Nguvu moja
JF-Expert Member
- Oct 20, 2017
- 3,371
- 2,713
Ilikuwa nikipata pesa tu nikimaliza kutoa mahitaji madogo madogo nyumbani ikiwemo pesa za matumizi kwa mke wangu
Basi hata kama nitakuwa na laki mbili zote nitazimaliza bar kwa kujenga heshima... Kunywa na kuwanunulia jamaa na marafiki asubuhi yake sina hata sentano
Yalikuwa maisha mabaya sana kwangu mpaka roho nafsi yangu ilikuwa aiko sawa kwa uteketezaji huo wa pesa niliokuwa naufanya, lakini mwisho wa siku nikawa namuomba mwenyezi mungu aniepushie hilo janga
Hadi leo ninapoandika hii thread nina miezi minne na wiki mbili nimeacha unywaji wa pombe najiona niko mwepesi mapigo ya moyo yalikuwa kasi sana sasa moyo wangu umepoa kabisa nimeamua kuishi maisha mapya kabisa hata familia yangu nyumbani wamefurahi na kushukuru.
Shukran pekee nampelekea mwenyezi mungu kwa kunitoa juani na gizani na kunipeleka kivulini.
Nawasilisha.
Basi hata kama nitakuwa na laki mbili zote nitazimaliza bar kwa kujenga heshima... Kunywa na kuwanunulia jamaa na marafiki asubuhi yake sina hata sentano
Yalikuwa maisha mabaya sana kwangu mpaka roho nafsi yangu ilikuwa aiko sawa kwa uteketezaji huo wa pesa niliokuwa naufanya, lakini mwisho wa siku nikawa namuomba mwenyezi mungu aniepushie hilo janga
Hadi leo ninapoandika hii thread nina miezi minne na wiki mbili nimeacha unywaji wa pombe najiona niko mwepesi mapigo ya moyo yalikuwa kasi sana sasa moyo wangu umepoa kabisa nimeamua kuishi maisha mapya kabisa hata familia yangu nyumbani wamefurahi na kushukuru.
Shukran pekee nampelekea mwenyezi mungu kwa kunitoa juani na gizani na kunipeleka kivulini.
Nawasilisha.