Nimrod Mkono na Mkono Advocates watch

Nimrod Mkono na Mkono Advocates watch

Kwa mlio Bongo, masaa 48 nadhani yametimia, je kuna apology yoyote toka kwenye magazeti ya Kulikoni na ThisDay? Ninatamani sana kufahamu hatima ya mkwara wa Mh Mkono!
 
Admin Naoma Uiweke Post Yake
Mbunge alia mafao kiduchu kwa wasomi.

Asema wanazidiwa hata na makarani. Akumbuka enzi za Nyerere
Na Joseph Damas, Dodoma.

MBUNGE wa Kyela (CCM) Dk. Harrison Mwakyembe amesema
wahadhiri wa vyuo vikuu nchini hawafundishi vizuri kutokana na kulipwa mishahara midogo, inayozidiwa hata na makarani wa wizara.

Alisema hatua hiyo imesababisha wahadhiri wengi kutumia muda
mrefu katika miradi yao binafsi ili kuweza kujiongezea kipato cha kutunza familia zao.

Dk. Mwakyembe alisema hayo alipokuwa akichangia hotuba ya makadirio ya matumizi ya Wizara ya Elimu ya Juu, Sayansi na Teknolojia kwa mwaka wa fedha 2007/2008 iliyowasilishwa bungeni jana na Waziri, Profesa Peter Msolla.

Alitoa mfano kwamba makatibu wakuu wanapostaafu wanalipwa sh. milioni 172 na kila mwezi wanalipwa zaidi ya sh. milioni moja, tofauti na wahadhiri wa vyuo vikuu ambao wanapostaafu wanalipwa fedha kidogo.

Alitoa mfano wa wahadhiri wa vyuo vikuu wanapostaafu wanalipwa kwa mkupuo sh. milioni 30, kiwango ambacho alisema ni kidogo na ndiyo maana huwalazimu kwenda mitaani kujiongezea kipato.

Dk. Mwakyembe alisema wakati wa utawala wa Baba wa Taifa,
Hayati Mwalimu Nyerere watumishi waliokuwa wakilipwa mishahara mikubwa kuliko wote walikuwa ni wahadhiri na watunza maktaba, lakini sasa mawaziri na makatibu
wakuu wa wizara ndio wanapata mishahara na mafao manono.

Alisema hatua hiyo imechangia
kushuka kwa elimu nchi hasa kwa masomo ya sayansi.

Dk. Mwakyembe alisema wasomi ambao ndio dira kubwa katika kuzalisha elimu bora nchi, wanalipwa mishahara midogo na kwamba, hata wanapostaafu wanapewa marupurupu ya chini kuliko hata makarani wa Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika.
"Katika utawala wa Nyerere watu waliokuwa wanalipwa vizuri ni wahadhiri na watu wa maktaba kutokana na kwamba, ndio wazalishaji na waendelezaji elimu nchini.

"Hivi sasa utashangaa mishahara mikubwa ni kwa ajili ya mawaziri na makatibu wakuu, wahadhiri wanalipwa
mishahara midogo sasa wengi hawafundishi vizuri na wanatumia muda mrefu kufanya miradi binafsi," alisema

Dk. Mwakyembe ambaye ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Kitivo cha Sheria.

Alisema haiwezekani kuingia kwenye dunia ya wasomi kwa kumkabidhi Profesa Msolla gari ambalo halina
matairi na kwamba, kama tutaingia kwenye Jumuiya ya Afrika Mashariki basi tutaburuzwa vibaya.

Akizungumzia kuhusu malalamiko ya mikataba ya madini, Dk. Mwakyembe alisema hatua hiyo inatokana na mikataba hiyo kutopitia kwenye kitengo cha Sheria cha Chuo Kikuu kwa ajili ya kupitiwa na wanasheria wenye fani
yao.

Alisema mawaziri wamekuwa wakipeleka mikataba mikubwa yenye maslahi ya taifa kwenye kampuni za nje kwa sababu ya mikato na kukiacha kitivo cha sheria tofauti na zamani ambapo watalaam wake walikuwa wakishirikishwa kikamilifu.

"Kuna suala la mikato, hii itatumaliza jamani hivi ni virusi. Kama mikataba ya madini ingepitia kwenye kitivo cha sheria kusingekuwa na malalamiko, lakini kwa sababu watu wanapenda mikato," alisema bila kufafanua maana halisi ya mikato.

Katika kuonyesha kukerwa kwake, Dk. Mwakyembe aliweka bayana kuwa, katika bajeti zinazokuja hataunga
mkono wizara ambazo zitapata ushauri wa kuingia mikataba kwenye kampuni binafsi bila kupitia kwa watalaam wa vyuo vikuu.

Dk. Mwakyembe pia alitaka maelezo ya kina kutoka kwa Profesa Msolla kufuatia kusimamishwa kwa ujenzi wa taasisi ya MIST kuwa chuo kikuu na badala yake kujengwa mkoani Arusha.

Naye Wilson Masilingi (Muleba Kusini-CCM) akichangia alisema kwa
kawaida nchi ikiwa masikini basi haitakuwa tofauti na familia masikini, ambayo migogoro ndani ya nyumba ni
kitu cha kawaida.

Alisema wanafunzi wengi nchini wanatoka kwenye familia masikini, hivyo kitendo cha serikali kuwataka
wachangie asilimia 40 na kuwakopesha asilimia 60 hakiwezi kuwasaidia.

Masilingi ambaye alikuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utawala Bora katika serikali ya awamu ya tatu, alisema serikali haijachangia elimu kwa
wanafunzi wa vyuo vikuu, kwani huwezi kumkopesha mtu na kujigamba kuwa umechangia elimu yake.

Alisema Rais Jakaya Kikwete aliwahi kuwahakikishia wanafunzi wa vyuo vikuu kuwa, watasoma watoto wote wa
masikini, lakini baadhi ya watendaji wamekuwa wakikwamisha na hivyo ahadi ya Rais kushindwa kutekelezwa.
Masilingi alisema alifurahishwa jinsi
tatizo la mgomo wa wanafunzi wa vyuo vikuu lilivyotatuliwa, lakini alionyesha kushangazwa na tatizo hilo kusababishwa na asilimia 40 ambayo
wanafunzi masikini wanatakiwa kuichangia.

Alisema elimu ndio msingi bora duniani kote, lakini hatua iliyofikia sasa inatia shaka, kwani walimu wengi hawafundishi inavyotakiwa na muda mwingi wanautumia kutafuta fedha mitaani.

Naye Benson Mpesya (Mbeya Mjini-CCM) alionyesha kukerwa kwake na hatua iliyochukuliwa na
serikali ya kutengua maagizo yaliyotolewa na Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere.

Alisema Baba wa Taifa aliagiza kuwa Taasisi ya Sayansi na Tekonolijia Mbeya (MIST) iboreshwe na kuwa Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia, lakini hivi
karibuni serikali ilikiuka maagizo hayo licha ya maandalizi kufanywa.

Mpesya akionekana mwenye uchungu alihoji hatua ya serikali kuelekeza nguvu zake katika ujenzi wa Chuo
Kikuu kipya cha Nelson Mandela mjini Arusha, ambacho kinategemea fedha za wahisani na kufuta mpango wa
kuifanya MIST kuwa chuo kikuu ambapo tayari kilitengewa fedha na nyingine kutumika kulipa fidia wananchi.

"Mnakiuka maagizo ya Baba wa Taifa, inawezekana mnatafuta laana au nini? Ni lazima tufuate maagizo japo ametangulia mbele za haki, sasa kwanini serikali inakuwa kigeugeu," alihoji Mpesya huku akimuuliza Mwenyekiti wa kikao Jenista Mhagama amwage machozi ama la.

Mpesya aliiomba serikali kubadilisha uamuzi na kuifanya MIST kuwa chuo kikuu kama ilivyoagizwa na watalaamu kutoa baraka zao na kwamba, sababu ilikuwa ni kumuenzi Mandela basi mkoa wa Mbeya ndio unastahili kwa sababu mpigania uhuru huyo aliishi na kusaidiwa na watu wa mkoa huo.

Kwa upande wake, Nimrod Mkono (Musoma Vijijini-CCM), aliiomba serikali kufuta mikopo kwa wanafunzi wa masomo ya sayansi ili wasome bure.
Mkono ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Mikopo alisema wakati umefika kwa serikali kutoa mikopo kwa wanafunzi wanaochukua masomo ya sanaa tu, huku wale wa sayansi wakisomeshwa bure bila kuangalia daraja.

Alisema nchi nyingi zinaendeshwa kwa mfumo wa sayansi na zimekuwa zikipata maendeleo ya haraka, lakini Tanzania wanafunzi wengi wanakimbilia masomo ya sanaa kwa sababu hakuna maabara.

Mkono alionyesha kushangazwa na wizara, ambayo inahusika na masuala ya sayansi lakini imejaa watendaji ambao si wanasayansi na hivyo kuonekana kama kichekesho kukuza sayansi.

Aliongeza kuwa serikali imejitahidi kujenga shule katika kila kata, lakini akahoji mara watakapohitimu
watakwenda wapi kwa sababu hakuna hata viwanda vya kuweza kuwaajiri kwani, vingi vinamilikiwa na wazungu
na wahindi ambao wanaviendesha kisayansi.
 
Wadau kuna Issue Kwenye Nipashe ambayo Inaelezea Wafanyakazi wa Serengeti Breweries Mwanza wagoma kwa Kuitwa Mbwa na Kulipwa Ujira wa Tshs 2000 a day, na kutopatiwa ajira ya kudumu.

Mwenye kuweza kuipata na kuipost itakuwa vizuri.
 
Ukiwashtaki halafu wakagundua kwamba hawana ushahidi wanaacha kukuandama. Siku hizi Manji wameachana naye baada ya kuwadai mamilioni.

That's the most ridiculous arguement I have ever heard for ages.Umeposema "ukiwashtaki halafu wakagundua hawana ushahidi wanaacha kukuandika" unaaminisha kuwashtaki MAHAKAMANI,au sio?Sasa ni kesi ipi iliyotolewa hukumu huko mahakamani kuonyesha magazeti hayo hayana USHAHIDI?Unaposema siku hizi wameacha kumwandika,nashawishika kuamini kuwa labda wewe si msomaji wa gazeti hilo coz had you been then ungegundua kuwa hao jamaa wameendelea kuwa consistent na kufuatilia ujambazi wa Manji.

Usiwe mvivu wa kufikiri.Hivi gazeti gani lina jeuri ya kuandika habari za biashara ya Mkapa akiwa Ikulu,helikopta feki kwa Wizara ya Ulinzi,skandali la Prof Mahalu,ishu ya Warioba,hili la Balali,Richmond,nk nk kama gazeti hilo halina uhakika na linachokiandika.

Changamsha ubongo wako kwa swali hili:hao wanaoshtaki Thisday na Kulikoni wanafanya hivyo ili kuyatisha magazeti hayo yaache kuwaandika au wanashtaki ili wapate haki yao (ie kama wamekashifiwa basi waombwe radhi/walipwe fidia au kama tumuma ni za kweli basi zithibitike mahakamani)?Swali la pili: hivi nikikukashifu halafu ukatishia kunishtaki then nikaacha kukukashifu,does that clean your name?Je kwa Thisday na Kulikoni kuacha kumwandika Manji (according to you) imesaidia kusafisha jina la Manji?

Tatizo hapa ni kuwa baadhi ya wenzetu wamezowea sana magazeti ya chama na serikali,Uhuru/Mzalendo na Daily/sunday News (kwa wale ambao lugha inapanda).Itachukua miaka mingi sana kabla wazembe hawa wa fikra kuelewa kuwa magazeti hayo ya chama na serikali yana kazi moja tu ya kusifia na kutetea maovu
 
Kwa mlio Bongo, masaa 48 nadhani yametimia, je kuna apology yoyote toka kwenye magazeti ya Kulikoni na ThisDay? Ninatamani sana kufahamu hatima ya mkwara wa Mh Mkono!

Ule mkwara cha mtoto tu.JK aliwahi kulichimbia mkwara jarida flani linalotoka UK (African Intelligence,kama sijakosea),akilitaka limwombe radhi within a certain time la sivyo atalipeleka mahakamani.Kisa kilikuwa habari kwamba Iran ilikuwa inamtumia Rostam Aziz kumsapoti JK ili once akipata Urais Iran iwekeze kwenye exploration ya uranium.

Baada ya mkwara wa JK journal hilo likasema halitaomba msamaha,na kama JK anataka kwenda mahakamani aende tu,nao wataenda kutoa ushahidi wao huko kortini.Kwani alienda?

Viongozi wachafu walikuwa wamezowea kulindwa na Uhuru/Mzalendo,Daily News na Sunday News,ambapo kilichoandikwa humo ni kuwasifia tu na kukariri hotuba zao za kitapeli.Wakifanya blunders inakuwa sio habari.Sasa wanaonjeshwa joto ya jiwe na Thisday na Kulikoni.Patamu hapo mwanangu.
 
Siku ambayo Mkono katishia kushitaki na barua kupeleka nakala katika magazeti (huko ndiko alikotumia kujisafisha) Bungeni likaibuka suala la City Water na Waziri Shukuru Kawambwa, akatoa data kwamba wamemlipa mamilioni Mkono.

Sasa aliandikwa na THISDAY kwamba amelipwa bilioni 8 na BoT, sasa hawezzi kubisha,, lakini je, akitokea mtu akasema anahusika katika kesi ya Rada atasemaje? Akitokea mtu akasema anahusika na TTCL atasemaje?

Akitokea mtu akasema anahusika na mikataba mingi mobovu wakati wa Utawala wa Mkapa na alifanya kazi za AG (Chenge) ambaye aliendelea kunywa bia zake pale Salander Club na Dodoma Hotel, huku Mkono akiendelea kuwa kama MWanasheria Mkuu anayelipwa mamilioni kwa jina la MTAALAM MSHAURI
 
Siku ambayo Mkono katishia kushitaki na barua kupeleka nakala katika magazeti (huko ndiko alikotumia kujisafisha) Bungeni likaibuka suala la City Water na Waziri Shukuru Kawambwa, akatoa data kwamba wamemlipa mamilioni Mkono... Sasa aliandikwa na THISDAY kwamba amelipwa bilioni 8 na BoT, sasa hawezzi kubisha,, lakini je, akitokea mtu akasema anahusika katika kesi ya Rada atasemaje? Akitokea mtu akasema anahusika na TTCL atasemaje? Akitokea mtu akasema anahusika na mikataba mingi mobovu wakati wa Utawala wa Mkapa na alifanya kazi za AG (Chenge) ambaye aliendelea kunywa bia zake pale Salander Club na Dodoma Hotel, huku Mkono akiendelea kuwa kama MWanasheria Mkuu anayelipwa mamilioni kwa jina la MTAALAM MSHAURI

Kaka halisi mbona unanitisha. maana kama kuna watu ninaweza kudanganywa nao kutokana na kuamini umakini wa habari zako ni wewe na wengine wacgacge mno humu. Sasa kama na wewe unakuja kuniambia kuwa hayo yote amehusika vitu ambavyo nilikuwa nakataa kama vina ukweli wowote sasa inakua kama kunyweshana maji ya muarobaini . Kupona unapona lakini uchungu wake si mchezo.

Tusubiri haya nayo kwa mkao wa pilau nini?

No wonder Mzee Mengi anaanza kufikiria jinsi ya kurithisha mali zake.

Lets hope we gonna find a light at the end of this crazy tunnel..

Tanzanianjema
 
No wonder Mzee Mengi anaanza kufikiria jinsi ya kurithisha mali zake
.

Kaka hii sijaielewa labda uniwekee katika PM kama unaona pagumu
 
Nani alisema Thisday wameacha kuandika mambo ya Nkono?

CAG`s audit queries on BoT: Ballali survives fiery Bunge interrogation

-Admits excessive payments in legal fees
-But not clear on gold mine company dealings

THISDAY REPORTER
Dodoma

BANK of Tanzania (BoT) Governor Dr Daudi Ballali was yesterday grilled for several hours by a parliamentary watchdog committee in Dodoma over allegations of funds mismanagement and misuse that have been hounding both him and the bank for several months now.

Among other things, members of the parliamentary finance and economic affairs committee asked Ballali to explain away excessive legal fees amounting to over 8bn/- that the BoT paid to one local law firm in the name of Mkono and Company Advocates for services rendered to the bank.

The governor was pressed upon to clarify on several key audit queries on the central bank accounts raised by the latest report of the Controller and Auditor General (CAG). Under the Bank of Tanzania Act of 2006, the CAG is a statutory auditor for the central bank.

Although the CAG's report gave the central bank a clean certificate of audit for the 2005/06 financial year, it also raised poignant question marks over a number of BoT payments made during the same period.

These include the more than 8bn/- in legal fees that had been paid to Mkono and Co. Advocates by June 30 last year for services rendered in relation to the long-running Valambhia case. Our sources say several members of the Bunge Committee, chaired by former cabinet minister Dr Abdallah Kigoda, pinned down Ballali on the matter and demanded a detailed answer.

The BoT supremo is said to have responded by acknowledging that the fees were indeed excessive, and assured committee members that the bank's management would discuss the matter with the law firm in question with a view to cutting down the ongoing payments.

He also managed to stave off committee questions on CAG queries with regard to payments from the central bank's external commercial debt account; the subject of a pending, deeper special audit ordered by the government at the behest of the International Monetary Fund (IMF).

However, according to our sources, Ballali was not so convincing on the subject of BoT's involvement with both Mwananchi Gold Company Limited and Meremeta Gold Mine Company Limited, which was also underlined in the CAG's report.

''The governor acknowledged to committee members that BoT is a shareholder in Mwananchi Gold, and extended a loan to that company on the basis that gold refining is an important activity for the national economy, and moreover the law governing central bank operations allows for such loans to be extended,'' said a reliable source.

But the source added that despite direct questioning from committee members, Ballali failed to explain clearly what Mwananchi Gold offered as collateral for the loan, or to identify who exactly are the company's other shareholders (apart from BoT).

''All he said was that the loan is fully secured�but there was no other explanation aside from that,'' the source said.

No representative from the National Audit Office was present at yesterday's session as committee members continued to delve deeper into the CAG's report on the BoT accounts.

The Bunge Committee's eventual endorsement of the report came on the heels of fresh reports that the deputy opposition leader in parliament, Dr Wilbrod Slaa (Karatu - CHADEMA), is getting set to table a private member's motion in the House for the formation of a parliamentary probe team to investigate the central bank.

The much-awaited special audit ordered by the government in tandem with the IMF is also in the process of selecting an international auditor able to meet the targeted deadline for conclusion of the exercise, announced as October this year.

According to recent THISDAY findings, the government has suspended all payments from the BoT's external payment arrears account pending the audit which, based on its terms of reference, will centre on assessing all transactions from the EPA account during 2005/06, as well as verification, monitoring, and control procedures related to the account.

The IMF on its part has also strongly recommended a 'safeguards assessment' of financial controls and management of resources at the BoT, which is to complement the planned special audit.

According to IMF policy guidelines, a 'safeguards assessment' is a diagnostic exercise carried out by IMF staff to ''help prevent the possible misuse of IMF resources and misreporting of information.''
 
Who the hell does Mnoko or Mkono or whatever the hell his name is think he is...?
 
Ina maana hawa This Day hawaogopi vitisho vya Nimrod Mkono? naona hawajipendi...

Wenzako sio waoga kama wewe. In fact, that is the reality of Bongo life...watu wanatishiana lawsuits kila siku magazetini na life moves on. It may surprise you, but here in Bongo not every squabble in the media, and not every negative story in the media, lead to death.
 
Kama Mkono altoa vitisho kwa nia ya kujiwekea ukuta tu akidhani kuwa umahiri wake wa sheria utafanya jamaa waache kumwandika hata kama wana data za kutosha, alifanya vibaya sana kisheria.

Mjini kwetu kuna mwanasheria mmoja alinyang'anywa leseni yake ya sheria kwa kutoa vitisho vya namna hiyo.
 
Back
Top Bottom