Nimewatengenezea hii wana cybersecurity

Nimewatengenezea hii wana cybersecurity

kali linux

JF-Expert Member
Joined
May 21, 2017
Posts
2,192
Reaction score
5,685
Hello bosses,

Nimekua nashiriki kwenye bug bounty programs na Pentesting lkn nikaja kugundua changamoto kubwa ni vifaa(software tools & scanners) pamoja na poor reporting. Yaan pentesting project nloifanya miezi sita ilopita ilibidi niianze upya kwa sababu tu sikua na report ambayo ni endelevu kwangu na kwa mteja wangu.

Kwa kuwa mwaka huu niliamua kuwa FOSS Developer kwa 20% ya muda wangu (Free Open Source Software) basi nikaona ni bora nianzishe hii project itakayosaidia wanafunzi na professionals kwenye cybersecurity na bug hunting. Isitoshe nimetumia Burp Suite, ZAP na Metasploit lkn zote kuna mwanya sana kuhusu reporting na inambidi researcher atumie external aid kutunza report yake. Vile vile cost kubwa kupitiliza ni hindrance kubwa kwenye kupata damu mpya ndani ya hii field.

Nimeamua kutengeneza software ambayo ni Kama IDE lkn ni maalum kwa pentesting. Hii software ni Integrated Pentesting Environment. Imebeba vitu vifuatavyo:

1) Guides & How tos
2) Tools & Scanners (New & efficient tools)
3) Workflow management
4) Efficient Reporting

Kuhusu tools sio kwamba nina 'reinvent the wheel' bali nina tools zangu nilizoandika mwenyewe ndizo naziboresha na kuziintegrate humo. User ataweza tumia tools nyingine za nje kama vile Burp na ZAP kisha kureport results kwenye hii software.

Pia software itamfanya researcher aende step moja baada ya nyingine kwa guide maalum ambayo itamfanya agundue bugs nyingi zaidi kwani kila step hutegemea step ya nyuma yake.

Lengo kubwa la kuleta huu uzi hapa ni kukusanya maoni ya wadau kuhusu features wanazozitaka then nitaona namna ya kuziweka. Project ni opensource ipo github ukitaka kushiriki kwenye development nijulishe PM au hapahapa kisha nitakupa muongozo.

Screenshot 2022-07-05 155600.png

Screenshot 2022-07-05 154707.png

Peace
~ kali linux
 

Attachments

  • Screenshot 2022-07-05 155600.png
    Screenshot 2022-07-05 155600.png
    22.8 KB · Views: 40
  • Screenshot 2022-07-05 154707.png
    Screenshot 2022-07-05 154707.png
    46.3 KB · Views: 39
This is so big congratulations bro!!!
I wish I could add some new notions on your project but this isn't my area of proficiency.
 
Toka Jana wachangiaji hakuna dah
Nadhan pia jf kuweka trending news kwenye homepage imetengeneza distraction kubwa kwa wale fans wa jukwaa fln. Yaan unakuja na lengo la kusoma news za tech lkn unakutana na story hapo homepage zinakudistract, polepole inakutoa kwenye line
 
Nadhan pia jf kuweka trending news kwenye homepage imetengeneza distraction kubwa kwa wale fans wa jukwaa fln. Yaan unakuja na lengo la kusoma news za tech lkn unakutana na story hapo homepage zinakudistract, polepole inakutoa kwenye line
Kweli kabisa kwenye trending unakutana na Uzi wa kula tunda huwezi kuja Huku tech aisee
 
Share Git repository yake mkuu tupitie kama kunae suggestion Hongera kwa hii kitu mkuu #pythonista
Nmeongelea kwenye uzi kwamba kama unataka kushiriki kwenye coding basi nicheki PM, project ni open source na iko Github lkn kutokana na complex nature yake na u-serious nlonao kwenye hio project ni lazima niwe nna uhakika beyond doubt kwamba unaweza kuchangia. Sababu ya kufanya hvo pia ni kwamba kuna resources natoa kwa wanaochangia codes ambazo bila hizo ni ngumu kwa mchangiaji kutoa msaada utakaokuwa na tija.

Kwa hapa unaweza suggest features na changamoto unazokutana nazo kwenye pentesting process kisha nitatoa feedback kila nnaposolve hzo challenges.

Vile vile unaweza suggest vitu vinavyohitaji automated scanners ambavyo labda kwa sasa scanners zilizopo haziperform vizuri ama hazipo kabisa.

Lengo kubwa ni kutoka na world class Integrated Penetration Software.
 
Back
Top Bottom