Nimetoka ukweni Kigoma, ila kama hii ndiyo aina ya wazee acha wabaki na watoto wao!

Kama unampenda Mkeo kaa nae, wazee watakufa, watapotea mwanao atabaki. Huwezi kuumiza mwanao na mkeo anayekupenda kwa dhati kwasababu ya wazazi wake. Wewe umetimiza wajibu wako, umewaheshimu, na mengine muache Mungu afanye kazi yake. Piga mimba nyingine wawe watoto wawili, somesha tunza mkeo halafu omba Mungu. Chuki zao Zina mwisho
 
Mkuu kwenda na bro wa 50s of age awe mhuni?
Achilia mbali hilo, mshenga tumemuomba mwenyeji wa huko huko, ili tusiharibu!
Lakini zaidi sana, kwa sisi tu nauli imekata zaidi ya 600k, tungeongezeka 2 tu (yaani shangazi na mjomba) kama unavyosema, nauli ingekuwa 1.2M

Kwa hali ya uchumi wangu na mazingira yalivyo walipaswa kuizingatia zaidi dhamira yangu kwao kuliko kuangalia makosa yangu na binti yao, (kwani makosa tulifanya wote)

Hizi tabia za kukandamiza vijana wenye nia nzuri na kuwanyanyasa ndo kunafanya wengine wakimbie kuanzia mimba, mpaka wapenzi wenyewe, na kuongeza idadi ya watoto wanaokosa malezi ya pande mbili.

Kwa mfano mimi nikiwa na roho ndogo, nikaamua kutokwenda tena na kuachana na mtoto wao, mwanangu atateseka mno, lakini pia mtoto wao atateseka pia kwa sababu ambazo hazina ulazima kabisa!

Kunitukana, kunidhalilisha kwa sababu ya eti nilizaa na mtoto wao inawaongezea nini? Inafuta makosa yetu? Kwa kunidhalilisha inafanya binti yao arejee kuwa bikra? (Obvious jibu ni hapana)

Acha hayo matusi na kunidhalilisha, wanapotaja mahari ya kunikomoa (ambayo mimi sina) wanataka nishindwe kulipa then niwaachie binti yao, wakibaki na binti yao wananufaikaje naye? wanaona bora waendelee kulea mtoto na mjukuu wao kwa kuwa tu, tulikosea? Yaani kila nikitafakari sipati majibu kabisa
 
Mkuu maisha yamebadilika, basi azalishwe huyo mtoto wako ubaki nae hapo nyumbani.

Maswala ya watu kwenda kujionesha Huwa yanachangiwa na sababu nyingi Uchumi ukiwa Moja ya sababu.
Kabisa aisee, yaani kwa uchumi huu nichukue baba, mama, shangazi, mjomba, mshenga , dada ,sijui mshenga na kaka, tunaenda kujitambulisha na kulipa mahari?
Hapo maana yake ingekuwa 8×300k = 2.4M nauli peke yake, haiwezekani! (Hapo ukijumlisha na mahari waliyoitaja ingekuwa 2.4M + 4M = 6.4M yaani)
 
Safe place ipi ikiwa wazazi watakana kutambua hiyo ndoa?

Wale huwa wanasubiri mtoto wao afariki ili wakatae kupokea mwili na kudai uwarudishie mtoto wao akiwa hai kama ulivyomchukua

Kigoma ni hatari, narudi tena ni hatari
Naogopa wasije wakamuua kweli ili tu wanikomoe, hawashindwi binadamu hawa!
 
Kosa la huyo binti uliyemzalisha na unataka kumuacha ni lipi??

Mbona vijana hamuishiwi sababu za kuongeza singo maza mtaani??

Umemchakaza binti mpaka umemzalisha halafu unamuacha kisa baba yake aisee, unamuoa binti au baba yake.

Umtie mimba binti akiwa kwao bila ndoa halafu baba afurahie kisa umekuja na mkaja wa mama na mbuzi watatu??

Acha dharau kijana, hata mimi babu yangu angekutoa baru, eti unampangia mahari aiseee.

Ukimuacha binti nae kwa hasira akakumwagia tindikali mtaanza lawama za kusema wanawake wana roho mbaya.
 
Nakuelewa mdogo angu. Hawaja kufanyia fair kabisaaa nakubaliana na wewe na uzur hata huyo mshenga alikua na wisdom sana .Ila sasa ambacho mimi nimejaribu ku focus ni kwenye tamaduni zetu kiafrika.Na hiki ndio sabab kwel vijana wengi hukacha kuoa kwakua customs and tabboos zetu haziko friendly
 
Milioni 4 kitu gani ww toa nusu oa iyo nyengine utamalizia mbele kwa mbele kikubwa muoe usisitishe mapenzi kwa mtu unae mpenda unajua inachukua years kumpata mtu umpendaye na akakushiba pia sasa mkuu unataka nini shinda hiyo vita mkuu mbona ndogo sana ungeambiwa ng'ombe 20 ungejisikiaje.

Alafu hata mm ningekuwa mzee ningemind vilevile unamtiaje mtoto wangu mimba than unamzalisha kifala bila kuja kujitambulisha nakufata taratibu zote.
 
Sasa unaponitimua kwako naishije na binti yako?
Mahari no formality ya kimila kuunganisha koo na kubariki watoto wanapokwenda kuanza maisha yao, mahari sio biashara ya kujipatia kipato, badili hiyo mindset, otherwise utajikuta unalea watoto wako, wanazalishwa na unaanza kulea na watoto wa watoto wako!
 
Wazee wetu tunapaswa kuwashauri saba kwenye maeneo haya, angalau watambue kwamba vijana wao kwa nyakati hizi tuna changamoto nyingi mno linapokuja swala la kutengeneza familia,watuvumilie kwa madhaifu yetu na watutie moyo tunapofanya maamuzi yenye kujenga!

Kutudhalilisha na kutukandamiza namna hii kunafanya tujione wajinga kwenda ukweni, na kudhani kuwa ujanja ni kukimbia unapotia mimba mtoto wa mtu, kitu ambacho sio kizuri kabisa!
 
Mzee wa watu hana makosa, wewe ndiye umepuyanga kwa kudhani kuwa unawamudu kwa kukaa na binti yao kumzalisha kisha kwenda kwao kwa kiburi. Unaenda kulipa mahari na bro? Huna wazee wala shangazi? Trna huyo mzee umemfanyia dharau sana.

Halafu kwani hujui mahari za waha? Mimi nilimzalisha binti wa kiha ingawa nilikuwa kwenye process. Nakumbuka nilienda kulipa mahari nikiwa tayari nina details zote kutoka kwa wazee wake na ndugu. Nilipeleka 3M casha ikijumuisha vikorombwezo vyote. Waha ukienda kulipa mahari kwao hadi bajeti ya vyakula watakavyokula ni juu yako.

Ila nashukuru binti yao ni mzuri sana, mtamu sana figa lake sasa na uzuri ana nidhamu sana. Nimekaa naye muda wa kutosha kabla sijaamua jumla na hajawahi kuonyesha dharau kwangu.

Nenda kakamilishe uliyoagizwa kwa dharau ulizoonyesha ama uanze kupata mikosi na kama huwajui waha basi nenda kigoma uone mtu anatumiwa radi inamfuata hata akiwa chini ya meza.
 
Pole mkuu. Lakini hiyo mahari nadhani ni reasonable hasa ukizingatia ulimzalisha mtoto wao na ulichelewa kwenda kujitambulisha! Mimi sijamzalisha wa kwangu lakini nimepigwa mahari 3.8 M na wanyakyusa wa Simike wale!
Umeokotwa tu nawewe
 
Sema nini, usimuache huyo manzi.Usimuache kwa shida hiyo labda kama zipo au zitajitokeza zingine..Ila kwahilo hana kosa na hakupenda kilichotokea ndio maana akaamua kuondoka.Pia kitendo cha mama mkwe pia kujua walikukosea ni ishara tosha kuwa hata dingi ujumbe huo ataupata na atajua kuwa alizingua. Endelea na kuwa nae.
Ila sasa piga kama 10 years hiv usikanyage ukwen.Kwa heri au kwa shari.

Wao kama watataka kuja sawaa
 
Jf bhana...
 
Acha ukoloni mzee wangu.

Dunia imebadilika.
 
Mahari haina kiwango maalum kila koo na familia hujipangia.
Kwa story yako hakuna mahali baba wa binti kakufukuza ni wewe na hasira zako, ulitegemea upokelewe kama mfalme wakati umeidharau familia ya ukweni.

Na hapo humkomoi baba mkwe ila unamkomoa huyo mwanamke maana inaonekana hapendi kuishi kijijini, aking'ang'ania kuishi mjini ni mateso kwake kama alikua anakutegemea wewe kwa kila kitu.

Acha kukimbia majukumu lea familia yako, unaacha kuwaza maridhiano unaleta hasira na wewe. Yani huyo mkwe wako na wewe ni sawasawa kabisa hamna tofauti.
 
Acha ukoloni mzee wangu.

Dunia imebadilika.
Nani kakwambia dunia imebadilika dunia iko vilevile na ardhi ndo ileile na majira ni yaleyale kuna asubuhi, mchana, jioni na usiku na hewa tunayoivuta ni ileile na mvua ndo zilezile yaani mm ungemtia mimba mwanangu umemzini, umemzalisha alafu unaleta story za dunia kubadilika nakukodia mabaunsa wakunyandue bila mafuta acheni kuharibu watoto fateni taratibu muoe.
 
Tusitishane bhana, kama wanaona watoto wao ni mitaji acha tuwaachie tu! Siwezi kulipa 4M mimi, siwezi n'a hiyo pesa sina!

Lakini unaponiambia nisafirishe shangazi, mjomba sijui na watu gani, kutoka Dar mpaka Kigoma ili kuonyesha kuwa sina dharau nao ni uvivu wa kufikiria, hivi kweli unapima heshima yangu kwa kuwaleta shangazi zangu kutoa mahari ?
Na unapotoa mawazo yako jaribu kufikiria, kwamba Kigoma sio Buguruni wala sio Kimara mwisho!
 
Mimi sikuhitaji kupokelewa kifalme mkuu, nilienda nikiwa najua kuna mahali tulikosea, lakini siwezi kukubali kulipa mahari ya kunikomoa, ukichanganya na maneno ya dharau na kunidhalilisha, kwa kufanya hivyo inawanufaisha nini?

Nilibeba zawadi za wazee nikijua ni kama ambavyo ningewabebea wazee wangu tu, wanaishia kuniambia "nilikutuma uniletee vizawadi vyako?" mbele za watu?

Halafu unataka kuniambia nione ni kawaida?

Huyu mzee siku akija kwangu, sitamfukuza, nitampa kila anachotaka ila nitahama nyumbani kwangu mpaka siku ameondoka ndo nitarudi!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…