Wakuu habari zenu.
Ulinzi wa taifa hili ni la wananchi wote na napenda kuishi kwa amani ndani ya nchi yangu.
Mimi ni kijana mpole na mbambe ninapochokozwa na huwa sipendi uonevu kutokana na sehemu nilipokulia,Mimi kwetu ni rorya Kanda maalum na siku zote nilishakataa kuwa siwezi kusumbuliwa na hawa watoto wanaojiita panya road ,kama ubabe nilifanya sana kipindi nachunga kule kwetu na nilipiga sana watu rungu na najua sana kucheza na silaa kwenye ishu kama hizi ndogo ndogo.
Ilikuwa hivi ,nilienda kuangalia eneo langu maeneo ya majohe huku Bomba mbili, nikawa natembea hivi mita kama 100 hivi nikaona kundi la vijana wadogo tu wanakuja nikasema hawa watakuwa panya road , kwenye begi langu nilikuwa na panga tena Haina hata wiki tena nimeinunua pale buguruni.nikaivaa Ile begi kwa mbele nikajisemea hapa kama ni wao atakae jipendeza itakula kwake, kabla mita kama 50 hivi mbele nikapita kushoto Ili kujiandaa vizuri ,wakaniona na kuanza kuniambia toa ulichonacho, wakaja kumi na tano nikawahesabu fasta.
Wakaja kama wanataka kunivamia ,sikuwachelewesha wale watoto na sikuona huruma,roho ya unyama ukanijaa fasta, niliwatembezea kichapo ,wale watoto nimewakata panga bila huruma, nilivyokuwa nawapiga mapanga wakawa wanakuja wengi na walivyokuwa wafupi ndo nilikuwa nawakata bila huruma,
Maeneo ya miili Yao kama mikono,vichwa na mabega nimewakata sana.nikasikia wanasema jamani huyu mkuria tukimbie[emoji3][emoji3] wakaondoka kwa kuvutana nikatamani kuwafuata nikawamalize Moja kwa Moja, na Mimi nikatembea,
Na naamini kabisa wale watoto hawafiki makao watadondoka tu njiani maana nimewapapasa sehemu muhimu.