Nimeshangazwa na Ushuru wa serikali wa kulipia mabango ambayo yapo kwenye biashara yako, mfano juu ya paa la sehemu yako ya biashara!

Nimeshangazwa na Ushuru wa serikali wa kulipia mabango ambayo yapo kwenye biashara yako, mfano juu ya paa la sehemu yako ya biashara!

Bongo biashara zinazo survive ni zile zenye uwezo wa kutoa support ya kifedha kwa mboga mboga political party
 
Wakuu,

Watu kutoka manispaa za Kinondoni na Temeke wamekuwa na hekaheka za kwenda kwenye sehemu za wafanyabiashara, maarufu kama fremu na kupima mabango ambayo yapo kwenye sehemu za biashara, na kuadai yalipiwe. Hizo ni sheria za manispaa.

Najiuliza sana, kuwa bango lengo lake ni kuelekeza wateja kuwa kuna huduma fulani sehemu, wakishapata huduma hiyo, mwenye biashara analipa kodi na maushuru kibao serikalini, chahce tu ni kodi ya TRA, service levy - halmashauri husika, leseni, withholding tax, kodi ya pango, tozo kibao, usafi, nk.!

Sasa hapa inategemea na aina ya biashara, zingine zina msururu wa kodi na ushuru na vibali mpaka unajuta!

Huu ubunifu ni wa serikali yetu, mtu binafsi au ni nini hiki?

Kama bango lipo eneo la serikali, mfano yale makubwa barabarani kulipia sikatai, lakini bango lipo exactly sehemu yako ya biashara na tayari unalipa kodi na maushuru ya kufa mtu!

Mbona tunaua biashara kwa makusudi?

Tujadili.

tf.
Hawa wapumbavu wameniletea bill ya 850,000/= @?>?@@>>?@@@@@@@ zao!
 
Kuna tatizo kubwa nchi hii kuliko nilivyodhani mwanzoni.
 
Halafu mtu anakuja na kauli kwamba tanzania walipa kodi ni milioni 2 tu.

Mapapa na manyangumi yalitetewa na bosi alipoingia madarakani tu kuwa yasisumbuliwe ktk kodi. Sie vidagaa wacha tukamuliwe utumbo.
Moja ya dalili ya serikali corrupt ni kuhangaika na vidagaa huku wakiwaacha mapapa yakitanua matamvua,
 
Wakuu, Watu kutoka manispaa za Kinondoni na Temeke wamekuwa na hekaheka za kwenda kwenye sehemu za wafanyabiashara, maarufu kama fremu na kupima mabango ambayo yapo kwenye sehemu za biashara, na kudai yalipiwe. Hizo ni sheria za manispaa. Najiuliza sana, kuwa bango lengo lake ni kuelekeza wateja kuwa kuna huduma fulani sehemu, wakishapata huduma hiyo, mwenye biashara analipa kodi na maushuru kibao serikalini, chahce tu ni kodi ya TRA, service levy - halmashauri husika, leseni, withholding tax, kodi ya pango, tozo kibao, usafi, nk.! Sasa hapa inategemea na aina ya biashara, zingine zina msururu wa kodi na ushuru na vibali mpaka unajuta! Huu ubunifu ni wa serikali yetu, mtu binafsi au ni nini hiki? Kama bango lipo eneo la serikali, mfano yale makubwa barabarani kulipia sikatai, lakini bango lipo exactly sehemu yako ya biashara na tayari unalipa kodi na maushuru ya kufa mtu! Mbona tunaua biashara kwa makusudi? Tujadili. tf.
 
Ongezea na roho mbaya ya uhasidi
Hivi mtu kaandika nje nashona nguo halafu hajashona wiki
Wanadai hela ya bango kama sio uchawi ni nini?
Walivyo lewa na madaraka wanatamani hata hizi sehemu zetu waziweke mabango Yao ya mamasamia. Unajua kuna Ile mtu unanufaika na kitu mpaka unaona wengine wanapoteza mda ndio CCM Sasa inaona siasa uchwara kua ndio ajira
 
Walivyo lewa na madaraka wanatamani hata hizi sehemu zetu waziweke mabango Yao ya mamasamia. Unajua kuna Ile mtu unanufaika na kitu mpaka unaona wengine wanapoteza mda ndio CCM Sasa inaona siasa uchwara kua ndio ajira
Yaani miaka yote tutakuwa masikini wa kifikra tu
Wao wanaona wanakomoa wananchi ila hawajui wanawakomoa mpaka mama zao
 
Tatizo ni kuwa na watu wasiokuwa wabunifu na wwshamba ambao badala hata ya kujisomea zaidi na kuangalia nchi zinazoendelea zinaingiza namna gani mapato yao miji?
Lazima kuangalia wapi pa kuzipata na zinasaidiaje
Hizo hela zinaishia kwa watu wachache na sio ubunifu kabisa
Kuna mabango barabarani ya Rais yapo kila sehemu hayo nani analipia kuwepo hapo na ni sh ngapi
Ubunifu ni akili ambayo wengi hawana
Mkuu, costs of advertising and marketing dunia nzima hutozwa levy.
 
Ukweli mchungu ni kwamba. Kwa Tanzania yetu hii mfanyabiashara akiwa mwaminifu kwa kulipa kodi kama inavyotakiwa basi miezi 6 haitoisha atakuwa ashafunga biashara.


Namfahamu mfanyabiashara mmoja (aliyefilisika) ambaye niliwahi kufanya naye mahojiano. Alilalamikia mifumo kandamizi ya kikodi ambayo ipo ikiwemo hilo la kodi ya mabango na tena kuna kupigwa faini pia.


Tanzania ili uweze ku sustain kwenye biashara yako basi unalazimika kukwepa kodi kama ukoma.
Ikiwa mtu analipa kodi nyingi namna hiyo. Iweje hata bango lake pia nje tu ya biashara yake alilipie?
Tanzania ukiwa mfanyabiashara unanyonywa ili ufunge biashara hasa biashara ndogondogo na za kati.

NB:
Sijasema watu wasilipe kodi ila angalia wewe mwenyewe. Ukiweza kukwepa “BIG UP” ukiwalipa SHAURI YAKO.
Mkuu,

Tatizo la kodi Haliko Tanzania tu, Ndiyo maana unaona duniani kwa sasa moja ya kesho za kibiashara zinazotrend sana ni kwenye ukwepaji wa kodi uliofanywa huko nyuma.

Shida ni kuwa tunadhani kodi ni kubwa Tanzania tu.
 
Mkuu,

Tatizo la kodi Haliko Tanzania tu, Ndiyo maana unaona duniani kwa sasa moja ya kesho za kibiashara zinazotrend sana ni kwenye ukwepaji wa kodi uliofanywa huko nyuma.

Shida ni kuwa tunadhani kodi ni kubwa Tanzania tu.
Wewe unaiona ni ndogo?
 
Wewe unaiona ni ndogo?
Ndogo au kubwa, concept ni kuwa Ukiwa Mfanyabiashara siku zote kodi Utaiona ni burden. It happens Tanzania, it happens everywhere. Ndiyo maana nimekuonesha kuwa kuna cases za tax planning za kutisha kwenye ulimwengu wa mwanza. Watu wanakuwa kubuni namna gani watakwepa kodi ama Wakilipa walipe kidogo kwa kutumia njia halali za kihasibu n.k
 
Kwangu wanataka mpaka stiker za mlangoni nilipie. Wamenipa invoice ya 600,000Tsh. Kilichopo Siwalipi nione watafanyaje.
 
Back
Top Bottom