Nimezaa na Mwanamke kutoka familia ya washirikina, najitoaje?

Nimezaa na Mwanamke kutoka familia ya washirikina, najitoaje?

alovera

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
220
Reaction score
173
Habari za siku nyingu wandugu, Mwaka 2010 nilioa mwanamke tuliyedumu naye uchumba takribani miaka 5 tena ndoa ya kanisani lakini huyo Mke aliniacha naye akakimbila USA, baada ya hapo mwaka 2012 nikapata mwanamke ambaye nilimkuta na mtoto mmoja ,na sasa tumeshazaa watoto watatu.

Shida yangu ni kuwa kwao huyu binti upande wa Mama yake ni wachawi sana. Bibi yake alishawahi kumdhuru mwanangu wa kwanza mara mbili tukaponea kwa waganga.

Na toka hapo nikapiga marufuku watoto wangu kukanyaga kwao. Siku za karibuni hasa baada ya kutumia Tiba ya Chumvi kama ilivyoelekezwa na baadhi ya members humu jukwaani,nahisi kama nimezinduka fulani naye ameanza kusema kuwa sina mapenzi naye na kuna kipindi anataka kuondoka (nahisi anatishia kwani haondoki).

Binafsi nina amani sana na wanangu lakini yeye hana amani kabisa na kila siku ni malalamiko tu. Lakini sababu kubwa ya malalamiko ni kuwa nimekata mirija yake mingi ya fedha nilizokuwa nampatia yeye na ndugu zake na pia nimemkataza mawasiliano na ndugu zake ambao nahisi ndio wanaopitisha ushirikina kwaangu,

Hili la mawasiliano limeshindiakana kwani nimekuja kugundua kuwa anawasiliana nao kwa siri,lakini pia ndugu zake ikiwamo mama yake wameanza chuki kubwa kwangu na nahisi nashambuliwa sana kishirikina,hatua nilizochokua kwanza ni kuzidisha ibada na sala,pili natumia tiba ya chumvi.

Ushauri naouomba kwenu wanaJamii Forums,nifanyeje niachane na huyu mwanamke bila kuleta mtafaruku kwenye familia yangu tena mimi ndio nibaki na watoto kwani akienda nao kwao nahisi wanangu watadhurika au nao wataingizwa kwenye uchawi.

Nawasilisha
 
Mfukuze kiakili mwambie nenda ukasalimie kwenu wiki ijayo mimi nakuja akisepa naww kama hujajenga timua hamia sehemu nyengine. Wachawi sio watu wazuri kadri unavyozidi kukaa nae ndio fursa zaidi kwao kutaka kukuuwa au kukudhuru au kuharibu mipango yako na familia yako. Kama wewe ni mbambe mtimue kwa nguvu mpe baadhi ya vipande vya mali afu tembea. Huwezi ishi na tatizo ndani afu bado ukaendelea kulifuga mnakua mnaishi kwa kuviziana sasa.
 
Mkuu unatumiaje Tibaa ya chumvi?
Nijibu hili Kwanza Kama namm ninapitia Hali inayoendana na hiyo nmejenga bila kujua mtaa ambao unawashirikina balaa
 
Haya yalimkuta kuna jamaa yangu. Aliteseka sana..binti alikua mzuri kwelikweli wa sura na umbile. Kumbe mwanga kuanzia ye mwenyewe, mpaka wazazi. Nasema alipata tabu, maana mwanamke alikua hataki kusikia neno la kuachika. Mwanamke alikua mpare, jamaa mtu wa Rombo. Oyaaa aliteseka mwamba mpaka alivyoweza kuachana naye hakuwahi kurudi nyuma kabisa kuhusu suala hata la mtoto. Anasema akikua mkubwa atamtafuta mwenyewe.
 
Ushamzalisha watoto watatu ndio unampa sifa ya ushirikina Ili umuache🤣 We Kama uchawi wake sio wa kukuua komaa nae tu, sa ukimuacha ataenda wapi?

Halafu wanaume punguzeni nongwa, Yani kupewa viuchawi kidogo tu Ili mtupende na muwahi kurudi nyumbani kucheza na watoto ndio kesi? Wenzenu wanafanywa misukule huko wanapalilia mahindi saa hizi.....jikaze bro ndo mapenzi, usimuache.
 
Ushamzalisha watoto watatu ndio unampa sifa ya ushirikina Ili umuache🤣 We Kama uchawi wake sio wa kukuua komaa nae tu, sa ukimuacha ataenda wapi?
Halafu wanaume punguzeni nongwa, Yani kupewa viuchawi kidogo tu Ili mtupende na muwahi kurudi nyumbani kucheza na watoto ndio kesi? Wenzenu wanafanywa misukule huko wanapalilia mahindi saa hizi.....jikaze bro ndo mapenzi, usimuache.
tuseme ni kaka yako amefanyiwa hivi tena kaka yako wa damu baba mmoja mama mmoja vipi ungeshauri hivi???
 
Najua uchawi upo ila siamini kurogwa.

Una hofu, lazima udhurike.
 
Umesha zaa na mwana mke watoto watano ndo sasa unaona uchawi wake, wewe u.emxhoka tu, kisingizio cha ushirkina ni dhaifu 90% familia za kiafrica huamini kwenye ushirikina japo in most cases is just scam.
 
Hajarogwa huyu anatafuta sababu, tuliosoma Cuba tushajua karesume mawasiliano na mzazi mwenzie wa US, anataka amuache mkewe.....masingle dad sio kabisa🤣🤣
hahahahahahaa nilikua sjaelewa
 
Mfukuze kiakili mwambie nenda ukasalimie kwenu wiki ijayo mimi nakuja akisepa naww kama hujajenga timua hamia sehemu nyengine. Wachawi sio watu wazuri kadri unavyozidi kukaa nae ndio fursa zaidi kwao kutaka kukuuwa au kukudhuru au kuharibu mipango yako na familia yako. Kama wewe ni mbambe mtimue kwa nguvu mpe baadhi ya vipande vya mali afu tembea. Huwezi ishi na tatizo ndani afu bado ukaendelea kulifuga mnakua mnaishi kwa kuviziana sasa.
Chukua hii.
 
Back
Top Bottom