Nimetoka ukweni Kigoma, ila kama hii ndiyo aina ya wazee acha wabaki na watoto wao!

Mfano wewe mtoto wako azalishwe bila ndoa itafurahia ? Na aje kuishi na mwanaume bila kumjua na aje kwako kujitambulisha na vizawadi vya kuwadanganya kama watoto au familia yenye dhiki sana.
Yule mzee yuko sahihi umekaa na binti yao kiunyumba mda wote huo na wanajua alafu unaenda unategemewa upokelewe vizuri si ujinga huo
 
Ka
kabla sijamalizia kusoma hili gazeti, hapo mwanzo pamenichekesha kwamba “ mapenzi yana nguvu bro, sijawahi kuwaza kutembea umbali mrefu kufata mwanamke” ( a.k.a mbususu)🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣
 
Masikini
 
Learn from experience ya baba yangu mdogo. Yeye alipomaliza chuo Mlimani miaka ya 90 mwishoni alikuwa na mchumba wake waliodumu nae kwa miaka mingi sana na akamtoa mimba nyingi sana katika kipindi cha uchumba wao. Alipeleka mpaka barua ya posa Kigoma huko halafu mwisho wa siku akaja kumuacha huyo mchumba wake kimyakimya na kumtelekeza kwao huko Kigoma huku akimuachia dada wa watu matumaini kuwa atarudi kuja kumalizia michakato amuoe.

Hellooo alikuja kuoa mwanamke mwingine, halafu nyumbani kwa mchumba wa zamani wakapata taarifa. Mama wa mchumba alikujaga kumtafuta mshua mdogo akamwambia kuwa kwa kuwa alimchezea mtoto wao na pia akawadanganya na wao basi alichoona kuwa binti yao hawezi kumpa atakipata mwanaume mwingine atayemuoa ila na yeye hawezi kukipata kwa aliyemuoa.

Huwezi amini hofu ya mshua mdogo ilikuwa ni kwenye maswala ya uzazi kwa sababu ya mimba alizomtoa yule mchumba wake na kilichompata mke mpya ni kuwa hakuwahi kupata mimba mpaka sasa ameshafika menopause. Walishafanyiwa kila kipimo unachokijua wewe hakuna yeyote kati yao alionekana kuwa na tatizo lolote. Wameenda mpaka South kupandikiza mimba lakini wapi, mimba iligoma kukaa.

Nakwambia ukimuacha huyo mwanamke kwa hizo sababu basi hutakaa ufurahi kwenye hiyo ndoa mpya utakayoingia kwa jinsi Waha walivyo na visasi baba.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huwezi kuelewa kikamilifu kwa kuwa hujui kitu,ukikua utaelewa...
 
Huwezi kuelewa kikamilifu kwa kuwa hujui kitu,ukikua utaelewa...
Mim au wewe
Unaenda ukweni hujui hata jinsi ya kuandika barua ya posa unajifananisha na mim yaan unaenda kutoa posa bila hata kuwa na mtu wa makamu kutoka kwenu serious
Unachimbwa mkwara na baba mkwe alafu unaufyata a.k.a kuzira wewe ni mvulana na sio mwanaume
 
Mengine namuachia Mungu,mimi sikuwahi kuwa na roho mbaya, wala nia haikuwahi kuwa ovu dhidi yao, kama wamefanya kunikomoa ili waje waniroge kwa kushindwa kufikia matakwa yao basi na waroge tu!
 
Naamini haujasoma nilichoandika, kama umesoma una kichwa kigumu, haujaelewa, soma tena!
 
Huyo mkeo Kama anaona ulichofanyiwa sio fair siku awapigie simu awaambie huku ndoa imeshindikana mwenzangu kaniambia hataweza kumudu mahari iliyopangwa hivyo tuachane yeye atahudumia tu mtoto hivyo muda wowote narudi kuja kukaa kijijini uone Kama mzee akili haijamkaa sawa
 
Ushauri wa vijana wa sasa hivi ni waajabu sana kwenye maisha mda mwingine hakuna jambo rahisi kama mwanaume lazima uwe mpambanaji sio unakubali kirahis rahisi
Kama ukiwa mwoga mwoga unaweza ipigania familia
 
Ushauri wa vijana wa sasa hivi ni waajabu sana kwenye maisha mda mwingine hakuna jambo rahisi kama mwanaume lazima uwe mpambanaji sio unakubali kirahis rahisi
Kama ukiwa mwoga mwoga unaweza ipigania familia
Sio kila kitu Ni Cha kufuata kisa ni Cha zamani Kuna sababu gani ya kuozesha mwanao Kama unamuuza ,kwani lazima baba uwe mafia?tuache vingine vipite na wakati kikubwa tuwaombee watoto waishi kwa amani milioni 4 mahari ya mtu mmoja sio fair
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…