Nimetuma fedha kwenda benki ya Tanzania na zimepotea!

Nimetuma fedha kwenda benki ya Tanzania na zimepotea!

Richard

JF-Expert Member
Joined
Oct 23, 2006
Posts
15,692
Reaction score
23,038
Kama ilivyo kwa raia wengi wa Tanzania ambao hubahatika kwenda ng'ambo, mimi pia nilipata bahati hiyo kwenye miaka ya tisini.

Nimeishi miaka mingi ughaibuni kiasi cha kuwa mwenyeji kabisa na nikiwa naishi na kufanya kazi.

Lakini kama ilivyo tabia yetu sisi waafrika huwa hatupendi kusahau nyumbani kwetu tutokako kwa kuhakikisha ndugu zetu wanapata angalau pesa ya mkate au hata soda.

Sasa hivi karibuni niliamua kuanza kutuma pesa nyumbani Tanzania kwa kutumia mtandao wangu wa benki moja kubwa tu na maarufu ughaibuni(jina nalihifadhi kwa sasa) kwenda kwenye akaunti ya ndugu yangu mmoja Tanzania katika moja ya benki maarufu pale Dar-es-Salaaam (jina nalihifadhi kwa sasa).

Lakini kwa kuwa ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kufanya hiyo transaction, nikajaribu kutuma fedha kiasi tu kama paundi 60 ambayo inatoa fedha ya madafu kama tshs 150,000 hivi.

Benki yangu ya ughaibuni wakathibitisha kwamba pesa imekwenda kwa kutumia details zote za Account name,Account number SWIFT CODE NA BIC CODE au Bank Identifier Code na IBAN.

Lakini yule ndugu yangu alipokwenda pale ofisi za benki hiyo zilizopo barabara ya Samora akaambiwa kwamba hakukuwa na ingizo la fedha yoyote kwenye akaunti yake kutoka Ughaibuni na hakuna kitu cha namna hiyo.

Mimi mwenyewe nikajaribu kuwatatuta watu wa benki hiyo pale Dar na majibu yao yalikuwa ni yake yale kwamba hakuna ingizo, pamoja na kuwapatia details zote za jinsi transfer ilivyofanywa na kwamba kwa huku kila kitu kilikuwa kimefanywa kwa asilimia 100.

Sasa najaribu kutafuta sababu za fedha kutoingizwa kwenye hiyo akaunti na utata huu kuhusiana na jambo hili ukiwemo ushauri wa watu wanaofanya kazi benki hasa wataalam wa international clearance.

Nina imani na vyombo vyetu vya fedha Tanzania isipokuwa naomba kuwa clear na hii kitu maana haieleweki kabisa.

Naombeni ushauri wenu, ahsante.
 
toka miaka ya tisin leo ndo unawakmbka ndugu zako tna kwa kuwatmia 150,000. Siku nyngne utmiage WU au money gram wafanyakaz wa benki za kibongo cku izi n wadokoz sana watakuwa wamedokoa na kuclear kabsa na history ya transaction.
 
Ni muda gani tangu umetuma manake it sometimes takes time, kwa international inter-bank transactions, 14 days zaweza kupita kabla muamala haujakamilishwa. so unapaswa kuliangalia hilo!
 
Umeshapita muda gani tokea utume?

Mimi huwa naona ni vyema zaidi kama unataka kutuma pesa basi uzitume kwa kutumia mojawapo money transfer companies kuliko bank to bank wire transfers.
 
Ni miezi zaidi ya mitatu imepita na nimepanga kuonana na watu wa benki hiyo hivi karibuni.
 
Umeshapita muda gani tokea utume?

Mimi huwa naona ni vyema zaidi kama unataka kutuma pesa basi uzitume kwa kutumia mojawapo money transfer companies kuliko bank to bank wire transfers.

Ni kweli unavyosema na nimekuwa natumia huduma zote hizo ulizosema.

Nilitaka tu kuona kwamba bank to bank transfer inakuwaje.

Niliwahi kumtumia jamaa yangu afanyae kazi Uchina kwa kutumia benki hii hii ya kwangu na akawa amepoata ndani ya wiki moja.
 
Ni miezi zaidi ya mitatu imepita na nimepanga kuonana na watu wa benki hiyo hivi karibuni.

nimefanya kazi kwenye kitengo kinachohusika na international Transfers kwa miaka mitano

1. unahitaji kuongea na benki yako, hiyo ya huko nje, ndio wanaweza kukusaidia kwa urahisi, na sio hii ya Dar, pesa hupita benki kadhaa kabla haijafika final destinatination

2. weka hapa swift copy, unaweza kuta msg yenyewe ime-NAK

3.sioni uwezekano wa afisa wa benki kuiba pesa kutoka System ya swift kwa namba hii, pesa lazima ipo
 
Nenda katika bank uliyotuma huko ughaibuni waombe wakupe swift copy ambayo inaonyesha pesa ilipotoka, chanel ilipopitia hadi ilipoishia.
TT huwa zinazingua sana huenda ime'bounce somewhere. Good news ni kwamba ni very easy ku'trace.
Otherwise nina mashaka na huyo ndugu yako uliyemtumia pengine ameshaipata ila analeta sanaa za kibongo bongo.
 
Nenda katika bank uliyotuma huko ughaibuni waombe wakupe swift copy ambayo inaonyesha pesa ilipotoka, chanel ilipopitia hadi ilipoishia.
TT huwa zinazingua sana huenda ime'bounce somewhere. Good news ni kwamba ni very easy ku'trace.
Otherwise nina mashaka na huyo ndugu yako uliyemtumia pengine ameshaipata ila analeta sanaa za kibongo bongo.

Lol

Huyu hana tabu amefaidi sana pesa yangu lakini ana ubinadamu sana ni kijana mwenye nidhamu.
 
Kama ilivyo kwa raia wengi wa Tanzania ambao hubahatika kwenda ng'ambo, mimi pia nilipata bahati hiyo kwenye miaka ya tisini.

Nimeishi miaka mingi ughaibuni kiasi cha kuwa mwenyeji kabisa na nikiwa naishi na kufanya kazi.

Lakini kama ilivyo tabia yetu sisi waafrika huwa hatupendi kusahau nyumbani kwetu tutokako kwa kuhakikisha ndugu zetu wanapata angalau pesa ya mkate au hata soda.

Sasa hivi karibuni niliamua kuanza kutuma pesa nyumbani Tanzania kwa kutumia mtandao wangu wa benki moja kubwa tu na maarufu ughaibuni(jina nalihifadhi kwa sasa) kwenda kwenye akaunti ya ndugu yangu mmoja Tanzania katika moja ya benki maarufu pale Dar-es-Salaaam (jina nalihifadhi kwa sasa).

Lakini kwa kuwa ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kufanya hiyo transaction, nikajaribu kutuma fedha kiasi tu kama paundi 60 ambayo inatoa fedha ya madafu kama tshs 150,000 hivi.

Benki yangu ya ughaibuni wakathibitisha kwamba pesa imekwenda kwa kutumia details zote za Account name,Account number SWIFT CODE NA BIC CODE au Bank Identifier Code na IBAN.

Lakini yule ndugu yangu alipokwenda pale ofisi za benki hiyo zilizopo barabara ya Samora akaambiwa kwamba hakukuwa na ingizo la fedha yoyote kwenye akaunti yake kutoka Ughaibuni na hakuna kitu cha namna hiyo.

Mimi mwenyewe nikajaribu kuwatatuta watu wa benki hiyo pale Dar na majibu yao yalikuwa ni yake yale kwamba hakuna ingizo, pamoja na kuwapatia details zote za jinsi transfer ilivyofanywa na kwamba kwa huku kila kitu kilikuwa kimefanywa kwa asilimia 100.

Sasa najaribu kutafuta sababu za fedha kutoingizwa kwenye hiyo akaunti na utata huu kuhusiana na jambo hili ukiwemo ushauri wa watu wanaofanya kazi benki hasa wataalam wa international clearance.

Nina imani na vyombo vyetu vya fedha Tanzania isipokuwa naomba kuwa clear na hii kitu maana haieleweki kabisa.

Naombeni ushauri wenu, ahsante.

Pesa za Telegraphic Transfer kuja/kutoka kwetu Tanzania kwa bank zote zinapitia kwa intemidiary banks

Ukituma from tanzania US $ zinapitia intermidiary bank Newyork ambako bank husika tanzania watakua na account nayo

Ukituma from tanzania kwenda sehemu yyote duniani kwa US $ zinapitia intermidiary bank Newyork ambako bank husika tanzania watakua na account nayo


Ukituma from tanzania kwenda sehemu yyote duniani kwa Uk £ zinapitia intermidiary bank London ambako bank husika tanzania watakua na account nayo


Ukituma from tanzania kwenda sehemu yyote duniani kwa euro € zinapitia intermidiary bank ujerumani ambako bank husika tanzania watakua na account nayo

Same applies kwa hela zinazotumwa toka nje ya tanzania kuja tanzania


Nduguyo alitakiwa kwenda kwenye branch yake nakuomba INTERNATIONAL INWARD TT INSTRUCTIONS. But bankers wetu walivyo vilaza ni hadi umkute mwenywe ufahamu na hiyo kitu na asiwe na furstrations zake toka nyumabani

Na kwa kiwango cha £60 wasingekukubalia kutuma kwa tt kwani TT huchargiwa kila bank hela inakopita kwa US hufika hadi $60 which meeans wangekwambia zitaliwa hazitafika


Kwa kesi yako bila ww kupata transaction copy, huku bongo hawawezi fanya trace

Pole
 
Majibu yaliyotolewa na baadhi ya wataalam hapo juu yanakidhi lakini sina budi kuongeza. Watu wengi hufikiri kufanya kazi benki ni kama kufanya kazi "dukani kwamba unaweza kuiba change". Mambo sio hivyo. Kutoa pesa kwenye account ya mtu ni ngumu zaidi ya watu wanavyofikiri!

Sasa tuje kwenye suala husika hili la mtoa mada.

Moja, pesa kutoka nje huchukua sio chini ya siku tatu. Baadhi ya benki za nje hazina uhusiano wa moja kwa moja na benki za kitanzania hivyo ukituma pesa, inapitia kwa baadhi ya corresponding banks.

Pili, international transfers ni very risk and sensitive. Kosa kidogo tu linaweza kufanya pesa iende na kurudi. Sasa inategemea na kosa hilo limegunduliwa wapi, na nani. Mara nyingine, makosa ya hapa na pale upelekea ela kukaa suspense account kwa muda fulani likisubiri upande unaohusika kulirekebisha ili ela iende mahali husika.

Kuna walioshauri uombe swift copy. SWIFT ni Society of Worldwide International Fund Transfer..ni mtandao wa kutuma na kupokea pesa duniani. Swift copy, na sio copy of transfer form unayopewa na benki kujaza, hii inakuthibitishia kwamba fedha zako zimetumwa. Ni system generated report confirming money transfer. Unaweza kujaza fomu ya kutuma pesa benki, halafu benki yako baadae wakati wa kutuma transaction inakuwa rejected kwa sababu mbalimbali.

Sasa kama ukipata swift copy na ikaonyesha kweli kila kitu kiko sahihi, mpe huyo ndugu yako aipeleke kwa benki yake. Benki yake inaweza kuitumia pia kuangalia pesa iko wapi.

Kama yote hayo yameenda kama inavyotakiwa, basi nina imani ndugu yako ela ameipata labda anaweza asiwe mkweli kwa sababu ya binafsi au ikawa pungufu kwa sababu ya charges.

Nimalizie kwa kusema..kiasi ulichotuma mbona ni kidogo sana? Kumbuka swift charge sio chini ya USD 50 (TZS 80,000) per transaction. Kama unatuma vijisenti ni bora utumie Western Union, benki ni ghali kwa kutuma vijisenti. Isije ikawa ndugu yako amepata kiasi pungufu ndio maana anasema hajapokea hiyo 150,000!

Jamani benki ni salama! Hakuna benki inaweza kufanya kosa la kitoto la namna hii.
 
Siku nyingine tuma kupitia west union,nimetumia hii njia zaidi ya miaka 5 sijawahi kupata tatizo
 
Bwana rich mambo vp???mimi nipo UAE-Dubai tangu 2004 natuma pesa kwenye acc ya TZ bila tatizo,natumia Western union ambayo gharama yake ni ndogo 45 uae dhs ($12 ) na ndani ya siku tatu(siku za kazi) pesa inakuwa Tz..na kama kuna tatizo(japo halijawai kunitoke kwa hicho kipindi chote) watapata habari na watakwambia
 
Nduguyo alitakiwa kwenda kwenye branch yake nakuomba INTERNATIONAL INWARD TT INSTRUCTIONS. But bankers wetu walivyo vilaza ni hadi umkute mwenywe ufahamu na hiyo kitu na asiwe na furstrations zake toka nyumabani
Yeye ndio anatakiwa awe na TT outward copy, na afanye tracing hukohuko, beneficiary bank hawajapata huo mzigo, sasa unawahusishaje? kwa hili wewe ndio KILAZA na wala sio bankers wa TZ




Na kwa kiwango cha £60 wasingekukubalia kutuma kwa tt kwani TT huchargiwa kila bank hela inakopita kwa US hufika hadi $60 which meeans wangekwambia zitaliwa hazitafika
Unazidi kupotosha watu, hata pound 10 anaweza kutuma, kuna namna tatu ya kuhandle charges, SHA bank charges hugawanywa kwa sender na receiver, OUR bank charges hubebwa na sender na Mwisho BEN ambapo bank charges hupelekwa kwa beneficiary, Sasa kama alienda kwa 2nd option (OUR) manake charges zote zinabebwa na sender, hata kama umetuma pond 10 inafika.




Kwa kesi yako bila ww kupata transaction copy, huku bongo hawawezi fanya trace
Hata kama uko na hiyo copy, Huku bongo kufanya trace ni kukusaidia tu, kule pesa imetoka ndio trace inatakiwa ifanyike
 
Unazidi kupotosha watu said:
Ukatume $10 kwa charge ya $20????? you must be a confuser!!!!!!!!! au kilaza mwingine wa bank fulani hapa mjini na shule umemaliza banking IFM
 
Mie nashauri uchukue swift copy kwa benki yako uliyotuma pesa huko ugaibuni, Swift copy ita acknowledge pesa yako imeenda wapi mkuu.
 
Nenda katika bank uliyotuma huko ughaibuni waombe wakupe swift copy ambayo inaonyesha pesa ilipotoka, chanel ilipopitia hadi ilipoishia.
TT huwa zinazingua sana huenda ime'bounce somewhere. Good news ni kwamba ni very easy ku'trace.
Otherwise nina mashaka na huyo ndugu yako uliyemtumia pengine ameshaipata ila analeta sanaa za kibongo bongo.
Kweli kabisa hela huwa haipotei Benki hasa (BOT) unachotakiwa mtumie huyo nduguyo hizo copy yeye aende BOT ndio utakapomjua mwizi wako huenda ni yeye mwenyewe keshazichukua Ndibalema upo sahihi, maana hat pesa za kwenye Mobile (M-Pesa, tiGo Pesa nk) hazipotei ije iwe hiyo ya ughaibuni, huyo jamaa yake naona anataka kumzika
 
Last edited by a moderator:
Ukatume $10 kwa charge ya $20????? you must be a confuser!!!!!!!!! au kilaza mwingine wa bank fulani hapa mjini na shule umemaliza banking IFM

Out of Point! Hujitambui wewe

kama charge ni kubwa kuliko amount hiyo ni decision ya anayetuma, aendelee au aache.

hata kama ni dola 1, as long as bank wamepata comm yao kwa nini wakatae kutuma?
 
Yeye ndio anatakiwa awe na TT outward copy, na afanye tracing hukohuko, beneficiary bank hawajapata huo mzigo, sasa unawahusishaje? kwa hili wewe ndio KILAZA na wala sio bankers wa TZ


Unazidi kupotosha watu, hata pound 10 anaweza kutuma, kuna namna tatu ya kuhandle charges, SHA bank charges hugawanywa kwa sender na receiver, OUR bank charges hubebwa na sender na Mwisho BEN ambapo bank charges hupelekwa kwa beneficiary, Sasa kama alienda kwa 2nd option (OUR) manake charges zote zinabebwa na sender, hata kama umetuma pond 10 inafika.





Hata kama uko na hiyo copy, Huku bongo kufanya trace ni kukusaidia tu, kule pesa imetoka ndio trace inatakiwa ifanyike

Out of Point! Hujitambui wewe

kama charge ni kubwa kuliko amount hiyo ni decision ya anayetuma, aendelee au aache.

hata kama ni dola 1, as long as bank wamepata comm yao kwa nini wakatae kutuma?

My point of argument was huwezi tuma pesa dierct(called wire transfer) to a bank account in tanzania bila kwanza anyetumiwa pesa kwenda kwenye bank branch yake nakuomba inward tt instructions toka bank husika, hizo instructions anamtumia huyo anaye mtumia hizo pesa aende kwa bank yake huko nje ya nchi akafanye hiyo transaction na mfano wake ni huu

View attachment INWARD TRANSFER DATEILS.pdf

For USD $, and for View attachment Inward TTs-GBP.pdf british pounds

Note: kila bank ina form yake attached is from my bank i use na hii form for instructions for inward tt bankers wanaiona dili or ukiwauliza juu juu watakwambia nao hawajui?

Pia kuna mifumo mingine ya kuweza tuma pesa tanzania tokea nje ya nchi e.g Western Union, Mony Gram, unofficial via specific bearu de change n.k

siku ingine uwe unasoma usigombane na keyboard utaumia .......
 
Pia kuna mifumo mingine ya kuweza tuma pesa tanzania tokea nje ya nchi e.g Western Union, Mony Gram, unofficial via specific bearu de change n.k
Najua but again it is irrelevant kwa huu uzi



Note: kila bank ina form yake attached is from my bank i use na hii form for instructions for inward tt bankers wanaiona dili or ukiwauliza juu juu watakwambia nao hawajui?

Ukisaidiwa saidika, hizo wiring instructions huwa zipo wazi tu,normally unapata hizo taarifa hata kwa website, lakini mtu keshatuma pesa, hizo details zinamsaidiaje sasa?

attachment nyiiingi hakuna unachoongea, hizo details zitamsaidia mtu ambaye anataka kufanya transaction lakini kama transfer ishafanyika (ambayo ndio mada hapa), hizo zitamsaidiaje ku-Trace?


Ukifundishwa fundishika mdogo wangu, umemaliza form four 2012 nini?
 
Back
Top Bottom