Nina hamu ya ujasiriamali wa aina hii.

am a girl

JF-Expert Member
Joined
Nov 1, 2016
Posts
748
Reaction score
505
Naomba kujuzwa kuhusu kodi na makato yoyote pale ambapo ntaagiza bidhaa za urembo (accessories,nguo nguo,etc) kutoka nje mf. Kg X ni tshY, au mzigo wa tsh X vat rate ni Y, vitu kama hizo yani.

Pia kama kune sheria za kufata mziweke hapa, challenges zake pia tushee hapa tujuzane.

Na pia mnashauri kama nikianza hiyo biashara nianze na capital ya sh ngapi ambayo kidogo italeta return ya afadhali na risk ndogo.

Please wale ambao mna experience na wale ambao mnajua tujuzane hapa, ili tusiojua tufaidike.
 
Let say umeenda china kununua shati na kuja kuliuza
1. Gharama za manunuzi kwa shati hiyo ni 100/- hadi mzigo unaingia dukani
2. Then unaweka faida yako, let say Tshs. 30/-. kwa hiyo utauza Tshs 130/-
3. Serikali itakwambia usiuze bai hiyo ya Tshs 130/-, bali uongeze 18% (Tshs 24.3/-) ambayo ni VAT. Kwa hiyo mpaka hapo bei utakayotakiwa kuuza ni Tshs. 154.3/-
4. Hiyo 30/- unayopata kama faida, utatakiwa ulipe serikalini 30% yake kama corporate tax. Ambayo ni Tshs 5.4/-.
5. Hivyo katika bei ya 154.3/- utalipa serikalini Tshs 24.3 +5.4 = 29.7/-
6. Kwa hiyo kwa bidhaa uliyonunua kwa Tshs 100/-, ukaiuza kwa Tshs 154.3/- utabakiwa na 154.3-29.7 = 124.6/- NA HIVYO KUFANYA EFFECTIVELY UWE UMEPATA FAIDA YA TSHS 24.6/-

NB: Wakwepa kodi huwa wanabaki na hela yote yaani 154.3/- Tshs, badala ya 124.6/- Tshs (Wanatia ndani Corporate tax, na VAT waliyoikusanya.

VIle kama na wewe umenunua bidhaa ukapewa EFD risiti, baana yake itakusaidia kupunguza hiyo 18% ya VAT ambayo nawe umeilipa wakati wa manunuzi (VAT returns)

UELEWA WANGU UNAISHIA HAPO
 
hiyo VAT rate inategemea na cost ya bidhaa au?
 
No.4 - Itakua kodi ya 30% iwapo biashara hiyo ipo ndani ya kampuni.
 
Asante mkuu kwa kunielimisha hili

Karibu ndugu. Kama mtu anafanya biashara kwa TIN binafsi, TRA wanaangalia Total Income yake ni kiasi gani, halafu watapiga hesabu ya kodi yake ya mapato (Income Tax).

Kwa mwaka huu wa fedha 2016/2017 (Kwa mujibu wa Finance Act ya 2016), itakua kama ifuatavyo:

1. Kama mapato hakijazidi TSH 2,040,000/=, hatalipa;
2. Kama mapato yanazidi THSH 2,040,000/=, lakini hayazidi TSH 4,320,000/=, watachukua mapato (mfano TSH 3,050,000/=) watatoa TSH 2,040,000/= [3,050,000 - 2,040,000 = 1,010,000/=]. Hapo atalipa 9% ya jibu letu (1,010,000 * 9/100).

n.k.
 
Kitu ambacho kinacho nishangaza nchi hii mtu ndio kwanza unaaza biashara unalipishwa tax
Wenzetu nchi za ulaya, hulipi tax kwa mwaka wa mwanzo, inategemea na biashara yako itakavyo run,kama faida ndogo tax unarudishiwa ikiwa utalipa, wameweka earning ya mwaka ya biashara yako,na mtaji wako. Alimuradi mtu aweze kuwa na ajira uweze kujikimu maisha yako, serikali haipo kukukandamiza, ipo ku kusaidia.

Sasa hapa kwetu huu mfumo sijui tumetoa wapi, ndio maana tunazidi kuwa masikini siku hadi siku.

Hata kwenye kazi ndio hivyo hivyo, ukilipa tax ,kama income yako lower unarudishiwa mwisho wa mwaka tax yako.
 
Yani kweli kabisa mmmh.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…