Half american
JF-Expert Member
- Sep 21, 2018
- 38,283
- 97,793
Hapana mkuu kwa sasa focus yangu ni kuweza kuwa accommodate wateja nilionao ifike kipindi nisikose hata muamala kisa eti sina cash au float nikishafika level hiyo ndio nitafikilia kuongeza kitengo kingineHongera sana Mkuu, naamin ukiachana na ofisi yako bado unaendelea zaid kujitanua (kuongeza assets)
Ahsante mkuu, hakika biashara inahitaji uvumilivu wa hali ya juu na kutokukata tamaa kwani upepo muda wowote unaweza badilika ukaanza kupata matumainiHongera mkuu na hayo ni matokeo ya kuamini kile unachokifanya bila kukata tamaa. Focus yako kwenye mipango yako inakulipa sasa, ungekubali kuyumbishwa na wayasemayo leo hii ingekuwa majuto.
Hakika mkuuAhsante mkuu, hakika biashara inahitaji uvumilivu wa hali ya juu na kutokukata tamaa kwani upepo muda wowote unaweza badilika ukaanza kupata matumaini
Tupambane tusikate tamaa siku moja tutatoboa tu
sahihi kabisaKwemah wakuu,,,tunapeana tu motisha na kuongeza mapambano ya kila siku hasa kwa wadundulizaji kama mimi
Iko hivi, nilipomaliza chuo niliingia zangu kitaa na idea ya kuuza vifaa vya simu na tigo pesa ambayo nilikuwa naifanya toka nikiwa chuoni hasa tukifunga chuo au nikiwa mwanzoni mwa semester hiyo ilikuwa 2019
Wakati naanza kazi ilikuwa ngumu sana kwa siku wateja hawazidi kumi na wakija wanakuja wale walioshindwa na madoni wa mtaa yaani wanataka kutuma au kutoa mpunga mkubwa ambao sikua nao na biashara ya accessories ilikuwa haisogei kabisa
Changamoto kubwa ilikuwa majungu ya wateja na maneno yao ya kukatisha tamaa mara wakwambie kama huna si ufunge mara wakuchane live kuwa hapa hutoboi fulani ndio kila kitu na ukizingatia sikuwa na mtaji wa maana lakini niliendelea kupambana kwani sikuwa na idea ya biashara nyingine hata kama kamisheni ilikuwa ndogo sana kipindi kile bado niliendelea kupambana
Hadi kufika muda huu ni takriban miaka 5 nashukuru Mungu kijiwe kimechangamka wakati mwingine unashindwa kupata hata muda wa kula kwa ubize, cha kushangaza ni kuwa walewale waliokuwa wakinikatisha tamaa ndio marafiki zangu na wateja wangu wakubwa
Huwa wakija watapiga stori za mawakala wengine na kukupa umbea mwingi na uongo sijui wamefirisika, walikuwa na pesa za mkopo n.k lakini kwakuwa naijua biashara huwa siwasapoti kiviile zaidi ya kuwaitikia na kutabasam kama vile nawasapoti ilimradi kazi inaenda safi
Mwisho, kwa experience yangu ndogo ya miaka mitano nimegundua biashara yoyote changa inapitia hatua nyingi sana hadi kuimarika kabisa inaweza chukua miaka hadi 10 au 20 kuwa doni wa mtaa kwa hiyo vijana tusikate tamaa hasa kama umeamua kuwa upande wa biashara wakati wetu uwaja
Ahsanteni
Nieleweshe kuhusu super agent MkuuNa hayo ndio malengo yangu, ila nataka nitafute capital ya kutosha kwa income yangu sitaki kuingia chocho za depts najua safari itakuwa ndefu sana ila nitaifikia inshallah
Hivi mawakala wakuu profit ratio yao ktk kamisheni kwa muamala mmoja inalingana na mawakala wa kawaida? na je super agent pia anaweza akafanya na miamala ya kawaida?Wanaitwa mawakala wakuu ambao wakala wa kawaida anaenda kuweka au kutoa float kwake
Ni vizuri lakini kuna kanuni moja inasema usiweke mayai yote kwenye kapu moja.Hapana mkuu kwa sasa focus yangu ni kuweza kuwa accommodate wateja nilionao ifike kipindi nisikose hata muamala kisa eti sina cash au float nikishafika level hiyo ndio nitafikilia kuongeza kitengo kingine
Ushauri mzuri nasubiri kisa nipate kujifunzaNi vizuri lakini kuna kanuni moja inasema usiweke mayai yote kwenye kapu moja.
Siku nikitulia nitaeleza kisa changu chote mpak kufikia level nilizopo sasa hivi... Binadamu ni watu wabaya sana wenye roho za kichawi na husda hasa ukifanikiwa mbele ya macho yao.
Mkuu nakufuata pmTafuta Mil 10 uwe super agent.
#YNWA
#YANGA_BINGWA
Ni vizuri lakini kuna kanuni moja inasema usiweke mayai yote kwenye kapu moja.
Siku nikitulia nitaeleza kisa changu chote mpak kufikia level nilizopo sasa hivi... Binadamu ni watu wabaya sana wenye roho za kichawi na husda hasa ukifanikiwa mbele ya macho yao.