Nina mill Tshs milioni 20, naomba ushauri wa mradi wa kufanya

Nina mill Tshs milioni 20, naomba ushauri wa mradi wa kufanya

Tafuta ardhi ya isiyopungua ekari 10, Chimba kisima cha maji ili uwe na uhakika wa maji,jenga na kijumba cha kidogo cha kufikia au vibarua,anzisha mradi wa kilimo cha umwagiliaji cha mbogamboga na ufugaji wa kuku wa kienyeji (anza na kuku 100).
Uzuri wa miradi ya kilimo na ufugaji hakuna cha kulipia kodi
 
Thanks, VP mradi wa kufungua mashine na kusaga na kukoboa nafaka mnauonaje?
 
Thanks, VP mradi wa kufungua mashine na kusaga na kukoboa nafaka mnauonaje?

Wazo zuri,baba yangu alikuwa moja kati ya watu wa kwanza kuanzisha mradi huo kigamboni... Alinipa kama wiki mbili niusimamie kucheki kinachoingia,pesa iliyokua inaingia siku pakikaa vibaya anachukua elfu thelathini naa... Siku ikikaa vema elfu tisini,hakika mradi huu ukiuweka sehemu nzuri hutajuta.
 
Motor za mashine za nafaka kama mahindi zinazotumia Umeme zinauzwaje pamoja na vinu vyake?
 
fungua duka la hardware i mean uza vifaa vya ujenzi na umeme utakuja kuniambia.vinalipa sana halafu haviozi expire date ni zaidi ya miaka mitano mbele,
 
Najaribu kuangalia ni mradi gani naweza kuuanzisha kwa kiasi hicho nashindwa, naombeni ushauri, eneo nilipo kuna Umeme ,maji na Huduma zingine

Mkuu, mimi nilifungua duka la spare kwa mtaji wa 15m miaka miwili iliopita. Sasa hivi nina mtaji approximately 80m na turn over kwa mwezi btn 12-15m. Ila naomba nikufahamishe magari na spares nazijua vizuri sana ila biashara nimejifunza baada ya ku fail kwenye biashara kadhaa.

Inahitaji nidhamu ya hali ya juu,kila hela unayoipata unairudisha kukuza mtaji,bado nafanya hivyo. Tatizo watz wengi wakifanya biashara tu wanaanza kujenga,kununua magari ndio maana biashara hazikui.

Uwe na malengo,usikate tamaa na nidhamu ya hali ya juu.
 
nenda pale hongera bar au ambiance tafuta mke uoe, wanasema to every succeful man there is woman behind him
 
Mimi nipe laki 5 tu na kila mwezi nitakurudishia laki 250 000 kwa miezi mitatu na utajifunza biashara kupitia kwangu
 
Ndugu mm nalima morogoro, toa pesa tushirikiane kwenye kilimo hautokaa shamba utakuwa unakuja kukagua mradi mm ndio nitakua shamba
 
Mkuu, mimi nilifungua duka la spare kwa mtaji wa 15m miaka miwili iliopita. Sasa hivi nina mtaji approximately 80m na turn over kwa mwezi btn 12-15m. Ila naomba nikufahamishe magari na spares nazijua vizuri sana ila biashara nimejifunza baada ya ku fail kwenye biashara kadhaa.

Inahitaji nidhamu ya hali ya juu,kila hela unayoipata unairudisha kukuza mtaji,bado nafanya hivyo. Tatizo watz wengi wakifanya biashara tu wanaanza kujenga,kununua magari ndio maana biashara hazikui.

Uwe na malengo,usikate tamaa na nidhamu ya hali ya juu.

una point nzuri sana mkuu ..
 
Mkuu umezipataje hizo milioni 20? Tujuze ili tuweze kutoa ushauri zaidi.
 
Back
Top Bottom