Nimsaidieje huyu mdogo wangu ana div four ya 26?

Nimsaidieje huyu mdogo wangu ana div four ya 26?

Access Denied

JF-Expert Member
Joined
Aug 10, 2012
Posts
655
Reaction score
210
Wanajamvi naomba mnisaidie kwa mawazo huyu ni mdogo wangu ameangukia division four ya point 26 na amefanikiwa kupata C mbili tu za chemistry na biology ila physics ana D na yeye ndoto zake ni kuendelea na form five kwa combination ya PCB na hapo tatizo ni kwamba hana credit 3 inabidi atafute nyingine na ameshikilia msimamo wake wa kuendelea na form five hataki kabisa chuo.
Sasa wasiwasi wangu huo upatikanaji wa hiyo credit moja na nimesikia siku hizi ku re-sit ni lazima kufanya masomo kuanzia 7 na cheti cha kwanza hufutwa, je ni kweli iko hivyo na kama ndo hivyo nimshauri nini mdogo wangu?
Naombeni msaada wenu wana jamvi ahsanteni sana.
 
Mshauri aende clinical officer ngazi ya diploma moja kwa moja kutokea form iv kwa matokeo yake hayo ndo qualification inayohitajika tangazo lipo jukwaa hili anaweza akarisit na akachemka vilevile akaenda advance akachemka short cut ndo hiyo
 
Mshauri aende clinical officer ngazi ya diploma moja kwa moja kutokea form iv kwa matokeo yake hayo ndo qualification inayohitajika tangazo lipo jukwaa hili anaweza akarisit na akachemka vilevile akaenda advance akachemka short cut ndo hiyo
Ahsante mkuu nitamshauri na hilo pia.
 
kwa matokeo ya mwaka huu huyo mbona anaenda A level kwa hizo c mbili? awe anapiga a level huku akirudia hiyo aliyofeli
 
Mbona kwa matokeo ya mwaka huu huyo mdogo wako inatakiwa umpe zawadi? Wala usiwe na wasiwasi watamchukua tu form five tena hata serikalini. Ni mwanamke/msichana?
 
Fanya hivi mnunulie ungo, nenda dukan nunua karanga na mifuko size ya kati rudi nyumban zikaange hzo karaga then zifunge hzo karanga kwenye hiyo mifuko! Tayari?

Ziweke kwenye ungo ulionunua,,, Mwambie azibebe hizo karanga aje nazo stendi! Mwambie akimbize kila gari linaloingia na kutoka awaambie watu waliomo kwenye magari karaga karaga karaga!


Wanajamvi naomba mnisaidie kwa mawazo huyu ni mdogo wangu ameangukia division four ya point 26 na amefanikiwa kupata C mbili tu za chemistry na biology ila physics ana D na yeye ndoto zake ni kuendelea na form five kwa combination ya PCB na hapo tatizo ni kwamba hana credit 3 inabidi atafute nyingine na ameshikilia msimamo wake wa kuendelea na form five hataki kabisa chuo.
Sasa wasiwasi wangu huo upatikanaji wa hiyo credit moja na nimesikia siku hizi ku re-sit ni lazima kufanya masomo kuanzia 7 na cheti cha kwanza hufutwa, je ni kweli iko hivyo na kama ndo hivyo nimshauri nini mdogo wangu?
Naombeni msaada wenu wana jamvi ahsanteni sana.
 
usijali ataingia kidato cha tano huyo,serikali itamchagua tu asiwe na wasiwasi.
 
Aende pale wizaran kwa Kawambwa na Mlugo watamwajiri hata kufuta na kupanga zile paper zenu kwa ajili ya kumbukumbu.WAHI NAFASI NI CHACHE NA MKO WENGI
 
Jinsi ninavyojua mm D ni Passed na kama Kemia na Biology ana C it means ana credit tayar yani PCB sa cjajua kama ile D ni kikwazo au vp lkn nijuavyo uwezo wa kusoma advance anao
 
Fanya hivi mnunulie ungo, nenda dukan nunua karanga na mifuko size ya kati rudi nyumban zikaange hzo karaga then zifunge hzo karanga kwenye hiyo mifuko! Tayari?

Ziweke kwenye ungo ulionunua,,, Mwambie azibebe hizo karanga aje nazo stendi! Mwambie akimbize kila gari linaloingia na kutoka awaambie watu waliomo kwenye magari karaga karaga karaga!
Huwezi kua serious [GOOGLE]
 
Umetaja masomo matatu tu,je masomo mengine amepata grades gani?Ni vizuri akarudia mtihani,maana hapo haujaweka hesabu Kiingereza na kiswahili amepata grades gani.
 
just tel her to relax coz 4 wat i think mwaka huu wanaweza kuchukua hadi four ya 26 lakini waziri alitangaza credit 3 xo asitarajie sana coz wanaweza wakazingua.
 
Huyo inaelekea mnamdekeza. Kwa matokeo yake hayo hatakiwi kuwa mtu wa kijafanya anachagua eti hataki chuo na lazima aende form five. Mtua ambaye ni lazima aendele form five ni yule aliyepata marks za kwenda form five, wengine wote ni LAZIMA wafanye maamuzi yaliyo compatible na matokeo yao. Msimdekeze huyo dogo mtamharibu. Yeye sasa anatakiwa kuwa mtu wa kusikiliza zaidi kuliko kujifanya mfanya maamuzi...
 
Back
Top Bottom