Nimeuza kiwanja na kununua simu ya ndoto yangu

Nimeuza kiwanja na kununua simu ya ndoto yangu

Dah, Sasa mkuu, hata kama nitaiuza kwa 2m na kununua bidaboda, hiyo 7k ya siku nitakayoletewa itanifaa nini kurudisha kiwanja? Hiyo hela ya kununua kiwanja pembezoni mwa barabara kama kile nitaifikisha lini? Je, niwadanganye vipi ndugu kuhusu kiwanja kwa sasa ili wanielewe wasinichukulie kama shetani? [emoji24][emoji24]
kama hiyo simu inakuingizia zaidi ya 7k basi kaa nayo, uijengee na kaofisi kake
 
Safi sana mkuu fanya kile moyo wako umependa na unahisi kitakupa furaha.

me nadhani tumpongezeni kwa uthubutu.
 
Vijana wasio na mchango kwa Taifa
Mkuu, naomba ushauri wa nini cha kufanya. Napitia wakati mgumu sana, naogopa kukaa ndani peke yangu maake naweza kujichoma kisu[emoji24][emoji24][emoji24]
 
Safi sana mkuu fanya kile moyo wako umependa na unahisi kitakupa furaha.

me nadhani tumpongezeni kwa uthubutu.
Mkuu, sina furaha kwa sasa. Moyo unaweweseka, kiwanja sio karatasi mkuu[emoji24][emoji24]
 
Habari wakuu,

Hapa nilipo nimejaa kitete siyo poa. Yaani hata sielewi, ingawa maamuzi niliyoyachukua nilishauriana na moyo wangu nikaridhika, lakini still nafsi inanisuta.

Nimeuza kiwanja changu cha urithi nilichopewa kwenye mgao wa familia, tena kiwanja kilicho barabarani kabisa. Nilitakiwa kukiuza kwa Tsh. Mil 18 (atleast), lakini nimejikuta nakiuza kwa milioni tano ili ninunue simu ya ndoto yangu kabla haijatoka kwenye chati.[emoji24][emoji24]

Tayari nishafanya yangu. Nimenunua kitu cha Samsung Galaxy Z Fold 4 kwa Mil. 4 na laki 9. Hapa mfukoni nimebaki na laki tu. [emoji24][emoji24] Kiwanja kimeenda. Naombeni mnipe moyo ili nisiugue presha mwenzenu, nafsi inatapatapa maskini[emoji24][emoji24], bora hata ningefungua biashara.

Nilivutiwa na hii simu kwa sababu imekaa kama kitabu, nikiifungua inaungana vioo viwili inakuwa kama ka TV kadogo, kamera safi na hadhi ya kimataifa.

Moyo umejaa kitete, nifanyeje? [emoji24][emoji24]View attachment 2428948
Hiyo laki tatu unga bundle la Super speed sijui super faster ndio uta enjoy hiyo simu
 
Unaacha kufurahia maisha na mkeo mnajibana mnunue asset, mjenge msomeshe watoto ili badae wasije oata shida mkiwa mmetoweka duniani, mwisho wa siku unakufa kwa maradhi yaliyotokana na msongo wa mawazo, kukosa mda wa kupumzika na kufurahia maisha unakufa unaacha Mali kwa wanao wanao mwisho wa siku ndio hawa pumbafu kabisa

MY TAKE
Jamani tuishi kula vizuri, lala vizuri furahia maisha na mkeo watoto watatafuta na wao si mnaona upumbafu huu
 
Nina laki tatu niuzie mkuu
Dah[emoji29] Yaani hata 10% ya gharama ya simu haifikii. Si bora niitishe kikao cha ukoo niiweke simu kati kati yao ili waichalange mapanga mbele yangu[emoji24][emoji24]
 
Unaacha kufurahia maisha na mkeo mnajibana mnunue asset, mjenge msomeshe watoto ili badae wasije oata shida mkiwa mmetoweka duniani, mwisho wa siku unakufa kwa maradhi yaliyotokana na msongo wa mawazo, kukosa mda wa kupumzika na kufurahia maisha unakufa unaacha Mali kwa wanao wanao mwisho wa siku ndio hawa pumbafu kabisa

MY TAKE
Jamani tuishi kula vizuri, lala vizuri furahia maisha na mkeo watoto watatafuta na wao si mnaona upumbafu huu
[emoji24][emoji24]Usiseme hivyo mkuu, unafanya nione kama laana itanitafuna mkuu
 
Sio wewe tu, kuna aliyeuza nyumba akanunua gari zuri la kutembelea ili aendane na wakati. Labda nafikiria kuna wakati ubongo unachanganyika na makamasi. Uwezo wa maamuzi unakuwa mdogo.
 
Habari wakuu,

Hapa nilipo nimejaa kitete siyo poa. Yaani hata sielewi, ingawa maamuzi niliyoyachukua nilishauriana na moyo wangu nikaridhika, lakini still nafsi inanisuta.

Nimeuza kiwanja changu cha urithi nilichopewa kwenye mgao wa familia, tena kiwanja kilicho barabarani kabisa. Nilitakiwa kukiuza kwa Tsh. Mil 18 (atleast), lakini nimejikuta nakiuza kwa milioni tano ili ninunue simu ya ndoto yangu kabla haijatoka kwenye chati.[emoji24][emoji24]

Tayari nishafanya yangu. Nimenunua kitu cha Samsung Galaxy Z Fold 4 kwa Mil. 4 na laki 9. Hapa mfukoni nimebaki na laki tu. [emoji24][emoji24] Kiwanja kimeenda. Naombeni mnipe moyo ili nisiugue presha mwenzenu, nafsi inatapatapa maskini[emoji24][emoji24], bora hata ningefungua biashara.

Nilivutiwa na hii simu kwa sababu imekaa kama kitabu, nikiifungua inaungana vioo viwili inakuwa kama ka TV kadogo, kamera safi na hadhi ya kimataifa.

Moyo umejaa kitete, nifanyeje? [emoji24][emoji24]View attachment 2428948
Nina 1.5m cash NIUZIE HIYO SIMU na anzisha biashara mara moja ili UJE UNUNUE KIWANJA KIKALI KULIKO ULICHOKIUZA....
 
Sio wewe tu, kuna aliyeuza nyumba akanunua gari zuri la kutembelea ili aendane na wakati. Labda nafikiria kuna wakati ubongo unachanganyika na makamasi. Uwezo wa maamuzi unakuwa mdogo.
[emoji24][emoji24][emoji24]Aisee, badala ya kunifariji, umeamua kuniulia mbali kabisa. Amaa kweli, sifai tena kuishi[emoji24][emoji24]
 
Nina 1.5m cash NIUZIE HIYO SIMU na anzisha biashara mara moja ili UJE UNUNUE KIWANJA KIKALI KULIKO ULICHOKIUZA....
Dah, mkuu, fanya walau mbili na laki tatu. Nakuomba lakini, walau nitakuwa na uhakika wa kufanya biashara fulani, ndani ya miezi sita nikafanikisha pesa hata ya kununua kiwanja kwa 10m, japo sidhani kama kitakuwa eneo zuri kama lile

Mkuu, umekubali? Walau tugawane hasara tu, hakuna namna[emoji24][emoji24]
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]! Zuzu namba wani
Aisee, badala watanzania mnipe moyo, ndio kwanza mnanisanifu dah, sio poa kwa kweli. Naelekea duka la madawa sasa hivi kufanya yangu [emoji24][emoji24]
 
Back
Top Bottom