Nimetoka ukweni Kigoma, ila kama hii ndiyo aina ya wazee acha wabaki na watoto wao!

Mwamba maamuzi ni yako. Ingekua mm ningemwachia akae na binti yake na amlee mjukuu. Na hawatokuja kuniona kigoma wala kujua naishi wapi.
 
Ni muha kabisa mkuu
Ok. Nimekupata kama ni muha OG basi ongea na binti yy ndo atawatuliza wazazi wake mahari itapunguzwa. Binti wa kiha aliyepokea maadili ya Kiha asee bro umepata pipa na mfuniko wake. Nasema nikiwa na ushahidi hai. Binti wa kiha hata usafiri uende sehemu miaka 10 ukirudi utamkuta. Hata mgombane vipi upige vipi hawezi kukuacha kama kakukubali mtu wangu
 
Sijajua wewe kabila gani yani umuharibi maisha binti yangu uishi naye kama mke bila baraka ya wazazi kisha umzalishe aje nyumbani kwangu kila uje na zawadi za danganya toto.
Kaka mimi ni mtu wa nyanda za juu kusini, alichofanya jamaa hakwenda mikono mitupu, alibeba kiasi

Jamaa milioni 4 sio mchezo, bora hata huyo dingi angepokea hiyo moja, mahari italipwa kidogo kidogo mbeleni huko

Au ndo ile ukiona mkwe unataka upate hela ya solar, upige plaster nyumba yako, mara ununue ng'ombe

Kaka tuache kufanya binti zetu mitaji kama huyo mzee wa kiha
 
Kigoma !? Sijawahi sikia washkaji zangu wakitaja mahali walizolipa below 2.5m mkuu.
Jipange umtumie angalau nusu ya mahali. Vita bado hujaianzisha ila ukiendelea kuishi na huyo mkeo bila mahali utakuja kujuta kwa watu type ya mkweo toka huko kgm
Hili suala la mahari ni umaskini tu mm mwanangu sitataka mahali kikubwa waishi kwa amani na upendo tu basi tena nawapa makataba kabisa kua mm fulani bin fulani naozesha mtoto wangu bila mahari ninachotaka muishi kwa amani na upendo ikitokea mmeshindwa kuishi pamoja namchukua mwanangu bila masharti yoyte
 
Mkuu

ACHA utoto!wewe ni mshindi!

Umeushinda moyo wa Binti siyo mzee!!

Wewe chukua huyo Binti hyo hela mwambie mzee UTAKUA unamlipa kidogo kidogo kwani kwa SASA halinya uchumi haijakaa SAWA!!

Anza kutuma laki tano kwenye simu yake ,baadae laki tatu,mwakani laki tano halafu ikifika nusu ya mahari sitisha zoezi la kulipa!!!

Kwanini nakuambia mkuu!!?


Kwasasa no ngumu sana kumpata Binti ambae yupo commited kwako kiasi hicho!!!

Unaweza pata mwingine lakini aka a loyal kwao kuliko kwako na UKIPATA wa hivyo imekula KWAKO!

Mwanamme aliefanikiwa kumfanya Binti asiwe msikivu kwao no mshindi sana KWA DUNIA ya leo!!!

Chukua hiyo itakusaidia!!

Nina experience na hiyo personal!sema alikuja change baadae alipooma mambo yamekaa SAWA!
 
Kamzalisha mtoto wawatu akaishia naye bila wazazi kuruhusu, anataka wazazi wa mwanamke wafurahie vijizawadi vyake.
Kamzalisha kvip kwani huyo mwanamke alilazimishwa kuzalishwa si alikubali kwa ridhaa yake na ni mtu mzima anajua hili ni kosa na hili si kosa
 
Nimeshuhudia jamaa ametoa mahari ng'ombe 20, lakini hesabu aliyopewa ni kila ng'ombe mmoja sh.50,000/=
kwa nini vijana mnataka mahari ichezee 1m,yani mnafanya kila namna 1m ipite kama bei elekezi
 
Dah, unaroho ngumu sana mkuu
 
As for me,ninachoweza kusema huyo mzee alichokosea ni alipolalamika kutotumiwa hela na mkwewe but mengine kama mzazi ana haki ku-react maana kwanza umekaa na mtoto wao bila taarifa pili ukamzalisha tatu umetokea msiba umeshindwa kuhudhuria bila kutoa sababu za kueleweka na hata ulipopata nafasi ulishindwa kuitumia na nashangaa huyu mzee mshenga uliyeenda nae alishindwa nini kukushauri ktk hili?ilibidi kabla ya yote uombe msamaha kwa yote hayo kisha kikao kiendelee.

Hilo ulipaswa wewe mwenyewe usimame uombe msamaha au kaka yako mtoe udhuru maana maisha yana dharura kisha utoe hizo faini zao,baada ya hapo suala la mahari Tsh 4mill lingezungumzika vizuri maana uungwana wako umeshaonekana na ingepungua tu mbona mfano mimi niliambiwa mahari mill3 nikalia nao ikafika 800K nikalipa 400K mpaka leo mwaka wa kumi amani tu maisha yanaenda.

Sijaona bado sababu za kumuacha huyo mwanamke kama ni hizo ulizoandika hapo juu,kama yupo bora angle zote heshima nidhamu ya maisha etc wewe jishushe tengeneza future yako na watoto wako rudi Kigoma ukweni mtafute yule mzee uliyeenda nae mwanzo aongeze wenzake watatu wawe kamati wakamshushe pressure mzee mwenzao maisha yaende,ukisema una hasira hizo hasira hazikusaidii maisha ni kusikilizana.

Nimeona umesema mshenga alikutisha watamuuwa mtoto wakihisi hutorudi hilo linaweza lisitokee ila ukimuacha huyo mama wa mtoto wakati umekiri mwenyewe hana shida yoyote ukaowa mwengine kwa kilio chake na lawama atakazokupa utakutana na wakwe smoothly lakini mtoto wao ambaye ndiyo mkeo atakuwa bomu.
 
Huo ndiyo umasikini wa kufikiria, "kusomesha ili waje watusaidie baadaye"

Kwani sisi wengine tulisomeshwa kwa mawe? Mbona watu mnakuwa nafikra finyu hivi?
 
mzee pia atakua na zile itikadi za kwamba jamaa ana hela[emoji23][emoji23][emoji23] we kutoka dar hadi kigoma ndani ndani huko sio poa[emoji119][emoji119]
Mzee kazingua sana ila jamaa alifanya vyema kutuliza hasira
 
Mkuu ukubwa dawa jifunze kusamehe maisha yaendelee,sababu yule ni babu wa mtoto wako......
 
Kwanz Pole sana kwa yaliyokukuta mmi yaliwahi nitokea ila yako kiboko ....ushauri wangu wale ni wazee wana mapungufu yao kwa mawazo yangu wew jishushe jaribu kuzungumza nao Wenda hata wao kule wana jutia wakati mwingine hasira ni hasara ...... japo ni kweli wamekosea ..... fanya ivi kwa amani ya moyowako maisha mengine yaendelee
 
Appreciated!
 
Kwao ni sawa tu ndiyo maana hawaja kushobokea, watalea mjukuu wao maisha yataendelea.
Halafu hasara inakuwa kwa nani?
Halafu "kushobokea" unamaanisha nini, mbona naona ni negativity na ushamba tu!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…