Nimesajili kampuni ya Ujenzi wa Majengo na Barabara

Nimesajili kampuni ya Ujenzi wa Majengo na Barabara

Hongera kwa kuthubutu, wengi tunaogopa kuanza, endelea kuonyesha njia kwa watanzani.
 
Wadau wakati huu naombeni kuwajulisha kuwa nimefanikiwa kusajili kampuni ya Ujenzi katika majengo na barabara daraja la saba ,lakini ni matarajio yangu ku upgrade kuwa daraja la Tano muda ni mrefu.Nakuombeni ushirikiano ili kuweza kujenga Taifa letu na kuongeza ajira kwa watz.Nategemea kufikia mwanzoni mwa mwezi April mambo yote yatakuwa yamekamilika na kuanza kupiga mzigo.

Habari kiongozi. Nimejaribu kukutumia PM lakini haziendi... Tunaweza kuwasiliana?
 
mkuu ndo umetupa kabisa ukiwa unahitaiji huduma za kutengenezewa receipt book, forms, delivery note tuonane tufanye biashara
Hongera mkuu kwa hatua hiyo,
ukiwa unahitaji kupurchase vifaa used heavy duty machine kama excavator, crane,loader etc nitaarifu nikupatie huduma hiyo.
Nami nipo ktk construction industry ila upande wa kuuza used heavy duty machines
 
Naomba kukuuliza kama nina kiwanja akijapimwa nataka kujenga ghorofa ,je ofisi yako inashughulikia vibali vya ujenzi kama huo?na kibali kipi na kipi hapo kinahitajiwaili ujenzi uanze?
 
Naomba kukuuliza kama nina kiwanja akijapimwa nataka kujenga ghorofa ,je ofisi yako inashughulikia vibali vya ujenzi kama huo?na kibali kipi na kipi hapo kinahitajiwaili ujenzi uanze?
kibali kinachohitajika ni kimoja ambacho ni building permit kinatolewa nA halmashauli ya mji ambayo kiwanja chako kipo. Ila kibali hicho kinatolewa kama kiwanja chako kimepimwa na kina hati.hapo inabidi upeleke ramani ambazo ziko stamped na registered architect na kwa vile unajenga gorofa inabidi pia uwe na ramani za structure ambazo ziko stamped na registered structure engineer. Sasa kwa vile kiwanja hakijapimwa anza na kumtafuta surveyor akupimie kwanza halafu mengine ndiyo yafuate.Vinginevyo unaweza ukafanya investment yako at your own risk
 
Huyu mjomba tangu afungue kampuni amepotea hapa jukwaani
 
Back
Top Bottom