Nimeshangaa sana NSSF, asilimia kubwa wanaodai mafao ni vijana na si wazee kama ilivyokuwa zamani

Nimeshangaa sana NSSF, asilimia kubwa wanaodai mafao ni vijana na si wazee kama ilivyokuwa zamani

Deceiver

JF-Expert Member
Joined
Apr 19, 2018
Posts
9,446
Reaction score
17,017
Juzi Kati nikiwa kwenye jiji la maraha niliingia kwenye ofisi moja ya mkoa ya NSSF. Nilichokuta pale kilinishangaza sana, kulikua na watu wazima wawili wengine wote zaidi ya 50 ni vijana under fourty years. Wote wamesimamishwa kazi wamekuja kudai mafao.

Ilibidi yule Askari wa Suma pale getini awe na kazi ya ziada ya kuruhusu waingie kumi kumi kupunguza msongamano ndani.

Zamani NSSF ulikua hukuti mtu asiye na mvi au kipara. Leo hii wanaodai mafao vichwani ni viduku na Rasta kwa wadada kichwani ni twende kilioni.
 
Back
Top Bottom