Hiyo ndio sababu ya kukukataa - mali. Wamejipatia mali ya dhuruma na hawako tayari kukutambua. Hao wanaweza hata kukuua. Una haki kama mtoto wa marehemu ila wanakuchinjia baharini. Usikate tamaa mtafute mwanasheria ili uone kama haki yako inaweza kupatikana. Pole pambana usiogope.
Lukas...sijasema ujitenge namaanisha uendelee na maisha yako bila kujari kuna mtu mwingine au la...ni bahati mbaya watu hatuweki baadhi ya mikasa yetu...ninauona wako mdogo sana ukilinganisha na wa kwangu...lkn nasonga!!
By the way in short!
Baba alikuwa manager wa ttcl iringa centre kutokana na kufanya kanzi baada ya mda akastafu na kuanza kanzi binafsi, ilipofika kupatikana kwangu kwakuwa mama mkubwa alikuwa yupo naye pamoja na baba bc mama akawa yupo kijijini niliko zaliwa nikaanza shule chekechea akiwa yeye ndio axis wa waisha yangu sina pen was up to him, kitu chechote kile ninachokita nilikuwa napewa. Kupewa kwa matumizi hayo nilikuwa naenda mjini na pewa pesa kama nguo kununuliwa bc na nunuliwa. Hadi ilipo fika form form nikamaliza. Akapiga sim kuwa niende mjini anakokaa yeye ili twende tukaishi wote, bc huo mswaada ukawezekana tukawa tunakaa naye tulikaa naye kama mwenzi mmoja dada zangu wakatambulishwa pa moja na mama mkubwa, baada tu ya kutambulishwa wiki 3 mbele mzee kuumwa mpaka kufa kwake, baada ya kufa ikawa ndio ngao kuu ya kufukunzwa na kukataliwa kuwa sio mtoto wa familia mmoja .KUMBUKA KUWA NAYE MAMA ALIKUFA BAADA YA WIKI INAYOFUATA. Je im still child, im still student in diploma first as you the prices needed at unversity of medicala laboratory.
Thanks.
pamoja na hayo mkuu, jamaa anayo haki ya kisheria, kikanuni na kikatiba ya kupata urithi kutokana na mali za baba yake. kwanini wengine wapate, yeye akose? haikubaliki hata kidogo. lazima naye apate walau ekari 1 kutoka mashamba ya babaye na mgawo wa mali zingine...ni haki yake ya MSINGI.
Kwani kuna mtu kweli atamkatalia haki ya ubini?hakuna.Ila kilichopo hapa yaonekana kaenda kutaka apewe mgawo.Mkuu HAKI siyo lazima iwe mali sin maan hiyo,
Haki nayo taka aipiganie ni HAKI yA ubini.
Hizo sio zako ndugu.Wewe jenga tu undugu kama watakusaidia sawa wasipokusaidia sawa.Utatafuta namna zingine.Thanksgiving, labda nikueleze mimi nibado mwanafunzi kwa sasa nasomea maabara diploma mwaka wa kwanza kutokana na kuhangaika kulipa ada ya chuo ninatamani niombe hadi misaada wakati najua kabisa kwa nyumba za urithi kwa mwenzi si chini ya 1mill na laki kadha kwa nini nihangaike isitoshe yeye ndiye aliye nisomesha kutoka kinderndagarten hadi form 4! Je is there any right to human being mkuu?
Im african
Im human
Im child
agombee undugu kwa watu wasiomtaka ili iweje? mali ndio muhimu...naye ni mtoto halali wa marehemu na anastahili kupata urithi kama watoto wengine. acha kumtia mwenzako unyonge.
Najua huruma uliyoipata lakin umeenda mbali sana.Hiyo ndio sababu ya kukukataa - mali. Wamejipatia mali ya dhuruma na hawako tayari kukutambua. Hao wanaweza hata kukuua. Una haki kama mtoto wa marehemu ila wanakuchinjia baharini. Usikate tamaa mtafute mwanasheria ili uone kama haki yako inaweza kupatikana. Pole pambana usiogope.
Okey, but father na motherless died at the same time there is no mother mkubwa.
Thanks.
HAKI HAMNA HAPO NDUGU, zaidi atajipotezea muda tu.mkuu, kwa kuwa una picha na vyeti vya kuzaliwa, komaa mpaka upate haki yako ijapokuwa sasa suala la kupima DNA litakuwa gumu. onana na mawakili mahali ulipo wakusaidie kupata haki yako. ndugu wengine ni waroho sana...wanataka mali zote hizo wagawane wenyewe? yakhe hawana khaya! komaa sana tu mkuu mpaka kieleweke.
Kikubwa zaidi, ichukulie umri umefika wa kuoa, mke mtarajiwa anasema nami natamani kuja kwenu kwa wazazi wako, kwa mtazamo wako unafikiri nitampeleka wapi akidai twende kwa baba mzawa! Just help,
Pambana mkuu uhakikishe haki yako imepatikana. Hao wanao kuambia achana uachane na familia yako ambayo kimsingi ni muhimu kuijua
Hata kama haitakusaidia kitu.
KomAa nao kisheria.
kufahamiana kwao na mama ni kwamba kulikuwa kuna kaka wa kwanza alikufa mbaye alikuwa mkubwa kwangu ndiyo huyo wao ndio wanadai kuwa angekuwa yule wa kwanza wangekubaliana nae ila sio mimi,tatizo ndio hlo.
Kikubwa zaidi, ichukulie umri umefika wa kuoa, mke mtarajiwa anasema nami natamani kuja kwenu kwa wazazi wako, kwa mtazamo wako unafikiri nitampeleka wapi akidai twende kwa baba mzawa! Just help,
Najua huruma uliyoipata lakin umeenda mbali sana.
Hao wamepata mali ya dhuruma kivip?huyo Baba alikuwa anaishi na hiyo familia yake na mke wangu, mali ya ndoa ni ya mke na mme, sasa mme kaondoka hivyo sasa mali ni za mke au watoto wa ndoa. Na huyu wao hawamtambui, sasa wameiba vip?unamewaonea bure.
Suala hapa ni Baba ndio alichemsha, alipaswa ajue haya tatatokea hivyo kama ni kumpa angempa akiwa hai, kwa kuwa Baba yake hakumoa unataka hawa wengine wampe mtu wa nje kwa sababu gani?kwa wema gani walionao ambao Baba yake hakuwa nao?Ni sawa nawe uwe na mme, mkachuma mali kadhaa na mkazaa watoto ndani ya ndoa, zile mali mlizopata ndani ya ndoa sio za baba tu kama anavyofikiri huyu, ni mali za ndoa yaan za mme na mke wa ndoa, hivyo mtoto wa nje ya ndoa uwa hawi considered.Huyo ni wa Baba binafsi hivyo Baba kwa mali zake binafsi zisizo za ndoa angempa huyo mtoto akiwa hai au angeandika will kwa mali zake binafsi ambazo kwa maelezo yake hapo hakuna kitu kama hicho, hivyo hana namna ya kudai mali kwa sasa. Kama hao watoto wa ndoa wakitaka asipate chochote hatapata na ni haki yao, ni mali ya pamoja ya Baba na Mama yao, haajamuibia wala kumdhurumu hapo.
Ndio maana hapa aamue tu kujenga undugu, by the way kasema ana mchumba anayetaka kumuoa, hii maana yake ni mtu mzima, hakuna njia moja ya mafanikio, afungue macho njia zingine zitaonekana.
Msome vizuri, amesema amekaa hapo kwa wiki 2 tu kabla Baba hajafa, Mama yake hakuwa mke, huyo Baba alikuwa na mke wake sa ndoa, mali alichuma kwenye ndoa yake ndoa ambayo ina watoto pia.Kama umeuelewa vizuri uzi huu ni kwamba, mkataliwa alishawahi kuishi nao nyumba moja wakati baba yake akiwa hai na walitambulishwa na kuelewa hilo. Alifukuzwa/kukataliwa baada ya baba kufa. Unapaonaje hapo sio kudhurumiwa/kuibiwa haki??
Hapa ndipo umuhimu wa mke mmoja, mtoto mmoja unapokuja.
Hakuna chance ya watoto kugombea mali.