Nimesikiliza mahojiano ya Prof. Assad na Kikeke, huyu Prof. ana ujuaji mwingi. Unafukuzaje mfanyakazi akikataa kufanya majukumu ambayo sio yake?

Walimuajiri wa nini in the first place?? Na gari wakampa.
Huelewei kwa nini watu walioajiriwa leo wanafutwa kazi hata kesho yake?? Kazi zisizo za kitaaluma kama dereva unauliza kwa nini walimuajiri in first place?? Udereva ni kazi zisizo za kitaaluma kama kibarua au saidia fundi.
 
Huelewei kwa nini watu walioajiriwa leo wanafutwa kazi hata kesho yake?? Kazi zisizo za kitaaluma kama dereva unauliza kwa nini walimuajiri in first place?? Udereva ni kazi zisizo za kitaaluma kama kibarua au saidia fundi.
Duuh mkuu unaishi dunia ipi??

Veta na NIT huko unadhani watu wanacheza rede au??
 
Duuh mkuu unaishi dunia ipi??

Veta na NIT huko unadhani watu wanacheza rede au??
Kwenda Veta au NIT hakuufanyi udereva kuwa kazi ya kitaaluma, hakuna hata degree ya udereva ila kuna degree ya mapishi inaitwa culinary arts.
 
Sijaona kosa la Prof.kumfukuza kazi huyo dereva! Kama alikuwa jobless angekuwa analipwa mshahara bure.
Hata hivyo Prof hakutumia busara kumfukuza kazi huyo!
Kwa namna ambavyo hakumhurumia huyo dereva ndiyo Magufuri hakumhurumia wakati anaachishwa u CAG!
 
Na sihitaji kupandishwa cheo kwenye kazi ya utumwa
Huwezi ukampa mtu kazi kama driver kesho ukamwambia apange mafile kesho kutwa awe Gardner baada ya hapo aandae chai kisa awe flexible kama ni hivyo wangeorodhesha kwenye job descriptions kuwa kuna kupanga mafile
 
CAG hapaswi kuondolewa kwa sababu zozote kabla hajamaliza muda wake isipokuwa za kimaadili tu tena kwa kuundiwa tume maalumu, dereva anaweza kuondolewa kama hana mtu wa kumuendesha.
 
Kupanga mafile kuna shida gani?, Mimi nimefanya kazi na madriver wenye elimu ya uhasibu 2. Siku ambayo hatuendi field walikuwa wanamsaidia mhasibu kazi za kihasibu, baada ya kuona utayari wao tuliwapandishia mishara.
 
Yaan huyo mfanyakaz akikomaa analipwa mabilioni ya pesa. Mahakama, itaangalia utaratibu kama ulifuatwa, mfano je kwenye faili la mfanyakaz kuna barua ya onyo.
Mambo sio rahisi hivyo, kama huna majukumu ya kufanya kazini unatakiwa uondolewe, huwezi kulipwa wakati huzalishi chochote.
 
Hapa tunajadili kufuata taratibu za ajira na sio utu.

Tukimaliza hilo tutakuja kwenye huo utu unaouzungumzia ambao hata huo huyo mtu wako hana.
Babako marehemu alimtishia akamwambia analindwa na nani wakati yeye ana majeshi yote ya ulinzi na usalama .hivi sasa Yuko wapi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…