Nina makovu yaliyobaki kwenye kichwa cha uume

Nina makovu yaliyobaki kwenye kichwa cha uume

Status
Not open for further replies.
nunua dawa ya meno ile ya whitedent herbal siku nne hazifiki kwisha kabisa
 
Habari zenu, natumaini wote ni wazima. Ninaomba mawazo yenu juu ya swala langu.

Mwishoni mwa mwezi wa name nilianza kupata vipele mfano wa malengelenge katikati ya vidole vya miguuni, upele ulivyokua unaanza haukua na muwasho lakini baada ya siku kadhaa muwasho ukaanza haswa wakati wa usiku, vipele vikasambaa na mikononi pia katikati ya vidole, na kimoja kikatoka kwenye kichwa cha uume, sikukigundua kwasababu hakikua na maumivu ila muwasho ulikuwepo kwenye uume ndo ulifanya nije kukiona.

Kuna siku moja nilienda kukojoa nikahisi maumivu, ikanibidi niende dispensery siku hiyohiyo nikapimwa na kukutwa na UTI maumivu yale yalikata lakini siku hiyo hiyo bila hata kuanza kutumia dawa.

Baada ya muwasho kuendelea kua mkali ikabidi niende hosp tena kumuelezea doc kuhusu vipele akaniandikia antibiotics na dawa ya kupaka pamoja na sabuni ya kuogea. Naweza kusema vilinisaidia kidogo kukausha vipele ila sio kupunguza muwasho mwilini na vipele japo kua vilikua vinakauka viliendelea kutoka.

Nilienda hosp tena kuhusu kipele cha kwenye uume maana kilikua kinanipa wasiwasi kwasababu hakiumi kipo tu ila kinatoa maji kikipasuka ila hakikutengeza kidonda. Nikapima HIV, kipimo cha damu pamoja na Syphilis lakini vyote vikawa negative. Kipele kilikua kimeshaanza kupona sijajua ni kwasababu ya antibiotics au ni ile cream ya kupaka.

Baada ya siku kadhaa tu kikauka na kuweka gamba juu ambalo nililitoa na ndo imebaki sehemu ya ngozi iliyonyanyuka ni kama kovu kama mtavyoona kwenye picha.

Naombeni kujua inaweza kua ni nini hii au nawezaje kuondoa kovu. Kuna doctor Regency hosp alinambia hii ni Scabies Kuna maktari wengine wa hosp nyingine hawakunambia ni nini ila walinipa dawa acyclovir ambazo hazijanisaidia chochote kwenye kupunguza muwasho wala vipele sehemu nyingine, ila nimeanza kutumia scaboma jumatatu iliyopita.

View attachment 2765547View attachment 2765548View attachment 2765549
Mkuu,

Kwanza pole sana.

Pili, mimi nitadili na tatizo kwenye uume. Ninachoona siyo kovu, bali ni vipele vibichi bado. Sijafahamu ilivyokuwa inaonekana hapo kabla unapodai kabla ya kukauka.

Tatu, umejitahidi sana kuelezea. Ila hujatoa muhtasari wa historia kabla ya tatizo kukupata. Lakini pia, hujaeleza alichokiona daktari baada ya kufika hospital.

Ukienda tena, kabla ya daktari kukupa dawa analazimika kukueleza tatizo linalokusibu. Hii ni muhimu sana kujumuishwa kwenye historia ya maradhi na matibabu yako tarajali. Na pengine ungeeleza ingesaidia kufikia hitimisho lenye mafanikio.

Nne, wataalam wa Regency kusema Scabies bila shaka ni kutokana na vipele miguuni na katikati ya vidole venye kuwasha.

Aciclovir ni antiviral, itumikayo kupunguza kuenea kwa magonjwa kadha wa kadha. Kwa minajili ya tatizo lako basi ni kwa ajili ya Genital Herpes. Hivyo ndiyo kusema, hao wa hospital nyingine waliona una herpes.

Tano, kwa kuangalia ninaweza kusema ni Herpes. Ili kujihakikishia kama ni Herpes basi inakubidi ufanye vipimo, HSV PCR. Hii itatoa majibu sahihi zaidi juu ya ugonjwa wenyewe.

Sita, Herpes hazina tiba. Hivyo hata kama majibu yatatoka positive basi dawa ya kuziondoa kabisa hakuna.

Kuhusu dawa ulizopewa endelea kuzitumia. Ili upate nafuu kwenye muwasho mwilini.

Nakutakia uponyaji mwema.
 
Shukrani Dr Restart
Nilikutana na daktari wa ngozi akanielezea vizuri kuhusu tatizo langu, Ni Scabies inatabia ya kutoa viupele sehemu mbalimbali za mwili hadi kwenye genitals kwasababu wanapendelea sehemu laini.

Kuhusu Herpes
Hapana, sipo sexual active kwa miaka zaidi ya miwili sasa na nilifanya vipimo vyote vya magonjwa ya zinaa hadi herpes na majibu yalikuja negative.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom