Nimetoka ukweni Kigoma, ila kama hii ndiyo aina ya wazee acha wabaki na watoto wao!

Hivi vitisho vya kipuuzi sana, sasa wamuue mtoto kwa sababu ya wao kutaka pesa nyingi?
Kwani kuoana ni miradi mpaka ihusishe mauaji?
Kama ndivyo walivyo inaniongezea sababu ya kuwakataa tena na kutojenga undugu na watu wa aina hii!
Mkuu kule sio pa kujenga mazoea, ndio maana ndugu zako wakakwambia kabisa. Shikilia msimamo wako, hakuna atakaeishi milele. Bora kufa kuliko kujenga mahusiano na muha
 
TheMnyonge pole sana,naamini una nia nzuri ila methodology unayotumia ndo haijazaa matunda.
Pia kuna tatizo nailiona kwako,umeleta mada,acha watu wakushauri,lkn naona unabishana nao,ni kama una maamuzi yako tayari,sasa kwa nn umeileta hapa?
 
HIYO NI BUHIGWE MOJA

Yes juzi nilienda huko ni mbali Heru ushingo nikatokea huru juu aiseeh acha tu jamani hili nchi ni jitu kuuubwa sana Buhigwe ndo kwao mpango wameanza kumtengenezea barabara

Yote kwa yote ba mkwe ni \|*}%{
Maisha ya kule ni magumu kuliko jiwe ni halali binti akulilie usimuache kule hamna
 
Kama mama mkwe hana shida na mke hana shida basi achana na huyo dingi. Ni stress tu za maisha.

Tunza familia yako achana na huyo dingi.

Ma mkwe keshachukua chake shida aitoe wapi tena?

Dingi anataka kwenye mahari awanange majirani na wazee wenzie sasa matarajio wamekuwa tofauti ko lazima ajae sumu
 
Aiseeh watu hawana Shukrani yaani umeamua ujulikane na zawadi umewapelekea bado dingi anadai nani alikutuma zawadi?

Upo sahihi kujaa gas mkuu na tena kaa na binti yao hadi wao watakapoomba po!

Kikubwa ushawajua hayo mengine kwa baadae waambie mambo yamekuwa magum hata ile mahari nilokupa ukaikataa muda ule kwa sasa sina hadi yeye akuombe samahani kwa kukukwaza ugenini!
 
Vijana wanaolelewa hovyo kimjinimjini ndiyo shida.Huku kwetu mikoani watu tupo kitamaduni zaidi,ukija njoo kwa nidhamu ya juu sana.
 
Hivi vitisho vya kipuuzi sana, sasa wamuue mtoto kwa sababu ya wao kutaka pesa nyingi?
Kwani kuoana ni miradi mpaka ihusishe mauaji?
Kama ndivyo walivyo inaniongezea sababu ya kuwakataa tena na kutojenga undugu na watu wa aina hii!
Linda familia yako kijana, wewe hutakua na undugu na hao watu upande wa kikeni.

Hata mwanao ndgu zake ni wa kiumeni si kikeni ndio maana anaitwa jina lako.
 
TheMnyonge pole sana,naamini una nia nzuri ila methodology unayotumia ndo haijazaa matunda.
Pia kuna tatizo nailiona kwako,umeleta mada,acha watu wakushauri,lkn naona unabishana nao,ni kama una maamuzi yako tayari,sasa kwa nn umeileta hapa?
Nimekupata, japo nashangazwa na baadhi ya watu wanaosema sijui ningewabeba wazazi wangu na blah blah kibao!

Nimeeleza kwa kina nilimchukua Kaka yangu mkubwa (over years) kutoka Dar mpaka Kigoma, then kwa kujua kwamba kule ni ugenini, hatujui taratibu zao, tukamuomba mzee mwenyeji wa huko ili atusaidie ku-cope na mila na desturi zao, lakini yakatokea yaliyotokea pasipokujali dhamira ya sisi kufika pale!

Sijaleta mada ili watu waniamulie cha kufanya, isipokuwa nimetoa hiyo experience walau tunapozeeka tusifanye upuuzi wa namna hii, mahari si kitu cha kukomoana, kujenga undugu na linapaswa kuwa jambo la heri, sio shari!
 
Pole hapo atakayeteseka ni mtoto wako tuu huyo pole
 
Sijaona shida ya Baba mkwe hapo.
Nimekuona wewe tuu sasa hasira zimetoka wapi, unavyoonekana wewe ni mtu mwenye hasira sana.
 
mama firstborn

Daa kuna rafiki yangu mmoja wa kiume alinisimulia kuhusu hiyo.
Yeye Baba yake na mama yake walimzaa nje , baadae baba akaoa huko na mama akaolewa huko.

Daaa aliniambia jinsi alivyoishi alipata shida sana upande wa saikologia,
Akienda kwa Baba anamkuta Baba yupo na mkewe na watoto wake, mbaya zaidi watoto wake wamefanana kinoma,
Akienda kwa mama yake anamkuta mama yupo na mume mwingine na watoto wao.
Yeye yupo kati , aliniambia kuwa hawajawahi kumtesa hata kidogo ila situation kama hio daa ailimuaribu kisaikolojia kabisa,
Aliniambia tuj usijaribu kuzaa nje bro mwenye kuathirika ni mtoto sio nyie wazazi. Aliniambia yeye amepata huo uzoefu hatakuja kufanya hivyo hata siku moja, ikitokea anamuoa huyo huyo kwa gharama yoyote ile.
Ila alinkambia ata akija kuoa akichepuka condom ni lazima atumie ili asitengeneze mtoto nje.
Yeye akabaki kwenda kwa shangazi yake, na aunt yake akuwa na mume, alikuwa na mtoto mmoja wa kike tuu( single mother),
Ndo akawaanashida huko.

TheMnyonge
Pole sana , hapo mtoto wako ndo wakuteseka hujui mke utakaye muoa atakuwaje bro.
Pole sana .
 
Kamanda umenena vyema. Bila shaka unajua kitu cha kufanya baada ya hilo sekeseke ili kuendelea kulinda familia na mapenzi yako kwa binti.
Fanya hivyo kaka...don't lose hope. Kumbuka your present situation is not your final destination.
 
Mfano wewe mtoto wako azalishwe bila ndoa itafurahia ? Na aje kuishi na mwanaume bila kumjua na aje kwako kujitambulisha na vizawadi vya kuwadanganya kama watoto au familia yenye dhiki sana.
Daaaaa
 
Ninavyojua mimi TheMnyonge
Ukitanguliza mtu kwanza na kishika uchumba na barua ya kuomba radhi ya kumzalisha binti yao na kuishi nae.
Mambo mengine baadae.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…