke wangu wa ndoa lakini amenitoroka. Naombeni mnishauri nini nifanye kwa kuwa suala hili limevuruga kichwa changu.

Mara ya mwisho kuwasiliana nae ilikuwa jioni Alhamisi kwa kum SMS kupitia private Facebook nikamuuliza uko wapi? Akanijibu kwa kifupi "my lovely husband ".Mpaka sasa simpati kwa simu.
 
Pole sana mwanajf mwenzangu!
Sijui mlikuwa na ugimvi kabla ya yeye kutoroka kama upo wala usiumie tafuta namna ya kumpata na kusolve lakini kama kaondoka kwa sababu zake binafsi mwache aende atarudi akichoka
 
Pole sana mwanajf mwenzangu!
Sijui mlikuwa na ugimvi kabla ya yeye kutoroka kama upo wala usiumie tafuta namna ya kumpata na kusolve lakini kama kaondoka kwa sababu zake binafsi mwache aende atarudi akichoka
Hatukua na ugomvi kwa kuwa tuliishi vizuri tuu ila huko kipindi cha nyuma tuliwahi kukwaruzana kama sehemu ya binadamu. Vipi kuhusu ndugu zake wanaomtafuta niwajibu nini?
 
Hatukua na ugomvi kwa kuwa tuliishi vizuri tuu ila huko kipindi cha nyuma tuliwahi kukwaruzana kama sehemu ya binadamu. Vipi kuhusu ndugu zake wanaomtafuta niwajibu nini?
saa unataka uwajibu nini zaidi ya kuwaambia hali halisi

weee usijal kwa kuwa kaondoka mwenyewe atarudi mwenyewe
 
Hatukua na ugomvi kwa kuwa tuliishi vizuri tuu ila huko kipindi cha nyuma tuliwahi kukwaruzana kama sehemu ya binadamu. Vipi kuhusu ndugu zake wanaomtafuta niwajibu nini?
Mkuu mtwara upo sehemu gani Kuna Bar pale maeneo ya nangwanda inaitwa shooters, kesho Kuna Manchester united vs Manchester City saa 1 usiku, tujumuike pale pamoja Kupata ulabuu mkeo kwa kifupi tuu anatafuniwa Sasa na hii hali ya hewa za mvua mvua na anatafunwa huko alipo.
 
Hatukua na ugomvi kwa kuwa tuliishi vizuri tuu ila huko kipindi cha nyuma tuliwahi kukwaruzana kama sehemu ya binadamu. Vipi kuhusu ndugu zake wanaomtafuta niwajibu nini?
Pole sana,kuachwa kunauma kuliko watu wengi wanavyodhani.
Jaribu kutuliza kwanza kichwa chako, ukikosa mawasiliano na mkeo mpaka kesho kutwa na ndugu zake wakadai hajafika kwao,nenda karipoti polisi.
 
Pesa niliacha na hakuchukua hata sent yangu.
Aisee ,,, tuliza kichwa,,,,,ila wataarif wazaz wake na ueleze tukio lilivyotokea, endapo km yupo sehem nyingine akipatwa na majanga wajue hajapatia kwako
 
NENDA POLISI TOA TAARIFA MAPEMA, HATA KAMA AKIRUDI KWAKO, HUYO NI NYOKA MBAYA SANA, ACHANA NAYE. BAHATI MBAYA UKRISTO UNAZUIA, ILA AFYA YAKO YA MWILI NA ROHO NI MUHIMU NDUGU YANGU. KUFA UKIJIONA KUBAYA SANA.
 
Back
Top Bottom