Nina Gari lenye Friji, natafuta kazi

Nina Gari lenye Friji, natafuta kazi

Nenda kagera, ukifika Bukoba ulizia Igabiro, kule hakuna mtandao kaandae mazingira ya kupata sato au sangara kwa bei ndogo hasa kipidi cha mvua hiki na gari yako upack bulumba ndio iwe center yako ya kukusanyia mzigo, hapo uhakikishe unapambana mwenyewe front usiagize mtu, vaa overroll ingia kazini na gloves zako za ngozi usichomwe na miiba ya samaki, soko direct utachagua Dodoma au Dar riverside pale hostel, hakikisha unakusanya mzigo wa kiwango na mabondo utauza huko huko, chapchap unakanyaga noti zako unarudi tena porini
 
Andaa vibali na leseni za kukuruhusu kukusanya mazao ya baharini au ziwani hapoumemaliza kazi
 
Ukishindwa nenda kilwa huko beba hata pweza ukanda ule ni wengi katafute connection pale feri kuna wapenda ukiungana nao mtapiga kazi vizuri pesa iko wazi kikubwa fanya utafiti wa kina zaidi kwenye maeneo yote na uwe na vibali na usiwe mpenda kulala hovyo kazi kazi na wewe
 
Au andaa meza yako nzuri kubwakubwa, nenda somanga huko ndanindani maana una gari tafuta machimbo ya samaki wa bahari hao, wanunue upange kwa bei na size uhakikishe unafika dar kuanzia saa tisa au kumi watu wakiwa wanatoka kazini, unaweza kua unazunguka kama machinga na meza yako unaweza kupaki mbagala unaangalia penye watu wengi una dogo mmoja wa. Kusaidia kuwakwarua wale samaki mteja akifika bei, utaona ulinunuaje huko na wewe utauza vipi unapiga naimanikufika saa mbili au tatu unamaliza mzigo, na unabeba samaki mixer madagaa yale na unauza bei ndogo ya faida lakini uwe kwenye mzunguko, lenga maeneo ya tegeta, mbagala, kimara, gongo la mboto na uhakikshe una vibali vyako hakuna kulala unaandaa mzigo wako kwa kiwango cha juu na usafi na bei iwe reasonable kwa hakika ilutaanza kuzidiwa na order za wateja,
 
Unajua Usipende kukaza ubongo kwenye Kila kitu..... Ndio maana mnatapeliwa sababu Kila kitu unawaza utapeli... Wewe kwenye ishu yangu hii unatapeliwa wapi? Gari yangu mm naomba tu kupata mawazo na connection ambazo huusiki au hata kama utanipa nikifika huko Hamna kupeana pesa Wala nn sana sana mm ndo labda ntapeliwe lakin mtu hata uwazi kwa kina unaenda kwenye vitu kama picha una doubt huo ni ujinga.... Wenye msaada wametoa mawazo Yao wamekausha ndio uungwana na tayar nshapata msaada lakin sio hizi pumba mnaleta nyie
Umensababisha nicheke..!!! Ukiweka kitu JF tegemea pumba, chuya, mawe, mchele etc..!! Kazi kwako kuchagua. La utapeli ilikuwa mfano tu..!! By the way ulishimndwaje kuweka picha ya gari yako, ukaweka iliyoko kwenye mnada? Na hata hujatoa caution kuwa umeitumia tu hiyo picha ili watu waelewe somo? Au hiyo ni yako wakati ikiwa huko?
 
Back
Top Bottom