Nina mpango wa kuanza kuuza vifaranga vya kuku vya siku moja hadi mwezi. Hii ni biashara nzuri?

babampigi

JF-Expert Member
Joined
Mar 19, 2013
Posts
364
Reaction score
312
Habari zenu wakuu. Kama kichwa cha habari kinavyosema nime order incubators 3 zenye ujazo wa 6,336 ingine 4,224 na 3,520 zinakuja na Hatchers zake pia nime order hatcher peke yake ya mayai 3500.

Naanza kutotolesha vifaranga wa aina zote Kama Cross breed, Black/white Australorps, kroiler, Red hamshire, Rhode island red, Sussex na wengine.

Nachohitaji ni upatikanaji wa mayai bora ya kutotolesha. Machines zinaingia October mwanzoni nitaanza machines zikifika tu nitakuwa Mbezi beach..

Je soko la vifaranga likoje kwa Dar? Naomba ushauri/muongozo wowote asanteni sana.
 
Kwema mkuu? Naona wadau hawajaona uzi wako

Hapo mkuu ni kupambana kutafuta wateja "BIASHARA MATANGAZO" jitahidi kufanya matangazo ya biashara yako hakika utapata tu wateja naamini demand ya kuku ni kubwa sana, wazo la nyongeza unaweza ukawa unafuga pia na wewe kuku kiasi yani uwe unapata faida kwenye kutotolesha na kwenye kufuga, all the best mkuu.
 
Hivi hayo mayai ya matabaka yote uliyoyataja yanauzwa wapi?
 

Kwema mkuu, nashukuru sana ndio pia niko kwenye process ya kujenga mabanda. Sema for the first few months nataka ni concentrate na kutotolesha na kuuza vifaranga.. Nashukuru Sana kwa ushauri wako
 
Hivi hayo mayai ya matabaka yote uliyoyataja yanauzwa wapi?

Since umekuja kishari Shari nitakujibu hivyo hivyo.. Unadhani naweza nunua incubators za kutotolesha vifaranga zaidi ya 14,000 bila kufanya research ya kupata mayai? Kama huna jibu au hujui kilicho ulizwa ungeweza pita kimya kimya tu
 
Samahani boss wangu kwa swali la kishari Shari ...Sina maana mbaya ila jukwaa hili ni sehemu ambapo kila mtu anaongea chochote na kuuliza chochote ilimradi asivunje sheria za jf kwa uzi wako huu mwenzio nimechungulia fursa hivyo nikauliza kujua mayai yanapatikana wapi ili kujua tu na sio vinginevyo I beg your pardon my brother
Since umekuja kishari Shari nitakujibu hivyo hivyo.. Unadhani naweza nunua incubators za kutotolesha vifaranga zaidi ya 14,000 bila kufanya research ya kupata mayai? Kama huna jibu au hujui kilicho ulizwa ungeweza pita kimya kimya tu
 

Your excused mkuu, ni vyema tuelimishane mie mwenyewe ndio kwanza machines hazijaingia nafanya more research kujua nini ni kina manufaa zaidi.. Nitakuwa nashirikiana na mdogo wangu pia.. Kuna jamaa yuko Mbeya anauza mayai ya mbegu zote hizo, na pia kuna dada yuko Tabata anauza hadi mayai ya bata mzinga( turkey)
 
Since umekuja kishari Shari nitakujibu hivyo hivyo.. Unadhani naweza nunua incubators za kutotolesha vifaranga zaidi ya 14,000 bila kufanya research ya kupata mayai? Kama huna jibu au hujui kilicho ulizwa ungeweza pita kimya kimya tu
Umefanya Research ukapata wapi?

Hahaha nikushauri tu tengenexa Parebts wako na anza kutotolesha mayai kutokana na kuku wako vinginevyo jiandae kuuziwa hata ya layers yadio kuwa na mbegu.

Hizo breeds unazo zitaja hapa kaka Light Susex au hata Red Rhodes na wakina New Hampshire maana yake lazima U import mayayi kutoka Nje sabs sana sana South Africa au Ulaya hapo ndo kuna Parents stock wa hizo breeds.

Tanzania hapa utauziwa vitu ajabu tu.

Na Kuwa na Parents stock wako ndo kitu muhimu na kuwapata Pure ni lazima kuagiza nje kuagiza nje ni lazima.kuwa na vibali kutoka wizaraya mifugo vinavyo kuruhusu kuingiza nchini mayai.

Na lazima yaje kwa ndege. bila vibali pale airport wapasua yote unless

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Asante mkuu nimekuelewa sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…