Nina milioni 10 Nataka kuwekeza...

Fuqin

JF-Expert Member
Joined
Dec 2, 2018
Posts
306
Reaction score
625
Natumaini muko powa kabisa... nina milioni 10 hapa ambayo nimeikusanya kutoka katika biashara yangu ya Nafaka nafikiria kufungua tigopesa hapahapa kwenye duka la Nafaka... sasa ambao munaijua biashara hii kwa pesa hii nitapata faida bei gani kwa mwezi??? ni hayo tuu
 
Wazo ni zuri na biashara pia ni nzuri, jambo la msingi tafuta mtu sahihi wa kusimamia hiyo biashara na jitaidi kuweka laini zote mana, kisha uje utupe mrejesho hapa baada ya miezi nane.
 
Mkuu mimi nimewekeza kwenye mikopo. Nakopesha kwa riba ya 20% kwa wiki.
Vitu vinawekwa bondi vyenye thamani kubwa ndio nakupa hela yangu. Maandishi Muhimu pia
 
Wazo ni zuri na biashara pia ni nzuri, jambo la msingi tafuta mtu sahihi wa kusimamia hiyo biashara na jitaidi kuweka laini zote mana, kisha uje utupe mrejesho hapa baada ya miezi nane.
nina sehem ya cashier hapa kwenye duka la mazao ndo nataka hapahapa niweke na tigo pesa yaani 2 in 1
 
Mkuu mimi nimewekeza kwenye mikopo. Nakopesha kwa riba ya 20% kwa wiki.
Vitu vinawekwa bondi vyenye thamani kubwa ndio nakupa hela yangu. Maandishi Muhimu pia
Dini yangu hairuhusu mambo ya Riba
 
Naomba abc ya biashara ya nafaka mkuu.
nafaka aina gani una deal nazo na kutokea wapi
Nafaka zote isipokuwa mchele na maharage... kila nafaka ina mkoa wake mimi naletewa na wakulima nauza dukani kwa jumla
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…