Nimeshindwa kabisa kuacha kamari wenzangu mliwezaje?

Nimeshindwa kabisa kuacha kamari wenzangu mliwezaje?

Bet365 ni ya Denise Coates mshahara wake wa mwaka 2022 ulikuwa £213m sijui kwa madafu zitakuwa ngapi?

Mimi sijawahi kucheza kamari maisha yangu ila wenye makampuni wanawapiga haswa wachezaji na stress juu

Jaribu kumsoma huyo msichana ambae hata kuolewa bado alijilipa bonus ambayo Uingereza tulishangaa

Ukiamka usirudie tena kucheza labda ufungue yako
 
Ili uweze kuacha hakikisha umepigwa hela kubwa at once, ukikumbukuka hicho kipigo hutabet tena nakuhakikishia mkuu.
 
Nawaza kuacha ila nikikumbuka hasara nilopata hapo sielewi
Usiwaze hilo kwani siku ikipita hairudi tena
Tunaishi na kufa, furahia ulichonacho
Mimi nasafiri sana, yaani nikipata mda tu naenda kutembea duniani
Ni bora kuliko kuitupa kwenye kamari

Mwaka huu napanda meli kubwa wiki 2 nikazunguke Caribbean huko
Lakini kama hobby yako ni kamari hiyo ndio hasara sio hela bali mda wako unaupoteza
 
Kuna UPUMBAVU umewaganda watu ambao Hupenda kusema eti kuacha kamari haiwezekani. Am telling you, hizi ni kauli za kipepo. Just Fanya maamuzi ya kutoka kama ulivyofanya maamuzi ya kuingia.
Huwezi kuacha kamari kwa kupewa ushauri na wacheza kamari. Amua kuamua na uieleze kamari kuwa Leo ndio ndoa yetu imefika mwisho.
Amua, maanisha, na tafuta Jambo mbadala la kujiburudisha.
Kwanza ujue kamari sio burudan ni biashara.
Pili usilinganishe pesa ya pombe au malaya na ya kamari maana ya kamari unafukuzia kitu kikubwa mno cha faida na pombe ni unatumia mazma au kuteketeza mazma hicho ulichopata. Plus na sumu mwilini.
Ukamaria misingi yake ni tamaa ya kupata haraka!
Ndio maana wakamaria pia ni wahangaikaj sana. Roho zina ombwe kubwa na ugomvi kati ya matamanio yao vs uwezo wao.
Ukamaria wa mikeka kwa wanaojua wanachofanya na kanuni zake ni biashara kama nyingine.
Kuhusu kuacha mdau aanzie na kamari ya mechi tu.
Na hata asiende casino kujua kinachojiri.
Asijari hata connections zinazoanzia casino.
Abadiri aina ya marafiki ili kubadiri story za maisha.
Apende kupatikana nyumba za ibada (zisizo na makelele) au msikitin.
Apende kusoma vitabu vya maarifa hasa aina kadhaa za uwekezeji wa kuwa milionea.
Apende kufanya mazungumzo na watu wenye falsafa kiwango cha juu kama Dr Ellie.
Watu wa kuombea sana ni wakamaria wa casino kama huyu mdau na wakamaria wa virtual games na machine za wachina.(Anything programmed). Huko ndo utakutana na msemo wa .THE HOUSE ALWAYS WINS!
(mpaka sasa watu pekee wanaofaidika kwa mcheza kamari ni wake maana mcheza kamari hajawai kukimbizana na ratba za kuchepuka maana hawana nguv za kiume, ni jamii ya mateja. hadi wakila ndo kwa mbaaali....)
 
Ninapozungumzia kamari siyo hii mikeka ya jero. Nazungumzia spin and win, Trukey, Russian and European roulette, poker, black jack, Barrancas wheel of fortune nk, hizi unacheza na dealers yaani ni kugongwa tu.

Kuna movie zinaitwa 👉God of gamblers 1, 2 , 3 weonesha uhuni wote unaofanywa na wamiliki wa ma cassino, na uchawi pia upo.

Hizi kitu zinamaliza hela asimwambie mtu🚮😬. Naandika haya baada ya kuliwa sana siku ya leo mapemaaaa cassino.

Yaani najiona nikilala saa mbili usiku kinyonge sana😓.
Umeliwa shi ngap?
Nikurudishie hyo Pesa
 
Ili uweze kuacha hakikisha umepigwa hela kubwa at once, ukikumbukuka hicho kipigo hutabet tena nakuhakikishia mkuu.

Boss wangu alichukua sales ya siku 21M akaibukia cassino akaliwa zote, wakubwa zake wakataka kumrudisha nchini kwao
Akasamehewa akaapa ameacha, Ila hajaacha kapunguza siku hizi anaenda na 1M-2M [emoji28] akipata anareplace akikosa, inakua imeisha hivyo.
 
Bro.... mimi nimekuelewa unacho sema wengi wanaongelea mpira, ila virtuals kuziacha inakubidi uziache mara moja sababu wewe mwenyewe unazijua ni mbaya , wala si wahuni tu spin and win au rouletes wale ni wahuni. Dawa ni kuacha ghafla iyo ni turkey law rapidly cooling yaani kuacha ghafla na kutocheza tena.

Option nyingine ni pale unapokuwa maskini ndiyo unaacha maana pesa ya kucheza huna and life bits you.

Option nyingine ni majukumu ya familia, kwani wewe huna family inayokutegemea kiongozi au upo under control.
 
Boss wangu alichukua sales ya siku 21M akaibukia cassino akaliwa zote, wakubwa zake wakataka kumrudisha nchini kwao
Akasamehewa akaapa ameacha, Ila hajaacha kapunguza siku hizi anaenda na 1M-2M [emoji28] akipata anareplace akikosa, inakua imeisha hivyo.
Anacheza CASINO na ashakuwa addicted, unaweza mcheka ila ni ulevi unaotesa sana.....

Hata uwe na akili kubwaaz hili dude likikuingia damuni kama boss wako huruki.

Daah hili dude bhana ni la kimataifa.
 
Back
Top Bottom