Kama kichwa kinavyojieleza. Nimeagiza gari japan, na inatarajiwa kufika tar 7 Nov.
Document zilishafika kama week moja iliyopita nikampa agent kwa ajili ya clearing, aliniambia gharama ni laki 2 tu. Sasa analazimisha nilipe mil moja jumla na gharama zake, na mm nimemwambia siwez kumtumia pesa nitalipa mwenyewe atume invoice naona amepaniki na amesusa kazi.
Nimemwambia anipe document zangu nitafute mtu mwingne, anadai haiwezekani kwasababu tauari ameshasajili kwenye syatem labda nilipie amendment fees. Kwa wenye uzoefu nipeni way foward, Je ni kweli kwa point hii ukishasajili maombi kwenye system huwezi kubadili agent? Na je nikiamua kulipa amendment fees itakua kama sh ngap huko kwenye syatem ili niachanae nae nianze upya?
Maana ananiambia tena mara pesa za kuhonga bandarini kwa ajili ya nn?